TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, February 24, 2012

Serikali yawaagiza wakaguzi wa ndani wa hesabu kuhakikisha kuwa matokeo ya utekelezaji wa miradi yanalingana na thamani ya fedha iliyotolewa

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Ramadhan Khijjah akifungua mkutano wa siku tatu wa wakaguzi wa ndani wa Sekretarieti za mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa leo jijini Dar es salaam wenye lengo kuwaelimisha juu ya marekebisho ya Sheria ya Fedha Sura 348 ya juni 2010 yaliyopelekea Wizara ya Fedha kuanzisha Idara ya Mkaguzi wa Ndani wa Serikali(Internal Auditor General Division) ambayo pia inajukumu kusimamia na kuboresha ukaguzi wa ndani kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa na Sekrietarieti za Mikoa.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Ramadhan Khijjah na baadhi ya wakaguzi wa ndani wa Sekretarieti za mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa baada ya ufunguaji wa mkutano wa siku tatu wenye lengo kuwaelimisha juu ya marekebisho ya Sheria ya Fedha Sura 348 ya juni 2010 yaliyopelekea Wizara ya Fedha kuanzisha Idara ya Mkaguzi wa Ndani wa Serikali(Internal Auditor General Division) ambayo pia inajukumu kusimamia na kuboresha ukaguzi wa ndani kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa na Sekrietarieti za Mikoa ulianza jana jijini Dar es salaam.
Na Tiganya Vincent-MAELEZO-Dar es salaam
Serikali imewaagiza wakaguzi wa ndani wa Sekretarieti za mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha kuwa hesabu za miradi yote ya maendeleo katika maeneo yao ya kazi inakaguliwa ili kuhakikisha kuwa inatoa matokeo mazuri yanayolingana na thamani ya fedha kwa matumizi yanaliyofanywa.
Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar es salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Ramadhan Khijjah wakati akifungua mkutano wa siku tatu wa wakaguzi wa ndani wa Sekretarieti za mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa.
Mkutano wa siku tatu wa wakaguzi wa ndani wa Sekretarieti za mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa unalenga kuwaelimisha juu ya marekebisho ya Sheria ya Fedha Sura 348 ya juni 2010 yaliyopelekea Wizara ya Fedha kuanzisha Idara ya Mkaguzi wa Ndani wa Serikali(Internal Auditor General Division) ambayo pia inajukumu kusimamia na kuboresha ukaguzi wa ndani kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa na Sekrietarieti za Mikoa.
Alisema kuwa ni wajibu wa wakaguzi kuanzia serikali kuu hadi Serikali za mitaa kuhakikisha kuwa miradi zaidi ya maendeleo inakaguliwa na taarifa kuifikia Wizara ya Fedha mapema ili hatua muafaka ziweze kuchukuliwa kwa lengo la kuboresha dosari zinazojitokeza ili miradi inayopelekwa katika jamii inasaidia e kuleta maendeleo yaliyokusudiwa na wananchi.
“Ni wajibu wenu katika kuongeza uwajibikaji na uwazi katika usimamizi wa matumizi ya rasilimali za umma , ili Serikali iweze kupata thamani ya fedha zinazotumika na kuboresha huduma kwa jamii “ alisema Khijjah.
Aidha Katibu Mkuu huyo aliwaagiza kuwa wakaguzi hao wa ndani kujielimisha zaidi kwa kusoma miongozo mbalimbali ya ukaguzi wa ndani na namna ya kuweka kumbukumbu vizuri ili kufanya kazi ya ukaguzi katika viwango vinavyokubalika kitaifa na kimataifa.
Alisema kuwa hatua hiyo itawasaidia kuwa watendaji wazuri na wanaotoa taarifa zinazoonyesha ukweli halisi wa matumuzi ya fedha na rasilimali za wananchi kwa ajili ya maendeleo yao na Taifa kwa ujumla.
Khijjah alisema kuwa Serikali ilianzisha Idara ya Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali kupitia marekebisho ya Sheria ya Fedha Sura 348 yaliyopitishwa na Bunge Juni ,2010 kwa lengo ya kuimarisha utendaji na uwajibikaji katika udhibiti na usimamizi wa matumizi ya rasilimali za umma na utawala bora.
Mkutano

Waziri wa wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu usitishwaji wa matangazo ya Televisheni kwa kutumia Technolojia ya analogia na kuhamia teknolojia ya utangazaji ya dijitali ambao utasitishwa rasmi tarehe 31 Disemba mwaka 2012 saa sita kamili usiku. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dk. Frorens Turuka.
(Picha na Anna Itenda - Maelezo)

