TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, December 14, 2013

Mpango wa Fedha kutoka TASAF wawanufaisha wakazi wa Kongwe Kiona

Diwani wa kata ya kamange, Husein Juma Hading’oka akielezea jambo kwa wanakijiji wa Kongwe Kiona pamoja na Wanahabari , tarehe 13 Decemba, 2013, wakati walipotembelea kijiji cha Kongwe Kiona, ambapo baadhi ya Kaya zimenufaika na Mpango  wa Uhawilishaji Fedha kwa Maendeleo Endelevu ya Kaya, Mpango huu unalenga kunusuru kaya maskini, kwa kutoa ruzuku kwa kaya maskini sana ili ziweze kupata huduma za elimu na afya.

Baadhi ya  waandishi wa habari na wahariri wakiwa pamoja na wanakijiji wa Kongwe Kiona wakimsikiliza Afisa Mtendaji wa kata ya Kamange, Suleiman Jumanne(hayupo pichani) akisoma taarifa fupi, kuhusu manufaa ya mpango wa Uhawilishaji Fedha kwa wakazi wa kijiji cha Kongwe Kiona.


Wanakijiji wa Kongwe Kiona wakimsikiliza Diwani wa kata ya kamange, Husein Juma Hading’oka (hayupo pichani).

Mkazi wa Kijiji cha Kongwe Kiona, Sufiani Juma Sungura akitoa ushuhuda wa jinsi alivyo nufaika na Mpango wa Uhawilishaji Fedha, kutoka  Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Kupitia Mpango huu Ndugu Sungura ameweza kuezeka nyumba yake kwa bati pamoja na kuweza kujikimu dhidi ya njaa kwa kuhifadhi mazao ya chakula.

Mkazi wa Kijiji cha Kongwe Kiona, Bi. Khadija Said Sengwira, akieleza ni kwa kiasi gani mpango wa Uhawilishaji Fedha kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF),umebadili maisha yake, nasasa ni mfugaji wa bata wa biashara.

Mkazi wa Kijiji cha Kongwe Kiona, Said Juma Kwavi akionesha Magunia ya Mahindi aliyoweza kuzalisha na kuhifadhi baada ya kunufaika na Mpango wa Uhawilishaji Fedha, kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)

Mkuu wa kitengo cha Habari na Mawasiliano kutoka  Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Zuhura Mdungi  akifafanua jambo kwa Wanahabari, tarehe 13 Decemba, 2013, wakati walipotembelea kijiji cha Kongwe Kiona, ambapo baadhi ya Kaya zimenufaika na Mpango  wa Uhawilishaji Fedha kwa Maendeleo Endelevu ya Kaya, Mpango huu unalenga kunusuru kaya maskini, kwa kutoa ruzuku kwa kaya maskini sana ili ziweze kupata huduma za elimu na afya. Kwasasa Mpango huu unatekelezwa katika Kaya za wilaya tatu za Mkoa wa Pwani ikiwemo Bagamoyo.

BARAZA LA MAWAZIRI KWA FUKUTA MOSHI

mawaziri+clip (1) 
Rais Kikwete akiendesha kikao cha baraza la Mawaziri siku za hivi karibuni. Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM chini ya Mwenyekiti wake Rais Jakaya Kikwete, imeanza kuwahoji mawaziri waliotajwa ni ‘mzigo’ kwa Serikali. Picha na Maktaba.
………………………………………………………………

