TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, March 22, 2014

USAID yatoa elimu ya lishe Zanzibar

pic 1 Mkuu wa Wilaya mjini Unguja ,Bw Abdul Mahmood Mzee (katikati) akisalimiana na Bw Charles David wa USAID na Bi Rebecca Savoure Mkurugenzi mkazi wa USAID Tuboreshe Chakula katika viwanja vya Karakana Unguja,wakati wa uhamasishaji juu ya umuhimu na faida za Virutubishi kwa watoto umri wa miezi 6 – miaka 5.Kampeni hizi zimefanyika katika wilaya 8 za Tanzania bara na 2 za visiwanipic 2 Mkuu wa mkoa Mjini Magharibi Unguja,Bw Abdallah Mwinyi Khamis (Kushoto) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi mkazi wa USAID Tuboreshe chakula(kulia) Bi Rebecca Savoure wakati wa uzinduzi wa kampeni za uhamasishaji  virutubishi kwa watoto umri wa miezi 6-miaka5,kiwa ni mkakati wa Serikali ya Tanzania,ikishirikiana na USAID Tuboreshe Chakula kupunguza utapiamlo nchinipicWanafunzi wa shule za awali waUnguja walishiriki katika sherehe sherehe za uzinduzi na uhamasishaji wa virutubishi kwa watoto umri wa miezi 6-miaka5.Watoto hawa ni walengwa wakuu wa matumizi ya virutubishi.
pic3Akina mama wenye watoto waliohudhuria kampeni za uhamasishaji wa virutubishi kwa watoto umri wa miezi 6-miaka5.Watoto wadogi ni walengwa wakuu wa matumizi ya virutubishi.Kampeni hizi zimefanyika katika wilaya kumi za Tanzania Bara na Visiwani chini ya udhamini  wa USAID
pict 4Mkurugenzi mkazi wa shirika la USAID Tuboreshe Chakula, Bi Rebeca Savoure ,akitoa zawadi ya unga lishe kwa mmoja wa  kina mama,mkazi wa Unguja mjini,katika kampeni za uhamasishaji wa virutubishi kwa watoto miezi 6-miaka 5,lengo likiwa ni kupunguza utapiamlo nchini

TASWIRA ZA RAIS KIKWETE BAADA YA KUHUTUBIA BUNGE MAALUM LA KATIBA MJINI DODOM MACHI 21, 2014

jk1 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongozwa na Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mhe Samuel Sitta mara baada ya kulihutibia Bunge hilo Ijumaa  mjini Dodoma Machi 21, 2104jk2 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipongezwa na Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mhe Samuel Sitta mara baada ya kulihutibia Bunge hilo Ijumaa  mjini Dodoma Machi 21, 2104jk3Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipewa pongezi kwa hotuba nzuti na Makamu  Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mhe. Samia  Suluhu Hassan mara baada ya kulihutibia Bunge hilo Ijumaa  mjini Dodoma Machi 21, 2104jkk Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Zanzibar Dkt Mohamed Ali Shein,  Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mhe Samuel Sitta na Makamu  Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mhe. Suluhu Samia Hassan wakifurahia jambo mara baada ya Rais  kulihutibia Bunge hilo Ijumaa  mjini Dodoma Machi 21, 2104
jk5Rais Kikwete katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba
PICHA NA IKULU