World class football stars made the dreams of four lucky football fanatics from across East Africa come true in the GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ Celebrity Finale last night and football icon Jay Jay Okocha showed why he is ‘so good they named him twice’ as he helped his partner hit the jackpot and win USD50K!
The episode kicked off with the four footballing heroes, Jay Jay Okocha, Marcel Desailly, Rigobert Song and Kalusha Bwalya, stepping out onto the pitch to pick their team mate. The Tanzania nation waited with baited breath to see which excited top scorer from the GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ mobile phone game got partnered with each celebrity footballer as they together took on the challenge to a life changing some of money.
It was Kenyan businessman James Nderitu from Nairobird who bagged Nigerian football icon Jay Jay and together went on to win USD50K. James has succeeded in business, succeeded in being partnering with a world class hero and succeeded in winning the Celebrity Finale! Speaking of his epic win, James said, “Winning makes me feel on top of the world – the whole experience, starring in the show and meeting Jay Jay – has been is a real dream come true.”
In classic hero style, Jay Jay gallantly donated his share of the winnings to the other three contestants in recognition of their incredible efforts on the show, so they took each took home just over USD8K .
Commenting on his experience of taking part in the show, Jay Jay said: “It was an incredible experience to be a part of, meeting the contestants, the audience and the hosts. This episode was filled with everything - drama, tears and laughter. Taking part you feel an amazing pressure, something that I did not expect to feel out on the GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ pitch. I am delighted that I came through for my team mate, he put in a great performance too and hitting the final target on the Guinness® Money Wall meant we secured a truly life changing amount of money for him.”
Together the duo saw off tough competition, so who are the other knowledgeable football fans that are now the envy of football lovers across East Africa?
  • The top scorer from the East Africa region was ICT officer, George Otieno from Mombasa who was paired up with his dream football partner, former French international, Marcel Desailly
  • Stepping up to represent Tanzania was bachelor of commerce and Liverpool FC fan, Hance Kimola from Kinondoni, Dar Es Salaam who was teamed up with his ultimate football hero, former Cameroonian international, Rigobert Song
  • Back for a second time and ready to show off his knowledge on behalf of Uganda was radio journalist, Patrick Ogua from Arua, who was standing alongside Zambia’s great ever footballer, Kalusha Bwalya
All four contestants battled the mobile phone game leader board and demonstrated that they knew the offside rule from the free kick rule and their Pele from their Ronaldo, but in this Celebrity Finale it was the chance for their football heroes to take centre stage as they went head-to-head on the physical challenges to see if they could get their partners to the final round.
The footballers were on fire throughout the episode with some incredible displays of skill, some closely fought rounds and some extravagant celebrations from former Cameroonian international Rigobert Song. But it was James and Jay Jay who worked together to see off the other teams and secure themselves the chance to take on the Guinness® Money Wall.
The Guinness® Money Wall had defeated many teams throughout the series, but the question on everyone’s lips was, would a member of Nigeria’s ‘Dream Team’ have the skill to beat the wall?
It was a fantastic team effort for the duo with James correctly answering all the questions and Jay Jay demonstrating some phenomenal skill as he worked his way up the targets. The tension in the studio was immense when they had one target left and just one final ball. And as you would expect, Jay Jay delivered and hit the target when it counted, securing the pair the jackpot and earning himself the honour of being the first ever player on the show to hit target six!
Please remember to drink responsibly – 18+.

Balozi wa kinywaji cha Redds Original Akimkabidhi kifurushi cha zawadi mbalimbali Mkurugenzi wa kampuni ya ASSET Intateiment Asha Baraka kwaajili ya maadhimisho ya kipindi cha siku ya wapendanao Duniani

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri masuala ya Jumuiya ya Madola, Umoja wa Mataifa na Afrika na Mazingira ( Parliamentary Under Secretary responsible for Africa, United Nations, economic issues, conflict resolution, and climate change) wa Uingereza Bw Hendry Bellingham wakishuhudia Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh Bernad Membe akiweka saini sambamba na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza William Hegue kuhusu makubaliano kati ya nchi hizo mbili juu ya taratibu za kukabadhiana watuhumiwa wa uharamia na mali zilizokamatwa katika matukio ya uharamia katika bahari kuu leo February 23, 2012 Lancaster House, London. (PICHA NA IKULU)
Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh Bernad Membe akiweka saini sambamba na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza William Hegue wakibadilishana hati za mikataba mara baada ya kusaini.