Dodoma. Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM chini ya Mwenyekiti wake Rais Jakaya Kikwete, imeanza kuwahoji mawaziri waliotajwa ni ‘mzigo’ kwa Serikali.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, jana alilithibitishia gazeti dada la Mwananchi, The Citizen juu ya kuanza kwa kikao cha Kamati Kuu (CC), lakini hakuwa tayari kuingia kwa undani kuhusu ajenda.
Hata hivyo, habari za ndani zilieleza kwamba miongoni mwa ajenda kuu za CC ni kuwahoji mawaziri wanaolalamikiwa na wananchi, kwamba wameshindwa kutekeleza majukumu yao.
Wakiwa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma, Nape aliwatupia lawama mawaziri wakati akielezea changamoto zinazowakabili wakulima ambao ni asilimia 80 ya Watanzania, huku mawaziri husika wakikaa kimya.
Mawaziri waliotajwa mzigo ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa; Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher Chiza na Naibu wake, Adam Malima, kwamba wameshindwa kazi na alipendekeza wang’olewe.
Hata hivyo, gazeti hili jana lilishuhudia mawaziri kadhaa wakifika na kuingia kwenye mkutano wa CC, taarifa zingine zilisema mawaziri waliofika kwenye kikao hicho walihojiwa na wajumbe wa CC.
Kuhojiwa na CC
Mawaziri waliohojiwa na CC hadi kufikia saa 8:00 mchana jana walitajwa kuwa ni Naibu Waziri wa Fedha, Saada Mkuya na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher Chiza. Mkuya ndiye ambaye kwa sasa anaisimamia Wizara Fedha kutokana na Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa kulazwa nchini Afrika Kusini akisumbuliwa na maradhi ambayo hayajatajwa.
Waandishi wa gazeti hili jana waliwashuhudia takriban mawaziri 10 wakiingia katika ofisi za makao makuu ya CCM, Dodoma, maarufu White House, huku baadhi wakiwa si wajumbe wa CC.
Habari zilizotufikia jioni ziliwataja wengine kuwa ni Dk David Mathayo David (Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi), Hawa Ghasia (Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa-Tamisemi), Dk Kawambwa, Celina Kombani (Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma).
Dk Kawambwa wakati akitoka kwenye kikao cha CC aliulizwa na waandishi wa habari kilichotokea na yeye alijibu kwa kifupi; “Mawaziri mizigo ndiyo tunatoka.”
Mawaziri ambao si wajumbe wa CC ni Mkuya, Chiza, Dk Kawambwa, Hawa Ghasia na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais anayeshughulikia Utawala Bora, George Mkuchika ambaye naye taarifa zilidai alihojiwa.
Tayari Bunge limepitisha azimio la kumtaka Ghasia pamoja na naibu mawaziri wake wawili, Aggrey Mwanry na Majaliwa Kassim Majaliwa, kupima na kutafakari kama bado wanatosha kusimamia wizara hiyo.
Kiini cha Bunge kupitisha azimio hilo ni taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali kubainisha kuwapo wizi, ubadhirifu na mtandao wa ufisadi ndani ya Tamisemi, Halmashauri na Hazina.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye baadhi ya wabunge wamemtaja kama waziri mzigo namba moja, amesema yuko tayari kuachia ngazi kama Rais ataamua kumwondoa katika wadhifa huo.
Pinda alitoa kauli hiyo juzi bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la papo kwa hapo kutoka kwa Mbunge wa Viti Maalumu, Rukia Ahmed (Cuf) aliyetaka aeleze anajisikiaje kuitwa mzigo namba moja.
Akijibu swali hilo, Pinda alisema yeye anasimamia wizara 20, hivyo kama wapo watakaomhukumu kwa sababu ya wizara moja ama mbili kutofanya vizuri basi watu hao watakuwa hawamtendei haki.
Alisema kama Rais atamwona ameshindwa kuwajibika yuko tayari kuachia ngazi na endapo Rais hatafanya hivyo na wabunge bado wakaona ipo haja hiyo, wampigie kura ya kutokuwa na imani naye.
Kauli ya CCM
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, mbele ya Katibu Mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana, alisema kuwa mawaziri hao wameshindwa kutimiza wajibu wao wa kuwatumikia Watanzania.