MATEMBEZI YA UVCCM KUADHIMISHA MIAKA 50 YA MUUNGANO YAZINDULIWA

IMG_7611 (1) Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein, akibonyeza kitufe  kuashiria uzinduzi wa matembezi ya vijana katika kuadhimisha miaka 50 ya Muungano wa Tanzania,uzinduzi huo uliofanyika leo katika viwanja vya Makao Makuu ya CCM Dodoma, [Picha na Ramadhan Othman,Dodoma,] 
IMG_7636 (1)Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Sadifa Juma Khamis (kushoto) na Katibu Mkuu wa jumuiya hiyo Sixtos Mapunda wakipeperusha bendera za Muungano na CCM wakati wa uzinduzi wa matembezi ya kuadhimisha miaka 50 ya Muungano wa Tanzania yaliyozinduliwa leo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein,Mjini Dodoma ,[Picha na Ramadhan Othman,Dodoma,]
TA1A7421 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein,akiwapungia mkono Wanachama wa CCM na Vijana alipowasili katika viwanja vya Makamo Makuu ya CCM Mjini Dodoma leo,kuzindua matembezi ya UVCCM katika kuadhimisha miaka 50 ya Muungano wa Tanzania, [Picha na Ramadhan Othman,Dodoma,]TA1A7434 Vijana wa UVCCM Mkoa wa Dodoma wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein, alipozungumza nao wakati wa uzinduzi wa matembezi ya kuadhimisha miaka 50 ya Muungao wa Tanzania katika viwanja vya Makao Mkuu Mjini Dodoma leo, [Picha na Ramadhan Othman,Dodoma,]TA1A7513Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na Vijana wa UVCCM Mkoa Dodoma  katika viwanja vya Makamo Makuu ya CCM Mjini Dodoma leo,akizindua matembezi ya UVCCM katika kuadhimisha miaka 50 ya Muungano wa Tanzania, [Picha na Ramadhan Othman,Dodoma,]TA1A7460 Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Sadifa Juma Khamis akisisitiza jambo alipokuwa akimakaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein, alipozungumza na Vijana wa UVCCM wakati wa uzinduzi wa matembezi ya kuadhimisha miaka 50 ya Muungao wa Tanzania katika viwanja vya Makao Mkuu Mjini Dodoma leo, [Picha na Ramadhan Othman,Dodoma,]IMG_7539Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein,alipokuwa akikabidhi vifaa kwa waendesha mapikipiki wa CCM watakaoshiriki mbio za kudhimisha miaka 50 ya Muungano wa Tanzania,zitakazotembea Mikoa ya Tanzia katika wakati wa Uzinduzi wa Matembezi Mjini Dodoma leo , [Picha na Ramadhan Othman,Dodoma,]

WANAFUNZI WANAWAKE CHUO CHA ELIMU YA BIASHARA DAR WAWEKA HISTORIA, WAANZISHA MFUKO WA KUWAKOMBOA KIELIMU

Picha na 2 (1)Waziri wa Wanawake wa Chuo cha Elimu ya Biashara Dar es salaam (CBE) Bi. Mwajuma Sangali akiwaongoza wananfunzi wa Kike wa chuo hicho wakati wa uzinduzi  wa mchakato wa kuanzisha mfuko wa Jumuiya ya Wanafunzi wa kike wenye lengo la kuwakomboa kielimu.
Picha na 6 Kikundi cha maagizo cha chuo hicho kikionyesha namna vitendo vya ukiukwaji wa maadili unavyodhibitiwa chuoni hapo na namna uongozi wa chuo hicho unavyowachukulia hatua za kinidhamu wanaokiuka maadili ya chuo hicho.Picha na 7 Igizo la wanafunzi wakiwa kwenye majadiliano chuoni hapo bila kujali tofauti za jinsia .Picha na 8 Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Mary Mwangisa (kulia) akizungumza  na wanafunzi wa Kike wa chuo cha CBE kampasi ya Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa  mchakato wa kuanzisha mfuko wa Jumuiya ya Wanafunzi wa kike chuoni hapo wenye lengo la kuwakomboa kielimu.Picha na 9 Baadhi ya wanafunzi wa kike wa chuo hicho wakifurahia  matukio mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea wakati wa hafla ya uzinduzi wa  mchakato wa kuanzisha mfuko wa Jumuiya ya Wanafunzi wa kike chuoni hapo wenye lengo la kuwakomboa kielimu, kisiasa na kiutamaduni leo jijini Dar es salaam.Picha na 10Wanafunzi wa Kike wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Mary Mwangisa (katikati). 
Picha na Aron Msigwa – MAELEZO
…………………………………………………………………………………………….
Na Aron Msigwa – MAELEZO, Dar es salaam.
 
Wanafunzi wanawake wa Chuo cha Elimu ya Biashara Dar es salaam (CBE) wamezindua mchakato wa kuanzisha mfuko wa Jumuiya ya wanafunzi wa kike wenye lengo la  kumkomboa na kumwezesha mwanafunzi wa kike kujitambua, kielimu, kisiasa na kiutamaduni.
 
Akizungumza na jumuiya ya wanafunzi wa kike wa chuo hicho wakati wa uzinduzi  wa mfuko huo  leo jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Mery Mwangisa ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo amesema kuwa kuanzishwa kwa jumuiya hiyo  ni ishara ya umoja na mshikamano wa wanafunzi wa kike chuoni hapo.
 