Mchezaji Ilunga (kushoto)wa Jamhuri ya Kiodemokrasia ya Congo akichuana vikali na mchezaji Hussein Javu wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars wakati wa mchezo wao wa kirafiki unaofanyika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam jioni hii. Mchezo huo ulikuwa ni kwa ajili ya kujipima nguvu kabla ya mapambano ya timu hizo kuwania kufuzu fainali za kombe la mataifa ya Afrika nchini Afrika Kusini, ambapo Taifa Stars itakutana na Msumbiji na RDC Congo itakutana na Sychelies, mpaka mpira unamalizika hakuna timu iliyopata goli hivyo matokeo ya timu hizo mpaka mwisho yamekuwa 0-0 kwa timu zote.
Kocha wa timu ya Taifa Stars Jan Paulsen akimuelekeza jambo Aggrey Morris mchezaji wa timu hiyo kabla ya mchezo huo kuanza kwenye uwanja wa taifa.
Wachezaji wa Timu ya RDC Congo na Taifa Stars wakisalimiana kabla ya mchezo huo kuanza kwenye uwanja wa taifa.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili Lancaster House jijini London jana February 23, 2012 kijiunga na viongozi wa nchi mbalimbali katika mkutano wa kujadili mstakabali wa nchi ya Somalia ambayo imekuwa katika misukosuko kwa zaidi ya miaka 20 ambapo jumuiya ya kimatifa ikiongozwa na Uingereza imepania kumaliza matatizo mbalimbali katika nchi hiyo ikiwemo kutokuwa na serikali inayoeleweka, uharamia, ugaidi pamoja na kujaribu kurudisha amani.
PICHA NA IKULU
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili Lancaster House jijini London jana February 23, 2012 kijiunga na viongozi wa nchi mbalimbali katika mkutano wa kujadili mstakabali wa nchi ya Somalia

MUIGIZAJI filamu nyota nchini, Charles Magali maarufu kwa jina la Mzee Magali, atachezesha mechi ya soka ya kuamua mbabe kati ya wasanii wa vichekesho wa Dar es Salaam na Mwanza katika Uwanja wa CCM Kirumba. Kwa mujibu wa mratibu wa mechi hiyo iliyoandaliwa na Kampuni ya Brayance Promortes, Pearson Samwel, Mzee Magali amechaguliwa kuwa mwamuzi baada ya kupendekezwa na wasanii wa pande zote. “Mzee Magali amekuwa kivutio kikubwa kwa wasanii wa Mwanza na hata nilipowaambia wachekeshaji wa luninga wa Dar es Salaam kwamba refarii atakuwa msanii huyo, wamefurahi sana,” alisema Samwel. Alisema kuwa nyota huyo wa filamu nchini amekubali kupuliza filimbi katika mechi ya kumaliza ubishi juu ya wasanii gani wanaweza kusakata soka kati ya wa Dar es Salaam na Mwanza ‘rock city’. Samwel alisema kuwa viingilio katika mechi hiyo itakayochezwa Machi 3, mwaka huu, vitakuwa sh. 5,000 katika jukwaa kuu na sh 2,000 mzunguko. Mratibu huyo ameongeza kwamba, kampuni inayoratibu mechi hiyo ipo katika mchakato wa kutafuta mgeni rasmi. Wasanii kutoka Dar es Salaam watakaoshuka uwanjani ni Kingwendu, Sharo Milionea, Mboto, Senga, Pembe, Bambo, Mtanga, Mau, Ringo na Chilly. Wengine Defender, Zimwi, Muhogo Mchungu, Masele, Erick, Kiuno na Hawa, ambao watawasili Mwanza mwishoni mwa mwezi huu kujiandaa kucheza na wapinzani wao. Timu ya wachekeshaji wa Mwanza inaundwa na Babu Mkombe,Sharobaro wa Kihaya, Mchele, Chugu, Ngosha, Brother K, Mama Brandina, Msimbe wa ukweli,Okech Okech, Kafuku Kaukananga, Mzee Dude, Itagata, Malapulapu, Choko na Tengambili. Wasanii wengine watakuwepo siku hiyo ni Tatu Mkate wa Arusha, Avodia Tolu, Mrefu kwenda chini na Jully Tax, ambao wamepania kuwafunga wachekeshaji wenzao wa Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Samia Suluhu Hassan akipata Maelezo Kuhusu Upakuwaji wa Makontena katika Bandari ya Zanzibar kwa Mkuu wa Mipango{ZPC]Ali Haji Haji wakati wa Ziara yake yakutembelea Miradi ya Maendeleo, Kulia Kaimu Mkurugenzi wa Bandari Bw Msanifu Haji Mussa na Maofisa wa Bandari ya Zanzibar[Picha na Ali Meja]