Alisema kuwa Waziri Chiza na Malima wamebaki wakifunga tai na kuvaa suti mjini wakati wakulima wa Ruvuma na mikoa mingine ya Tanzania wakiteseka.
Nape alisema Waziri Kawambwa naye anatakiwa kuchukuliwa hatua kwa kuingia mkataba na kampuni ya ujenzi ya Progressive iliyopewa zabuni ya kutengeneza barabara ya Namtumbo hadi Tunduru wakati mkandarasi huyo hana uwezo wa kuijenga na matokeo yake amefukuzwa kazi.
Dk Kawambwa ametupiwa lawama hizo kutokana na kuipa kazi kampuni hiyo wakati akiwa Waziri wa Miundombinu pamoja na kushindwa kusimamia elimu.
“Katibu Mkuu (Kinana), nilimuuliza Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Chiza na Malima wamefika lini kusikiliza matatizo ya wakulima wa tumbaku, korosho na mahindi, alinijibu hakumbuki kama wamefika mkoani hapa. Nikafuatilia na kubaini si yeye tu hata Waziri aliyetangulia Profesa Jumanne Maghembe naye hakuwahi kufika. Najiuliza sababu nini, hakuna majibu,” alisema Nape.
Alisema anasikitishwa na kitendo cha mawaziri hao waliopewa dhamana kushindwa kutambua wajibu wao na kwamba umefika wakati wa kuhojiwa na Kamati Kuu (CC) ya CCM, ili wachukuliwe hatua kwani bila kufanya hivyo aibu itarudi kwa chama chake.
Wabunge wajitosa
Kikao hicho cha CC kinafanyika huku kikiwa na taarifa kwamba wabunge wa chama hicho tawala wameanza kukusanya saini za wabunge, ili kushinikiza kuitishwa kwa kikao cha wabunge hao au Party Cocas.
Uchunguzi wa gazeti hili, uliofanywa kwa siku kadhaa mjini hapa, umebaini kuwa wabunge wa CCM zaidi ya 160 wametia saini katika fomu hiyo wakiwamo mawaziri zaidi ya 10.
Chanzo kimoja cha kuaminika kilisema kuwa fomu hiyo iliwasilishwa katika ofisi ya katibu wa wabunge wa CCM, ikiambatana na barua inayotaka kuitishwa kwa kikao kitakachowakutanisha.
“Tuliwaomba waitishe kikao cha wabunge wa CCM ili mawaziri ambao tunawaona hawatimizi majukumu yao kikamilifu waweze kuhojiwa lakini wakawa wanasuasua,”kilisema chanzo hicho.
“Lakini mmoja wetu akasema kwa kuwa wamepiga chenga ya kukiitisha basi kuna nafasi ya kikanuni ya kukusanya saini za wabunge zaidi ya nusu kushinikiza kuitishwa kwa kikao,”alisema mbunge huyo.
Taarifa ya ziada na Habel Chidawali
Mbunge mwingine wa CCM alisema katika kikao hicho wabunge walitaka kukutanishwa kwa pamoja kati yao, mawaziri wanaoonekana kuwa mzigo na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.
“Kikao hicho tulitaka kiwe Desemba 12 mwaka huu ili tuanze kuwahoji mawaziri kabla ya CC lakini Mwenyekiti (Mizengo Pinda), amekuwa akipiga danadana hadi leo (jana) inapokutana”alisema.
Habari zaidi zilisema baadhi ya wabunge wa CCM walikutana faragha na Kinana juzi jioni na kumtahadharisha kama mawaziri hao wasipowajibishwa, CCM kitakuwa na wakati mgumu.
Vuguvugu linaloendelea hivi sasa ndani ya wabunge wa CCM, liliwahi kujitokeza Bunge la Aprili mwaka jana na kumlazimisha Rais Kikwete kupangua Baraza lake Mawaziri Mei 4,2012.
Kung’olewa kwa mawaziri sita waliokuwa wakishinikizwa na wabunge wajiuzulu kulitokana na taarifa za kamati za kudumu za bunge na za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Katika baraza lake hilo jipya, Rais aliwatosa mawaziri waliokuwa wakishinikizwa kujiuzulu akiwemo Waziri wa Fedha, Mustafa Mkullo na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Cyril Chami.
Wengine waliotoswa kwa shinikizo hilo lililoungwa mkono na kambi ya upinzani ni wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, wa Nishati na Madini, William Ngeleja na wa Uchukuzi, Omar Nundu.
Pia Naibu Waziri wa Uchukuzi wa wakati huo, Dk Athuman Mfutakamba naye alitoswa sambamba na Waziri wa Afya, Dk Haji Hussein Mponda na Naibu wake, Dk Lucy Nkya.