Amesema kuanzishwa kwa mfuko huo kunatokana na kuongezeka kwa changamoto mbalimbali zinazowakabili wanawake pia  kukosekana kwa mifuko ya aina hiyo katika taasisi nyingi za elimu ya juu hapa nchini.
 
Ameeleza kuwa  malengo ya mfuko huo ni kumwezesha mwanafunzi wa kike wa CBE kujitambua kielimu, kisiasa na kiutamaduni na kuongeza kuwa yamekuja  wakati muafaka kufuatia  mabadiliko yaliyopo sasa ya kiuchumi, kisiasa, kijamii na kiutamaduni.
 
 Amefafanua kuwa mfuko huo ulioanzishwa katika chuo hicho ni fursa pekee ya kuwawezesha wanafunzi wa kike kunufaika kwa kupata elimu bora bila vikwazo.
 
“Napenda kutumia fursa hii kuushukuru uongozi wa chuo hiki kwa kuonyesha njia ya kuwajali wanawake na pia katika kuweka taratibu nzuri za kulinda maadili, katika maisha yangu sijawahi kusikia chuo kikuu chochote kimezindua jukwaa la wanawake lenye malengo mazuri kama yenu” Amesema Dkt. Mwangisa.
 
Ameeleza kuwa kwa muda mrefu wanawake kote nchini wamekuwa na juhudi  mbalimbali za kujikomboa kiuchumi pamoja na kulitumikia taifa kwa kushika nyadhifa mbalimbali serikalini kwa ufanisi mkubwa na kuwataka kuendelea kufanya kazi kwa bidii pindi wanapokabidhiwa madaraka.
 
“Ninapowaangalia ninyi nafarijika maana naona viongozi wakuu wa serikali, naona marais na pia wakurugenzi wa biashara”
 
Akizungumza kuhusu kuanzishwa kwa mfuko huo na mafanikio yake  Dkt. Mwangisa amesema kuwa atatoa ushirikiano kwa wanafunzi hao ili kuhakikisha kuwa mfuko huo unajengewa uwezo wa  kusimama na kuwanufaisha wanawake wanaokumbwa na changamoto zinazokwamisha maendeleo yao ikiwemo ukosefu wa fedha.
 
Amesema kuwa kukamilika kwa taratibu za jumuiya hiyo ikiwemo maandalizi ya katiba ya jukwaa hilo kutaliwezesha jukwaa hilo kupanga, kuandaa na kutekeleza mikakati mbalimbali ya kujiendesha ili kuwawezesha wanafunzi hao kutatua changamoto zinazowakabili kwa kulinda heshima yao katika jamii.
 
Kwa upande wake mjumbe wa Bodi ya Taaluma ya Chuo hicho Dkt. Ellen Oturu Okoedion amesema kuwa wanafunzi wa kike wa chuo hicho wanahitaji msaada kupitia mfuko huo utakaowawezesha kupambana na wimbi la wanafunzi wa kike kushindwa kumaliza masomo yao kwa kushindwa kumudu gharama za masomo.
 
Amewataka wanafunzi wa kike wa chuo hicho kutumia ipasavyo taaluma wanayoipata  kusaidia mfuko huo kupata fedha  ili uwe endelevu kwa maendeleo ya wanawake na chuo hicho.
 
“Ninyi mnasoma elimu ya biashara na ndio watalaam wenyewe sitarajii mfuko wenu ukose uwezo, naamini mtatumia taaluma yenu mnayoipata hapa chuoni kutafuta fedha kwa kuwa mnao uwezo huo” Amesisitiza Dkt. Ellen.
 
Naye Waziri wa Wanawake wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Bi. Mwajuma Sangali ameeleza kuwa wanawake kote nchini wana jukumu la kuandaa kizazi cha watu wenye upendo, uzalendo, kupenda kazi na maendeleo.
 
Amesema kuanzishwa kwa chombo hicho kunalenga kuboresha maisha ya wanawake hasa katika masuala ya elimu,jamii,uchumi na siasa.