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Emmanueli Nchimbi (kulia) akizungumza na Rais wa Kituo cha Utamaduni na Uhusiano wa Kiislam kutoka nchini Iran Dkt. Mohammed Basheir Khurrqmshad (kushoto) mara baada ya kuwasili katika Ofisi za Wizara hiyo leo jijini Dar es salaam. Pamoja na mambo mengine Rais huyo ameahidi kuendeleza ushirikiano kati ya Tanzania na Iran katika sekta ya utamaduni na michezo ikiwemo kusaidia kuleta makocha wa mchezo wa riadha. (PICHA NA ARON MSIGWA WA MAELEZO)
Benjamin Sawe na Ismail Ngayonga
Kitengo cha Habari
WHVUM.
Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Dk. Emmanuel John Nchimbi ameishukuru Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa kuanza utekelezaji wa kupatiwa kocha wa mchezo wa riadha ikiwa ni mkataba wa ushirikiano baina ya nchi hizo mbili.
Dk. Nchimbi aliyasema hayo (leo) alipokutana na Waziri wa Utamaduni na Muongozo wa Kiislamu wa Iran Dk.Mohammad Bagher Khurramshad jijini Dar es Salaam ambapo alisema hatua hiyo ni moja ya utekelezaji wa mkataba wa ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Iran.
Alisema nchi ya Iran imekuwa ni moja kati ya nchi yenye makocha bora na wenye uzoefu katika mchezo wa riadha kwa miaka mingi na kusema ni wakati muafaka kuichangamkia ofa hiyo.
“Nchi ya Iran ina makocha bora wa mchezo wa mbio za riadha sasa ni wakati muafaka kwa Chama cha Mchezo wa Riadha kuichangamkia ofa hii ili mchezo huu uweze kuiweka nchi katika ramani ya michezo duniani’’.Alisema Dr. Nchimbi.
Kwa Upande wake Waziri wa Utamaduni na Muongozo wa Kiislamu wa Iran Dk. Khurramshad alisema Iran itaendelea kuisaidia Tanzania katika sekta ya Michezo,Utamaduni na Sanaa ikiwa ni kuboresha uhusiano baina ya nchi hizo mbili.
“Huu ni mwanzo tu wa makubaliano ya mkataba lakini tutaendelea kuisaidia Tanzania katika sekta za utamaduni na sanaa kama tulivyokubaliana katika mkataba baina yetu”.Alisema Dr.Khurramshad
Serikali ya Tanzania na Jamhuri ya Kiislam ya Iran mwezi uliopita zilitiliana saini mkataba wa ushirikiano katika sekta za Utamaduni na Sanaa ambapo kwa upande wa Serikali ya Tanzania iliwakilishwa na Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Dr. Emmanuel Nchimbi na upande wa Jamhuri ya Kiislam ya Iran iliwakilishwa na Waziri wa Utamaduni na Muongozo wa Kiislamu Dk.Khurramshad.
Katika mkataba huo uliosainiwa Jijini Tehran moja kati ya makubaliano ni pamoja na ushirikiano katika sekta ya Utamaduni na Sanaa ambapo Serikali ya Tanzania iliombwa na ilikubali kuandaa Wiki ya Utamaduni wa Tanzania nchini Iran.

Wizara ya Maliasili na Utalii inatoa taarifa kuwa Tanzania itakuwa mwenyeji wa Kongamano la Kwanza la Africa kuhusu Uendeshaji, Changamoto na Fursa katika Uhifadhi wa Mbuga za Wanyamapori na Maeneo yaliyohifadhiwa (The 1st Pan-African Conference on Sustainable Tourism Management In National Parks and Protected Areas: Challenges and Opportunities).
Kongamano hilo la siku Tano limepangwa kufanyika katika Kituo ya cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) tarehe 15 hadi 19 Oktoba 2012. Washiriki wapatao 300 kutoka nchi mbalimbali wanatarajia kuhudhuria.
Tanzania imeteuliwa kuwa mwenyeji wa Kongamano hilo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii Duniani (UNWTO) kufuatia mkutano wake (UNWTO General Assembly) ambao ulifanyika nchini Korea 2011. Katika Mkutano huo Tanzania pia ilichaguliwa kuwa mjumbe katika Baraza la Utendaji (Executive Council) la Shirika hilo, nafasi ambayo itakuwa nayo hadi mwaka 2015.
Kongamano hilo la Oktoba 2012 ni la kwanza na la aina yake litawakuwakutanisha wahifadhi na wadau wa sekta ya Utalii ili wajadili namna ya kufanikisha uhifadhi na utalii duniani. Tanzania imepata fursa ya kuwa mwenyeji wa Kongamano hilo kutokanana na sifa nzuri na uzoefu ilio nao katika kuanzisha na kuendeleza hifadhi za Taifa.
Tanzania inategemea kupata manufaa kutokana na Kongamano hilo kwani washiriki watapata fursa ya kutembelea vivutio vya utalii vilivyoko nchini na hivyo kuvitangaza warudipo makwao. Pia watanzania watapata fursa ya kuuza huduma mbalimbali kwa wageni watakaohudhuria Kongamano hilo, kama vile malazi, chakula, burudani na usafiri.
Faida nyingine ni kuwa, washiriki kutoka Tanzania watapata fursa ya kubadilishana ujuzi na ueledi na wenzao watakaotoka nchi mbalimbali duniani.
Wizara inatoa wito kwa wanachi, wafanyabiashara na wadau wote kujiandaa ipasavyo ili kunufaika na ujio huo wa Kongamano hilo la kimataifa nchini.
Taarifa mbalimbali zitaendelea kutolewa kuhusu maendeleo ya maandalizi ya Kongamano hilo.
George Matiko
MSEMAJI
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