Afrika Kusini Maelfu wakwama kumuaga Mandela

mandela+clipWananchi wa Afrika ya Kusini wakishuhudia mwili wa rais Mstaafu Hayati Mzee Nelson Mandela ulipokuwa ukitoka Ikulu. Picha na mpigapicha wetu 
……………………………………………………………………………..
Pretoria. Maelfu ya wananchi wa Afrika Kusini wameshindwa kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Rais wa Kwanza mzalendo wa nchi hiyo, Nelson Mandela kutokana na muda uliopangwa kumalizika.
Kuanzia Jumatano wiki hii hadi jana, mwili wa Mandela aliyefariki dunia Desemba 4 mwaka huu, ulikuwa ukiwekwa katika Ikulu ya Pretoria, iliyopo ndani ya Majengo ya Umoja (Union Buildings), kila asubuhi kwa ajili ya wananchi kutoa heshima za mwisho.
Jana ilikuwa siku ya mwisho ya utoaji wa heshima hizo na hadi muda uliowekwa ulipokwisha saa 11:30 jioni, kulikuwa na maelfu ya watu waliokosa fursa ya kumuaga mpendwa wao huyo.
Dalili za idadi kubwa ya watu kukosa nafasi hiyo adhimu zilianza kuonekana Jumatano na baadaye juzi Alhamisi kwani hadi muda wa kufunga ulipofika jioni, maelfu ya watu walirejea nyumbani bila kupata fursa ya kuaga.
Jana mchana, Serikali ilitoa taarifa kwamba kwa kuzingatia idadi ya watu waliojitokeza kutoa heshima zao za mwisho, ilikuwa vigumu kwa watu wote kufikiwa.
“Hatuwezi kuahidi kwamba kila mtu ambaye amejipanga hivi sasa kwenye mstari atapata nafasi ya kufika katika Majengo ya Umoja, tunawaomba wananchi wasiende tena huko,” ilisema taarifa iliyotolewa na Idara ya Habari na Mawasiliano ya Serikali (GICS) jana na kuongeza:
“Tunawashukuru sana wananchi kwa kujitokeza, lakini sasa tunawaomba wale ambao hawakuweza kupata fursa ya kutoa heshima zao za mwisho, wafanye hivyo kwa kutumia njia zao wenyewe.”
Waziri katika Ofisi ya Rais, Collins Chabane, alisema kuwa hakuna jinsi ya kuwasaidia watu watakaokosa fursa ya kuaga na kwamba Serikali pamoja na familia wamejitahidi kiasi cha kutosha.
Serikali ilisitisha utaratibu wa usafiri kwa watu waliokuwa wakienda kuaga kuanza saa 8:00 mchana hali iliyozua mvutano baina ya maelfu ya waombolezaji na vyombo vya usalama.
Wengine waliokuwa wameishapanda kwenye mabasi na kufika Ikulu waliambiwa kwamba hawataweza kufikiwa hali iliyozidisha manung’uniko.
Ulinzi ni mkali na Rais Jacob Zuma jana aliliarifu Bunge kwamba amewaajiri kwa siku 15 Askari 11,894 kutoka Jeshi la Afrika Kusini (SANDF), ili wasaidiane na polisi katika ulinzi na usalama wakati wa maombolezo na mazishi ya Mandela.
Wakesha viwanjani
Maelfu ya wananchi walikuwa katika makutano ya barabara za kuelekea Ikulu kuanzia saa 10 alfajiri na wengine walisema walilala jirani na eneo hilo ili waweze kupata fursa ya kumuaga Mandela.
Miongoni mwa waliotoa heshima za mwisho ni ujumbe kutoka Venezuela, ambao ulimzawadia Mandela upanga wa dhahabu na kumkabidhi mjukuu wake wa kwanza, Mandla.
Mandla kwa siku tatu mfululizo amekuwa akiketi pembeni mwa jeneza la babu yake, wakati waombolezaji wakiaga na wakati wote ameonekana mwenye mawazo mengi na huzuni kubwa.
Ndani ya kibanda ambamo mwili wa Mandela uliwekwa kulikuwa na ukimya, ambao mara kadhaa ulivunjwa na kelele za vilio na majonzi kutoka kwa watu walioshindwa kujizuia.
Polisi na wasaidizi mara kadhaa walikuwa wakiwasaidia wale waliozidiwa au wale walioanguka baada ya kuona sura ya marehemu Mandela.
Mapema asubuhi, wengi walijipanga pembezoni mwa barabara kutoka Hospitali ya Jeshi hadi Ikulu, wakiimba nyimbo za kumsifu Mandela na wakati msafara uliokuwa ukisindikiza mwili wake ulipokuwa ukipita, wengine walisikika wakisema; “Siyabinga Tata Madiba…” (wakimaanisha ahsante Baba Madiba).
Wengine walionekana wakiwa wamekwea juu ya miti ili kuweza kuuona vizuri msafara huo wa magari zaidi ya 40, huku baadhi ya watu waliokuwa kazini wakionekana kutoka na kupungia msafara huo.
Wakati huo helikopta za SANDF na polisi zilikuwa zikizunguka katika anga la Jiji la Tswane ndani ya Pretoria na wakati mwili wa Mandela ulipoingizwa Ikulu zilizunguka eneo hilo kwa zaidi ya nusu saa kabla ya kuondoka.
CHANZO: MWANANCHI