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, WAKATI WA KULIHUTUBIA BUNGE MAALUM LA KATIBA, TAREHE 21 MACHI, 2014, DODOMA

220px-Coat_of_arms_of_Tanzania.svg
Mheshimiwa Samuel Sitta, Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba;
Mheshimiwa Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi;
Mheshimiwa Mizengo Peter Pinda, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Maalim Seif Sharif Hamad, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar;
Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
Mheshimiwa Anne Semamba Makinda; Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano;
Mheshimiwa Pandu Ameir Kificho, Spika wa Baraza la Wawakilishi na Mwenyekiti wa Muda wa Bunge Maalum la Katiba ;
Mheshimiwa Rashid Othman Chande, Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Othman Makungu,  Jaji Mkuu wa Zanzibar;
Viongozi Wakuu Wastaafu;
Waheshimiwa Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba;
Waheshimiwa Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba;
Wageni waalikwa;
Mabibi na Mabwana;
Pongezi
            Nakushukuru sana Mheshimiwa Mwenyekiti kwa kunipa fursa ya kuja kuzungumza na Waheshimiwa Wajumbe wa Bunge letu Maalum la Katiba katika siku hii muhimu na ya kihistoria kwa nchi yetu.  Nimekuja kuwatakia heri na naungana na Watanzania wenzetu wote kuwaombea baraka za Mwenyezi Mungu, ili muweze kuifanya kazi yenu kwa utulivu, hekima, umakini mkubwa na kuimaliza kwa salama na kwa mafanikio yanayoyatarajiwa  na Watanzania.
Natoa pongezi nyingi kwako na kwa Makamu wako kwa kuchaguliwa kwenu kuongoza Bunge hili maalumu na la kihistoria.  Ushindi mkubwa mliopata ni kielelezo tosha cha imani kubwa na matumaini waliyonayo Wajumbe wenzenu kwenu. Matumaini yao ndiyo matumaini ya Watanzania wote, kwamba mtaliongoza vizuri Bunge hili, ili liweze kutimiza kwa ufanisi mkubwa jukumu lake muhimu sana katika historia ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Niruhusu pia niwapongeze kwa dhati Wajumbe wote wa Bunge Maalum la Katiba kwa bahati ya aina yake waliyopata ya kutunga Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.  Fursa hii hutokea mara chache sana katika historia ya nchi yo yote na watu wake.  Mkifanikiwa kuipatia nchi yetu Katiba nzuri majina yenu yataandikwa kwa wino wa dhahabu, katika kumbukumbu za historia ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ni matarajio ya Watanzania kuwa mtatunga Katiba itakayokubalika na wengi.  Katiba inayotekelezeka.  Katiba itakayoimarisha Muungano wetu kwa kuondoa changamoto zilizopo sasa.  Katiba itakayoipa nchi yetu mfumo bora wa kuongoza na kuendesha mambo yetu.  Katiba itakayoimarisha umoja, upendo, ushirikiano na mshikamano miongoni mwa wananchi wa Tanzania, licha ya tofauti zao za asili za upande wa Muungano na maeneo watokako, au tofauti za jinsia, rangi, kabila, dini na ufuasi wa vyama vya siasa.  Katiba itakayodumisha amani, usalama na utulivu nchini.  Katiba itakayostawisha zaidi demokrasia, haki za binadamu, utawala wa sheria, utawala bora na kudhibiti maovu.  Na, mwisho ingawaje siyo mwisho kwa umuhimu, Katiba itakayoweka mazingira mazuri kwa uchumi wa nchi kukua, na wananchi wengi kunufaika sawia na maendeleo yatayopatikana
www.baloziwademokrasiatanzania.blogspot.com

Rais Dkt. Jakaya Kikwete azindua rasmi Bunge Maalum la Katiba.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea salama ya heshima kutoka Jeshi la Polisi kabla ya hotuba ya uzinduzi wa Bunge maalum la Katiba leo mjini Dodoma.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride liliandaliwa na Jeshi la Polisi kabla ya hotuba ya uzinduzi wa Bunge maalum la Katiba leo mjini Dodoma.

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samwel Sitta (kulia) na Makamu Mwenyekiti Samia Suluhu wakijadiliana jamba nje ya ukumbi wa Bunge kabla hotuba ya uzinduzi wa Bunge Maalum la Katiba leo mjini Dodoma.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutuba Bunge Maalum la Katiba wakati wa sherehe za uzinduzi wa Bunge hilo leo mjini Dodoma.