Uzinduzi wa kumbu kumbu ya mwanzilishi wa skauti Ulimwenguni bw Robert Baden PowelL na mkewe Bi. Oliva Powell(lady baden powell)kimkoa umefanyika leo na kilele ni siku ya tar.25 ya mwenzi huu kwenye viwanja vya sheikh Amri Abeid jijini hapa kwa maonyesho na matamasha kote nchini.
Hayo yamesemwa nakamishina mkufunzi mkuu wa taifa bi Margareth Olumbe wakati akisoma risala ya maskauti wa kike hapa Arusha na kusema kuwa girl guide hapa nchini ilanzishwa mnamo mwaka 1928 na girl guide 9 na walijiita 1st Kilimanjaro na walikuwa na uhusiano na mke wa gavana wa wakati huo ukaingia ukimya wa muda mrefu na guiding haikusikika hadi 1934 mke wa gavana Lady Mack alianzisha kampuni nyingine Dar es-salaam na ikaitwa 1st Dar –es-salaam kampuni na ilikuwa na wazungu tu baadae alianzisha first dar-es-salaam Brownes na ilkuwa mchanganyiko.
Kuna changamoto nyIngi kubwa zinazowakabili girl guide hapa mkoani na taifa kwa ujumla zikiwemo kuwatoa watoto katika tabia hatarishi kuwa raia wema,wazazi ambao wangesaidiana nasi wamekuwa na shughuli nyingi na wengine hawafikiki hata na watoto wao,mwitiko wa wananchi
Akatoa ombi kwa mgeni rasmi ambaye alimwakilisha mlezi wa skauti wa kike hapa nchini mama Salma Kikwete bi Pendo Laizer kutoka(CASEC) kuwa awe mlezi wa girl guide wa arusha na mgeni huyo kukubali kuwa mlezi na kuwatafutia wafadhli wakukisaidia girl guide mgeni huyo aliambatana na mgeni kutoka nchini uingereza bi jill Nicholson na Yona .M.Mziba kutoka kitengo cha polisi jamii mkoani hapa

Na Gladness Mushi - Arusha
Tanzania inajipanga vizuri kutekeleza sera ya makuzi na malezi ya awali ya mtoto wa kitanzania katika kutoa elimu ya awali hapa nchini na kuwa kila shule itatakiwa kuwa na shule ya awali kwani maandalizi tayari yalikwishaanza kwa walimu wa cheti kuwa ndio wafundishaji wa elimu hiyo.
Kauli hiyo imetolewa na waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi Dr.Shukuru Kawambwa wakati akiongea na vyombo vya habari katika jukwaa la kwanza la kitaifa linalo jadili utungwaji sera ya makuzi na malezi ya awali ya mtoto jukwaa hilo lililo andaliwa na banki ya dunia kupitia shirika la bennian la marekani inayofanyika jijini hapa.
Dr.kawambwa alisema kuwa kuangalia sera za maendeleo ya awali ya mtoto ni jambo ambalo serekali inajipanga nalo na kuwa inalipa umuhimu mkubwa ndiyo maana umeona mawaziri mbali mbali kutoka wizara za Elimu,Fedha,ofisi yawazirimkuu(Tamisemi),Afya na Maendeleo ya jamii jinsia na watoto na kuwa sera ya makuzi na malezi ni tofauti na sera nanipana zaidi kuliko sera ya elimu ilyopo hapa nchini kwa sasa.
'Unapoanza kuwekeza katika kuandaa sera na mafunzo ya awali kwa mtoto inamaana kuwa unamjali na kumthamini na kugundua vipaji vya watoto na huko ndiyo kujenga msingi wa awali wa mtoto ili anapoanza elimu ya msngi teyari anakuwa na msingi imara'.alisema Kawambwa
Alisema kuwa serekali njia iliyosawa hawajapotea kwani elimu ya kiwango cha chini inatolewa japo haikuwa inapewa kipaumbele lakini sasa tunaangalia uwezekano wakuanza kutoa chakula kwa shule zetu zote japo si kwa mwaka huu na hii inatokana na ukosefu wa fedha na akalishukuru shirika la chakula ulimwenguni (WFP)kwa kutoa chukula kwa baadhi ya shule za jamii za kifugaji hapa nchini na mafaniko meyaona kwani shule hizo viwango vimepanda.