Lowassa anusurika ajali ya ndege Arusha

lowassa+clip 
Abiria 37 waliokuwa wamesafaria ndege ya Shirika la Precision Air, akiwamo Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, jana walinusurika kifo, baada ya magurudumu manne ya ndege hiyo kupasuka ilipokuwa ikitua katika Uwanja wa Ndege wa Arusha. 
………………………………………………………………………..
Arusha. Abiria 37 waliokuwa wamesafaria ndege ya Shirika la Precision Air, akiwamo Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, jana walinusurika kifo, baada ya magurudumu manne ya ndege hiyo kupasuka ilipokuwa ikitua katika Uwanja wa Ndege wa Arusha.
Tukio hilo la aina yake, lilitokea saa 6:15 mchana, wakati ndege hiyo, ikitua kutoka jijini Dar es Saalam, ikiwa na abiria hao 37, marubani wawili na wahudumu wawili.
Kamanda wa polisi mkoani Arusha, Liberatus Sabas alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kueleza hakuna majeruhi aliyeripotiwa.
“Hadi sasa hali ni shwari, ndege iliweza kusimama licha ya kupasuka magurudumu. Kiutaratibu uchunguzi umeanza kufanywa na wataalamu husika,”alisema Kamanda Sabas.
Ofisa Mwendeshaji wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini (TCAA), wa Uwanja wa Ndege Arusha, Roland Mwalyambi, alisema kuwa katika tukio hilo, hakuna abiria aliyejeruhiwa licha ya kupata mshtuko mkubwa.
“Uchunguzi wa ajali hii umeanza, lakini hakuna majeruhi, abiria wote walifanikiwa kushuka salama,”alisema Mwalyambi.
Alisema ndege hiyo, kama ingetua salama ilitarajiwa kusafiri kurejea Dar es Salaam kupitia Zanzibar, lakini abiria waliotarajia kusafiria ndege hiyo, walipelekwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro ili kuendelea na safari.
Katika ndege hiyo, pia kulikuwa na maofisa mbalimbali wa Serikali na Jeshi la Wananchi, ambao leo wanatarajia kuhudhuria sherehe ya kutolewa kamisheni kwa maofisa wa jeshi katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli(TMA), ambapo Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.
Tukio hilo la ndege kupata ajali katika uwanja huo ni la pili kutokea mwaka huu, kwani mapema mwaka huu, mfanyabiashara maarufu wa Mkoa wa Kilimanjaro na Arusha, Babu Sambeki alipata ajali pia katika uwanja huo, wakati akijiandaa kutua na ndege yake.
Mfanyabiashara huyo, alifariki papo hapo baada ya moja ya mabawa ya ndege kunasa katika matawi ya mti jirani na uwanja huo. Hata hivyo, taarifa ya ajali hiyo hadi sasa haijawekwa hadharani.
Kukosekana kwa taa katika uwanja huo, ambao umekuwa ukitumiwa na ndege nyingi ndogo hasa za watalii, imekuwa ni kero kubwa na mara kadhaa safari zimeahirishwa kutokana na tatizo hilo.
CHANZO: MWANANCHI