Makamu wa kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Maalim Mh. Seif Sharif Hamad (kushoto) Jaji Mkuu wa Zanzibar Mh. Omar Othman Makungu(Katikati) na Rais Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt. Amaan Abeid Karume Wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa Hotuba ya Uzinduzi wa Bunge Maalum la Katiba Mjini Dodoma Leo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya Pamoja na Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba Leo Mjini Dodoma.

(Picha na Idara ya Habari-MAELEZO)
Posted By Blogger to THE GOVERNMENT OFFICIAL BLOG

MKUU WA WILAYA YA NKASI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA WA RUKWA INJINIA STELLA MANYANYA AFUNGUA RASMI KAMPENI YA TOHARA KWA WANAUME MKOANI RUKWA

Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Iddi Hassan Kimanta akihutubia katika hafla fupi ya uzinduzi rasmi wa kampeni ya Tohara kwa wanaume Mkoani Rukwa iliyofanyika kimkoa katika Tarafa ya Challa Wilayani Nkasi. Akihutubia katika hafla hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo Injinia Stella Manyanya Mkuu huyo wa Wilaya amesema hadi kufikia mwezi wa tisa mwaka huu 2014 Mkoa wa Rukwa unatakiwa uwe umeshafanya tohara za wanaume 22, 000 ikiwa ni agizo la kitaifa ambapo hadi sasa jumla ya wanaume 7,000 wameshafanyiwa tohara.  
 
Kwa mujibu wa mratibu wa zoezi hilo Mkoani Rukwa tangu kampeni hiyo ianze tarehe 17 Machi 2014 hadi jana tarehe 20 Machi 2014 jumla ya wanaume 583 wameshafanyiwa tohara ndani ya siku 4 katika kituo kilichopo tarafa ya Challa. Kampeni hiyo inaenda sambamba na zoezi la upimaji wa VVU ambapo kati ya wananchi 699 waliopimwa ni mmoja tu amekutwa na maambukizo ya virusi hivyo katika tarafa hiyo ya Challa.
 
Akizungumzia faida za tohara kwa wanaume amesema husaidia kupunguza uwezekano wa akinamama kupata kansa ya kizazi  pamoja na kusaidia  kuepusha uwezekano wa maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa wanaume kwa zaidi ya asilimia 50%.
Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Ndugu Smythies Pangisa akiwasalimia wananchi wa tarafa ya Challa waliojitokeza kwa wingi katika uzinduzi wa Kampeni hiyo.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Daktari John Gurisha akizungumza katika hafla hiyo. Akizungumzia juu ya zoezi hilo la tohara amesema tohara kwa wanaume husaidia  kuepusha uwezekano wa maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa wanaume kwa zaidi ya asilimia 50%. 
Zoezi la Tohara likiwa linaendelea katika zahanati ya Challa.
Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Iddi Kimanta akimkaribisha Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Ndugu Smythies Pangisa awasalimu wananchi wa Challa.
Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Ndugu Smythies Pangisa (wa nne kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. John Gurisha (watatu kulia), Katibu Tawala Msaidizi Serikali za Mitaa Albinus Mugonya (wa tano kulia) na watumishi wa Idara ya Afya katika Hospitali Kuu ya Mkoa wa Rukwa (kulia) mara baada ya uzinduzi wa kampeni hiyo.
(Na Hamza Temba – Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa @rukwareview.blogspot.com)