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AZINDUA MAGHARALA MAWILI YA KUHIFADHIA BIDHAA KTK BANDARI YA KASANGA NA KUTEMBELEA WAFANYA BIASHARA WA SAMAKI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka Jiwe la Msingi katika moja ya jengo kati ya mawili ya Maghala ya kuhifadhia Bidhaa yaliyopo katika Bandari ya Kasanga, kijiji cha Lusambo Wilaya ya Sumbawanga, wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Katavi na Rukwa jana februari 23, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozwa na Luteni Godfrey Semiono (Mkuu wa Kambi) kukagua kikosi cha Ulinzi wa Mipaka cha Kasanga kilichopo katika kijiji cha Lusambo, pembezoni mwa Wilaya ya Sumbawanga, wakati alipofika eneo hilo kwa ajili ya kuzindua maghala ya kuhifadhia bidhaa katika Bandari ya Kasanga jana Februari 23, 2012, wakati akiwa katika ziara yake ya mkoa wa Katavi na Rukwa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea kukagua maeneo ya kufanyia biashara ya baadhi ya wafanyabiashara wa samaki katika Soko la Samaki la Kasanga, baada ya kuweka jiwe la msingi katika soko hilo akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Katavi na Rukwa, jana Februari 23, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea kukagua maeneo ya kufanyia biashara ya baadhi ya wafanyabiashara wa samaki
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na kuwaaga wananchi wa Kijiji cha Lusambo waliojitokeza katika mapokezi yake alipofika kuweka jiwe la msingi katika Soko la Kasanga, akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Katavi na Rukwa jana februari 23, 2012. 