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI

DSC004611
WILAYA YA MBARALI – MAUAJI.
MNAMO TAREHE 1.12.2013 MAJIRA YA SAA 12:00HRS HUKO KATIKA KIJIJI CHA MPAKANI BARABARA KUU YA MBEYA/NJOMBE KATA YA IGAWA TARAFA YA   RUJEWA WILAYA YA MBARALI MKOA WA MBEYA.  MTU MMOJA ASIYEFAHAMIKA JINA WALA MAKAZI YAKE, JINSI YA  KIUME MWENYE UMRI KATI YA  MIAKA 37-40 ALIKUTWA AMEUAWA KWA KUCHOMWA KISU KICHWANI NA SHINGONI NA MTU/WATU WASIOFAHAMIKA KISHA MWILI WAKE KUTUPWA KANDO YA  BARABARA HIYO. CHANZO CHA MAUAJI KINACHUNGUZWA. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA HOSPITALI YA WILAYA YA MBARALI KWA UCHUNGUZI. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA NAIBU KAMISHNA WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA YA MAHALI ALIPO MTU/WATU WALIOHUSIKA NA TUKIO HILI AZITOE KATIKA MAMLAKA HUSIKA ILI WAKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE.
WILAYA YA MOMBA – AJALI YA GARI KUMGONGA MTEMBEA KWA MIGUU NA
                                        KUSABABISHA KIFO.
MNAMO TAREHE 13.12.2013 MAJIRA YA SAA 14:30HRS HUKO MAENEO YA MTAA WA MWAKA   BARABARA YA TUNDUMA/SUMBAWANGA KATA YA TUNDUMA, TARAFA YA TUNDUMA, WILAYA YA MOMBA, MKOA WA MBEYA. GARI T. 904 BXV AINA YA M/CANTER LIKIENDESHWA NA DEREVA MAAMZEE S/O MOHAMED, MIAKA 21, MNYIHA, MKAZI WA MTAA WA MWAKA – TUNDUMA  LILIMGONGA MTEMBEA KWA MIGUU ASIYEFAHAMIKA JINA WALA MAKAZI YAKE, JINSI YA  KIKE, UMRI KATI YA  MIAKA 25-30 NA KUSABABISHA KIFO CHAKE PAPO HAPO. CHANZO CHA AJALI NI MWENDO KASI. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KITUO CHA AFYA TUNDUMA KWA AJILI YA UCHUNGUZI. MTUHUMIWA AMEKAMATWA NA TARATIBU ZA KUMFIKISHA MAHAKAMANI ZINAENDELEA.  KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA NAIBU KAMISHNA WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA MADEREVA KUWA MAKINI WANAPOTUMIA VYOMBO VYA MOTO KWA KUFUATA SHERIA NA ALAMA ZA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUKA AJALI ZINAZOWEZA KUEPUKIKA HASA KATIKA KIPINDI HIKI CHA KUELEKEA MWISHO WA MWAKA.
Signed by:
[DIWANI ATHUMANI – DCP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

ULIMWENGU, SAMATTA, WAPATA SHAVU LA KIM

Posted: 02 Dec 2013 10:58 PM PST
  • NI WAKATI WA KUIVAA BURUNDI CHALLENGE
 Na Mwandishi Wetu, Nairobi
 Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars, Kim Poulsen alisema kwamba kuwasili katika kikosi chake kwa wachezaji Thomas Ulimwengu na Mbwana Samatta kungeongeza nguvu katika kikosi hicho hasa katika mchezo wao wa Kombe la Challenji dhidi ya Burundi
Samatta na Ulimwengu waliwasili jijini Nairobi wakitokea kuichezea timu yao, TP Mazembe ya DRC katika Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika, ambayo walifungwa jumla ya mabao 3-2 na timu ya CS Sfaxien ya Tunisia na hivyo kukosa kombe.
Akizungumza jijini Nairobi, Kim alisema ujio wa wachezaji hao ingekuwa ni ahueni katika kikosi chake ambacho bado kilikuwa kinakabiliwa na mechi ngumu dhidi ya Burundi kwani aliiona timu hiyo na aliipa matumaini katika kuleta upinzani mkali.
"Wachezaji niliokuwa nao walikuwa ni wazuri lakini kuongezeka kwa Samatta na Ulimwengu pia kuliongeza nguvu zaidi katika kikosi changu, hivyo nilitegemea mechi ya Jumatano ingekuwa nzuri zaidi," alisema kocha huyo.
Alisema timu zote zilizoshiriki michuano hiyo hakuna timu kibonde, hivyo hata walipovuka robo fainali bado walikuwa na kazi ngumu katika kuhakikisha wanatwaa kombe hilo na kurudi nalo Tanzania.
Kim alisema kuna kila sababu za kuboresha kikosi chake, kwani kuna mapungufu ambayo aliyagundua walipocheza na Somalia, hivyo anatakiwa kuyafanyia kazi haraka kabla ya michuano m ingine kuja.