SERIKALI KUTOA RUZUKU KWA WAVUVI ILI KUIMARISHA SEKTA YA UVUVI NCHINI

1Watendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi na baadhi ya waandishi wa habari wakipanda kwenye boti ndogo kwa ajili ya kuelekea kwenye kisiwa cha Bongoye kufanya mkutano. 2
Watendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi na baadhi ya waandishi wa habari, wakiwa wamefika kwenye kisiwa cha Bongoye. 3Watendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi na baadhi ya waandishi wa habari, wakielekea kwenye sehemu ya kufanyia mkutano. 4Msemaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi  Dk. Mohammed Bahari akizungumza na waandishi wa habari juu ya ruzuku kwa wavuvi.Katikati ni Afisa Habari wa Idara ya Habari (MAELEZO) Frank Mvungi na mwisho ni Mkurugenzi Msaidizi wa Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi, Baraka Mngulwi. 5Meneja Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dk. Milali Machumu akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani).Katikati ni Msemaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi  Dk. Mohammed Bahari na mwisho ni Afisa Habari wa Idara ya Habari (MAELEZO) Frank Mvungi. 6Mkurugenzi Msaidizi wa Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi, Baraka Mngulwi, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu ruzuku kwa wavuvi.Katikati ni Afisa Habari wa Idara ya Habari (MAELEZO) Frank Mvungi na mwisho ni Msemaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi  Dk. Mohammed Bahari. 7Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Msemaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Mohammed Bahari akizungumza na waandishi wa habari juu ya ruzuku kwa wavuvi. 9Baadhi ya Watendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi na waandishi wa habari, wakiteremka kutoka kwenye Boti baada ya kuwasili kwenye hoteli ya Sea Cliff wakitokea kisiwa cha Bongoye ambako ndiko kulikofanyika mkutano na waandishi wa habari. Picha zote na Hussein Makame
………………………………………………………………………….
Frank Mvungi- Maelezo
SERIKALI imetenga Shilingi Bilioni 1.9 kwa ajili ya ruzuku kwa wavuvi katika kipindi cha mwaka wa Fedha 2013/14 ili kusaidia kukuza sekta ya uvuvi hapa nchini
Hayo yamesemwa na  Msemaji wa Wizara  ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Mohammed Bahari wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam.
Dkt Bahari amesema kuwa ruzuku hiyo itatolewa kwa kuzingatia vigezo ikiwemo waombaji kuwa na vyama vya ushirika na vilivyosajiliwa kisheria.
Alitaja vigezo vingine kuwa ni chama cha ushirika kiwe kinafanya kazi za uvuvi kufuatana na sheria ya uvuvi na 22 ya mwaka 2003 na kanuni za uvuvi za mwaka 2009 na miongozo mbalimbali.
Aliongeza kuwa chama hicho kiwe na akaunti benki  iliyo hai na kithibitishe kuwa na uwezo wa kuchangia asilimia 40% ya gharama ya mradi husika, ambapo Serikali itachangia asilimia 60% ya gharama ya mradi husika.
“Chama husika kitapitisha maombi yao kwa Mkurugenzi wa Halmashauri husika kwa ajili ya kupitia maombi hayo na kuona kama yanakidhi vigezo viliwekwa na baada ya hapo kuwasilishwa Wizarani” alisema Dk. Bahari.
Alisema miradi itakayofadhiliwa ni pamoja na ununuzi wa boti za uvuvi, injini  na vifaa vingine vitakavyowawezesha wavuvi kuongeza tija katika shughuli za uvuvi
Dkt Bahari alifafanua kuwa ruzuku hiyo kwa wavuvi itakuwa na manufaa makubwa kama vile kuongeza mapato ya wavuvi na wafanyabiashara wa mazao ya uvuvi.
Aliongeza kuwa ruzuku hiyo pia itaongezeka maduhuli ya Serikali, kupunguza vitendo vya uvuvi haramu,kuimarika kwa biashara ya mazao ya uvuvi na kuongeza ajira katika sekta ya uvuvi.
Naye Mkurugenzi Msaidizi Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi, Baraka Mngulwi alitoa wito kwa wale wote wanajihusisha na vitendo vya uvuvi haramu kuacha tabia hiyo mara moja kwa kuwa Serikali imeimarisha doria katika maeneo yote .
Aliongeza kuwa kwa wale wanatumia nyavu  ambazo zimepigwa marufuku nao waache mara mara moja tabia hiyo na hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa wale wote watakaokwenda kinyume cha sheria ya uvuvi na. 22 ya mwaka 2003 na kanuni zake za mwaka 2009.
Alizihimiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha kuwa sheria za uvuvi na kanuni zake zinazingatiwa kikamilifu na kuwa uvuvi haramu na biashara ya samaki wachanga vinadhibitiwa katika maeneo yao.

HOTUBA YA KIKWETE WAPINZANI WAISASAMBUA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu.   mchimati@gmail.com    au

Wenyeviti wa vyama vya upinzani nchini, kutoka kushoto ni James Mbatia (NCCR-Mageuzi), Freeman Mbowe (Chadema) na Profesa Ibrahim Lipumba (CUF).
Dodoma. 
Wenyeviti wa vyama vya Upinzani vya Chadema, Chama cha Wananchi (CUF) na Chama cha NCCR-Mageuzi, jana usiku walikutana ili kutoa kauli ya pamoja, kutokana na hotuba ya ufunguzi wa Bunge kwa maelezo kuwa tayari Rais amevuruga mchakato mzima wa kupata Katiba Mpya.