VODACOM FOUNDATION YAKARABATI KITUO CHA POLISI MTO WA MBU KWA MARA YA KWANZA TANGIA KIJENGWE MWAKA 1967

Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba,akikata utepe wakati wa uzinduzi rasmi wa kituo cha Polisi Mto wa Mbu kilichopo Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha kilichokarabatiwa na Vodacom Foundation kwa mara ya kwanza tangia kijengwe mwaka 1967,kwa gharama ya shilingi milioni 17.Kushoto ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Thobias Andengenye na kulia ni Mkuu wa Vodacom Kanda ya kaskazin Nguvu Kamando.
Mkuu wa Kituo cha Mto wa Mbu kilichopo Wilaya ya Monduli Arusha.(INSP)Amilton Matangi akiwaonyesha moja ya chumba cha mahabusu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Thobias Andengenye kulia na Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba mara baada ya uzinduzi wa kituo hicho,Jumla ya shilingi Milioni 17 zilitumika kukikarabati kituo hicho tangia kijengwe mwaka 1967.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha (RPC).Thobias Andengenye akipanda mti wa ukumbusho wa uzinduzi wa kituo cha polisi cha Mto wa Mbu kilichopo Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha baada ya kukarabatiwa na Vodacom Foundation kwa mara ya kwanza tangu kijengwe mwaka 1967 na kugharimu kiasi cha shilingi milioni 17, wakishuhudia ni Mkuu wa Kituo hicho INSP Amilton Matagi ,Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba ,Mkuu wa Vodacom Kanda ya Kaskazini,Nguvu Kamando.
Mkuu wa Polisi Jamii wa Kituo cha Mto wa Mbu kilichopo Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha,Issaya Doya akimkaribisha Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa VodacomTanzania Mwamvita Makamba, wakati wa sherehe ya kakabidhi rasmi kituo hicho kilichakarabatiwa kwa mara ya kwanza na Vodacom Foundation kwa thamani ya shilingi Milioni 17,tangu kijengwe mwaka 1967.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha (RPC) Thobiasi Andengenye akimkaribisha Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba,wakati wa hafla ya kukabidhiwa kituo cha Mto wa Mbu kilichopo Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha , kilichokarabatiwa kwa mara ya kwanza na Vodacom Tanzania kwa thamani ya Shilingi Milioni 17 tangia kijengwe mwaka 1967.katikati ni Mkuu wa Polisi Wilaya ya Karatu ( OCD ) Mathias Nyange.
Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba,akipongezwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Thobias Andengenye katika hafla ya uzinduzi na makabidhiano ya kituo cha Polisi cha Mto wa Mbu kilichopo Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha,Jumla ya shilingi Milioni 17 zilitumika katika kukarabati kituo hiuchi. Kulia ni Mkuu wa Vodacom Kanda ya Kaskazini.Nguvu Kamando.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Thobias Andengenye kushoto akisalimiana na Mkuu wa Vodacom Tanzania Kanda ya Kaskazini Nguvu Kamando kulia wakati wa hafla ya uzinduzi wa kituo cha Polisi cha Mto wa Mbu kilichokarabatiwa na Vodacom Foundation katikati ni Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa kampuni hiyo Mwamvita Makamba akishuhudia, Jumla ya shilingi Milioni17.zimetumika katika ukarabati wa kituo hicho kwa mara ya kwanza tangu kijengwe mwaka 1967.
Baadhi ya wananchi wa Mto wa Mbu wa Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha wakishuhudia Makabidhiano rasmi ya Kituo cha Polisi cha Wilaya hiyo mara baada ya kukarabatiwa na Vodacom Foundation kwa mara ya kwanza tangu kijengwe mwaka 1967 na kugharimu kiasi cha shilingi milioni 17.
Waandishi wa habari wakiwa kazini kama kawa wakati wa Makabidhiano rasmi ya Kituo cha Polisi cha Mto wa Mbu kilichopo Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha kilichokarabatiwa kwa mara ya kwanza na Vodacom Foundation, tangu kujengwa kwake mwaka 1967,Maboresho hayo yamegharimu kiasi cha shilingi milioni 17.
Kituo cha Polisi Cha Mto wa Mbu kilichopo Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha kikionekana katika muonekano mpya baada ya kukarabatiwa na kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania kwa kiasi cha shilingi Milioni 17 kwa mara ya kwanza tangu kijengwe mwaka 1967.

TAARIFA KUHUSU UWEPO WA DAWA BANDIA YA KUTIBU UGONJWA WA MALARIA IITWAYO ELOQUINE (Quinine Sulphate 300mg USP)

Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) ni wakala wa Serikali iliyo chini ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii yenye jukumu la kudhibiti ubora, ufanisi na usalama wa vyakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba ili kulinda afya ya jamii.
TFDA inapenda kuutaarifu umma kuwa imebaini kuwepo kwa dawa bandia ya kutibu ugonjwa wa Malaria katika soko. Dawa hiyo inaitwa Eloquine (Quinine Sulphate 300mg U.S.P) na ipo katika makopo ya vidonge 1000 (elfu moja) kila moja. Maelezo yaliyopo katika lebo yanaonesha kuwa dawa hiyo imetengenezwa na kiwanda cha Elys Chemical Industries Ltd cha nchini Kenya.
Hata hivyo, TFDA imebaini kuwa kiwanda cha Elys Chemical Industries Ltd hakitengenezi dawa yenye jina la biashara la ‘ELOQUINE’. Kiwanda hicho kimesajili Tanzania Quinine Sulphate 300mg B.P isiyo na jina la kibiashara. Aidha, kiwanda cha Elys Chemical Industries Ltd kimebainisha tofauti mbalimbali zilizopo katika lebo ya dawa bandia ikilinganishwa na dawa halisi inayotengenezwa na kiwanda hicho iliyosajiliwa na TFDA na hivyo kuthibitisha kuwa kiwanda hicho hakitengenezi dawa hiyo.
Katika kudhibiti usambazaji wa dawa hiyo hapa nchini, hadi sasa TFDA imekamata jumla ya makopo 155 ya dawa hiyo bandia ya Eloquine jijini Dar Es Salaam yaliyokuwa yakisubiri kusambazwa. Aidha, kopo moja lenye vidonge 115 limekamatwa Moshi, Kilimanjaro. Tayari mtuhumiwa mmoja amekwishafikishwa mahakamani na upelelezi wa chanzo na wasambazaji wa dawa hii unaendelea kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi.
Uchunguzi wa dawa bandia katika maabara umebaini kuwa vidonge hivyo havina kiambato hai (active ingredient) cha Quinine Sulphate kwa ajili ya kutibu ugonjwa wa Malaria na hivyo matumizi yake ni hatari kwa afya ya binadamu.
Maelezo ya kina yanayotofautisha dawa halisi iliyosajiliwa na dawa bandia ni kama yalivyoainishwa katika jedwali hapa chini.
Dawa halisi iliyosajiliwa Maelezo ya dawa bandia
  • Jina la dawa: Quinine Sulphate 300mg B.P
  • Jina la biashara: Haina jina la biashara
  • Mtengenezaji: Elys Chemical Industries Ltd, Road B, Off Enterprise Road, P.O Box 40411, 00100 Nairobi, Kenya
  • Rangi ya Lebo: Nyeupe na kahawia (Brown)
  • Namba ya toleo: Huanzia na namba na siyo herufi. Kwa mfano: 2167E
  • Muda wa matumizi (Shelf life): Miaka 4
  • Jina la dawa: Quinine Sulphate 300mg U.S.P
  • Jina la biashara: ELOQUINE
  • Mtengenezaji: Elys Chemical Industries Ltd, Road B, Off Enterpises Road, P.O Box 4011 00100 Nairobi, Kenya
  • Rangi la Lebo: Njano na Nyekundu
  • Namba ya toleo: GE410
  • Tarehe ya kutengenezwa: 04/2009
  • Tarehe ya mwisho wa matumizi: 4/2014 (Miaka 5)
Wafanyabiashara wote wa dawa na wananchi wanatahadharishwa kutozitumia dawa hizi na wale wote waliouziwa dawa hizi wanaelekezwa kuzirudisha dawa hizo katika ofisi za TFDA, vituo vya afya vya Serikali au vituo vya polisi vilivyo jirani nao.
TFDA inapenda pia kuwakumbusha wafanyabiashara wa dawa, wasafirishaji wa vifurushi na wananchi kutoa taarifa haraka iwezekanavyo pale wanapohisi kuuziwa dawa duni, bandia au zilizoisha muda wa matumizi. Taarifa zitolewe ofisi za TFDA makao makuu zilizopo Barabara ya Mandela, EPI Mabibo External, Dar es Salaam na Ofisi za Kanda zilizopo mtaa wa Nkurumah, Mwanza, Mtaa wa Sakina – Arusha, Hosptali ya mkoa ya Dodoma na Jengo la Ofisi ya Mifugo Mkoa wa Mbeya.
Kwa maelezo zaidi tafadhali wasiliana na:-
MKURUGENZI MKUU
MAMLAKA YA CHAKULA NA DAWA
EPI MABIBO EXTERNAL,
DAR ES SALAAM

Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiwa Kishapu Mkoa wa Shinyanga

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitazama jiko banifu kwenye jiko la shule ya sekondari ya Kishapu akiwa katika ziara ya mkoa wa Februari 23, 2012. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kishapu wakicheza ngoma wakati Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alipofungua jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu akiwa katika ziara ya mkoa wa Shinyanga Februari 23, 2012. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Askari wa Jeshi la Jadi yaani Sungusungu wa mji mdogo wa Maganzo wakicheza ngoma yao wakati Waziri Mkuu Mizengo Pinda alipohutubia mkutano wa hadhara katika mji huo mdogo akiwa katika ziara ya mkoa wa Shinyanga Februari 23,2012. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwaaga kwa kuwapungia wananchi wa Mji Mdogo wa Maganzo baada ya kuwahutubia akiwa katika ziara ya mkoa wa Shinyanga Februari 23, 2012. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

VIINGILIO VYATANGAZWA TAIFA STARS VS MSUMBIJI

Kiingilio cha chini katika mechi ya mchujo ya Kombe la Mataifa ya Afrika kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Msumbiji (Mambas) itakayochezwa Februari 29 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni sh. 3,000.
Jumla viti 36,693 (rangi ya bluu na kijani) ndivyo vitakavyotumika kwa kiingilio hicho katika uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 60,000 wakiwa wameketi.
Viingilio vingine ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 10,000 kwa VIP C, sh. 15,000 kwa VIP B wakati kwa watakaokuwa miongoni mwa watakaokaa katika viti VIP A ambavyo viko 748 tu watalazimika kulipa sh. 20,000 kwa kila mmoja.
Tiketi zitaanza kuuzwa siku moja kabla ya mchezo katika vituo vya Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Kituo cha mafuta cha Bigbon kilichopo Msimbazi (Kariakoo), mgahawa wa Steers ulioko Barabara ya Samora/Ohio, Kituo cha mafuta cha Oilcom Ubungo na Uwanja wa Taifa.