Wakati viongozi hao wakikutana, Mwenyekiti wa Chama cha DP Mchungaji, Christopher Mtikila alisema, Rais ameingilia mchakato na kutoa maelezo jinsi ya kuandika Katiba.
Wakizungumza na wanahabari wa Full Utamu mara baada ya hotuba hiyo, Freeman Mbowe, James Mbatia na Profesa Ibrahim Lipumba, walisema wameipokea kwa masikitiko makubwa hotuba hiyo.
“Tunakwenda kujadili hotuba ya Rais na tutatoa msimamo wetu,” alisema Mbowe.
Awali Katibu wa muda wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Julius Mtatiro alisema Rais Jakaya Kikwete amevuruga mchakato wa Katiba, kwani walitarajia angetumia mamlaka yake kama Rais kuwaunganisha.
“Rais tulitarajia angeongea kama mkuu wa nchi, lakini amezungumza kama Mwenyekiti wa CCM na kutoa msimamo juu ya muundo wa Muungano jambo ambalo hatukulitegemea,” alisema Mtatiro.

Alisema kwa Rais kutoa msimamo ni sawa na mwongozo jambo ambalo limevuruga mchakato mzima.
Hofu ya kuvunjika Bunge
Wakizungumza nje ya Bunge, baadhi ya wajumbe wameeleza kuwa hotuba ya Rais Kikwete kama ikitekelezwa uwezekano wa kupata Katiba Mpya utakuwa mgumu.
Mjumbe Luhaga Mpina alisema kwa jinsi rasimu ilivyoandikiwa na kama muundo wa serikali mbili ukipita basi rasimu ya Katiba itabidi iandikwe upya.
“Rasimu yote imetengenezwa kwa mfumo wa serikali tatu sasa hapa kuna hatari ya Bunge kukwama ,” alisema.
Mtatiro kwa upande wake alisema sasa kuna hofu ya kushindwa kupatikana Katiba Mpya kwani Rais amewachanganya wajumbe na kama watapitisha maoni yake itabidi rasimu kuandikwa upya.
Mjumbe Mustapha Akoonay, alisema upatikanaji wa katiba upo shakani kwani sasa upinzani utakuwa mkubwa juu ya muundo wa muungano.
“Kwa sasa nadhani itabidi turudi upya kwa wananchi kupata kura ya maoni juu ya muundo wa muungano,” alisema.
Lucy Owenya alisema Rais amegeuza mkutano wa Bunge kuwa ni mkutano wa Chama Cha Mapinduzi, kwani ameshindwa kabisa kutoa mwelekeo wa nchi na badala yake ametoa msimamo wa CCM.
“Kutokana na hili, naamini kabisa Bunge halitakuwapo na ni bora iwe hivyo kwa kuwa amejibu hotuba ya Warioba na kwa maana hiyo amepingana na mawazo ya wananchi.”
Godbles Lema alisema kuwa Rais hakuja kuhutubia taifa bali alikuja kufanya semina na kujibu hotuba ya Warioba.
Mjumbe huyo ambaye ni mbunge wa Arusha Mjini alionyesha shaka kuwa baada ya muda wa wiki tatu hakutakuwa na Bunge la Katiba kwa kuwa wako baadhi ya watu ambao hawatakubali kilichofanywa na Rais Kikwete.
“Waliochukua fedha ni vyema wakaenda kumalizia nyumba zao kwa kuwa kiongozi wetu amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwafurahisha wanaCCM lakini kwa Watanzania hatutakubali,” alisema Lema.
John Cheyo alisema, “Mimi ninachokiona ni maridhiano tu, suala la kufumua rasimu halinipi shida kwa kuwa vitu vyote vinavyoletwa bungeni huwa ni mali ya Bunge na hivyo tutafanya tunavyoona sisi inafaa.”
Mchungaji Peter Msigwa, alisema kuwa kosa kubwa ambalo lilifanywa na upinzani ni kukubali na kuruhusu Jaji Warioba atangulie kuwasilisha rasimu yake akasema hilo ndilo lililowagharimu.
Alitaka Bunge livunjwe mara moja ili warudi kwa wananchi wakaamue na kuwahukumu kutokana na kile ambacho walikifanya katika Bunge ambalo kwa maoni yake wamekula fedha za walipa kodi bure.
Naye Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa aliipongeza hutuba ya Rais Jakaya Kikwete ya uzinduzi wa Bunge la Katiba.
Lowassa ambaye pia ni Mjumbe wa Bunge la Katiba, alisema kwa kifupi hotuba ya Rais Kikwete ni nzuri. Lowassa alitoa kauli hiyo, wakati akitoka nje ya Bunge, muda mfupi baada ya Rais Jakaya Kikwete kumaliza hotuba ya uzinduzi wa Bunge hilo.
Naye Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Mchungaji Ernest Kadiva, alisema hotuba ya Rais imetoa mwanga kwa wajumbe.
“Rais ameonyesha upungufu wa hoja mbalimbali hasa katika mfumo wa serikali tatu na sasa ameacha kazi ya kuamua tuwe na mfumo wa serikali mbili au tatu ni ya wajumbe,” alisema Mchungaji Kadiva.
Hata hivyo, mjumbe mmoja ambaye hakupenda kutaja jina lake alisema Rais alizungumza kama si mkuu wa nchi bali Mwenyekiti wa CCM kwa sababu amesimamia hoja za chama chake.
Alisema hata kama mapendekezo ya Rais Kikwete yatatekelezwa, kamwe hayatakuwa mwarobaini wa muungano. Mbunge wa Mwibara, Khangi Lugora alisema hotuba hiyo waliitarajia na ndio maana kulikuwa na ubishi wa nani atangulie kati ya Jaji Joseph Warioba na yeye kwa mujibu wa kanuni.
“Hotuba ilikuwa ikijaribu kumjibu Jaji Warioba na kwangu mimi nilikuwa naona kuwa Rais naye alikuwa anachangia katika kuitunga Katiba kwa kupitia hotuba yake hiyo. Tumeyasikia na sisi tutakwenda kutafakari katika kutunga Katiba ambayo itakuwa ya Watanzania wote,” alisema.
Kwa upande wake Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema) Mkiwa Kimwanga, alisema kilichofanyika ni Rais kwenda kutoa uamuzi juu ya mchakato uliokuwa ufanywe na Bunge hilo.
Kwa upande wake, Profesa Ibrahim Lipumba, alisema hakuitendea haki Tume ya Mabadiliko ya Katiba na kwamba Bunge hilo haliwezi kutengeneza Katiba ambayo inalenga katika mfumo wa serikali la mbili.
“Itakuwa ni vigumu zaidi kupata Katiba Mpya, alikuwa anapinga mambo ya msingi yaliyoelezwa katika rasimu ya kwanza. Hayo angeyaeleza katika hatua ya awali ili rasimu hiyo ibadilishwe na si katika hatua hii ya mwisho kabla ya kwenda kupigiwa kura na wananchi,” alisema.
Alisema ndani ya siku 70 haiwezekani kubadili rasimu hiyo ambayo imejikita katika muundo wa serikali tatu kwenda katika muundo wa serikali mbili.
Ezekiah Olouch alitahadharisha wajumbe wenzake kutodharau maoni ya wananchi waliyoyatoa katika rasimu hiyo ya pili.
Alisema haiwezekani tume zote ambazo zimeundwa kuangalia aina ya muundo wa serikali zije na jibu moja kuwa namna ya kuimarisha muungano ni kuwapo kwa serikali tatu.
Jussa Ismail Ladu alisema kwa ufupi kwamba hotuba ya Rais Kikwete imekuwa yenye sura ya CCM zaidi.
Naye Mbunge wa Lulindi, Jerome Bwanausi, aliielezea hotuba ya Rais kuwa imeibua mambo mengi ambayo baadhi ya watu walikuwa wakiyaelewa tofauti, hivyo imeweka uelewa mzuri katika baadhi ya maeneo.
Profesa Costa Mahalu alisema ni hotuba ambayo imewaachia changamoto, hasa katika eneo la muungano kwa sababu wanahitajika kuunda muungano usiotetereka.
Chanzo: Mwananchi.