KAMPUNI ZASHAURIWA KUHUSU AFYA ZA WAFANYAKAZI

Posted: 02 Dec 2013 10:47 PM PST
 Kampuni na taasisi mbalimbali nchini zimeshauriwa kujua hali ya afya za wafanyakazi kwa sababu itasaidia pia kuongeza mchango wao uzalishaji katika sehemu zao za kazi, anaripoti Mwandishi Wetu.
Kauli hii ilitolewa hivi karibuni jijini Dar es Salaam na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam (RAS),Teresia Mbando wakati wa maadhimisho ya Siku ya UkimwiDuniani katika makao makuu ya Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).
Bi.Mbando alisema huku suala la maambukuzi ya VVU / Ukimwi yakiwa yanaongezeka, ni muhimu kwa kampuni na taasisi kuchukua hatua ya kujua hali ya afya za wafanyakazi wake akisema kuwa kwa kufanya hivyo itakuwa ni kutekeleza harakati na mpango wa serikali wa mapambano dhidi ya Ukimwi.
Alisema Serikali imekuwa mstari wa mbele katika kutokomeza ugonjwa huo na kusema kuwa kwa 'kauli mbiu ya mwaka huu katika maadhimisho ya siku ya Ukimwi ya " kufikia asilimia sifuri katika maambukizi mapya,unyanyapaa na idadi ya vifo vinavyotokana na Ukimwi, inaonyesha kwamba juhudi zaidi zimeelekezwa kwenye mapambano dhidi ya ugonjwa huo.
Mbando aliipongeza TBL kwa kuweka mbele suala la afya ya wafanyakazi wake na kutoa wito kwa kampuni na taasisi nyingine kuiga mfano huo, kwani kwa kufanya hivyo kutapunguza kwa kiasi kiwango kikubwa cha maambukizi mapya.
Kwa upande wake, Meneja Rasilimali wa TBL, David Magesa alisema tokea mwaka 1990, kampuni hiyo ilikuwa na mpango ambao unawawezesha kupata huduma ya upimaji wa hiari na Ushauri nasaha.
Magesa alisema pia hadi sasa asilimia 80 ya wafanyakazi wa TBL wanajua hali ya afya zao, akibainisha kuwa mpango huu unafanyika kutokana na kuungwa mkono na utawala wa kampuni hiyo.
"Mbali na upimaji wa hiari na Ushauri nasaha, kampuni kupitia kliniki yake ambayo imejitosheleza inatoa bure dawa za kurefusha maisha (ARVs) na mpango huo pia unashirikisha zaidi ya asilimia 40 ya wanafamilia wa wafanyakazi," alisema.
Aidha, Magesa alisema kupitia programu hiyo wameweza kupunguza idadi ya vifo kwa asilimia 99.9 pamoja na kupunguza kesi za maambukizi ya magonjwa ya zinaa (STDs) na kuongezea kuwa programu hiyo imekuwa ya manufaa makubwa si tu klwa wafanyakazi bali hata wasio wafanyakazi wa kampuni hiyo.
Mbali na hayo alisema kuwa kampuni hiyo hadi sasa ina waelimishaji rika 116 ambao wanashiriki katika kutoa ushauri kwa wafanyakazi wenzao ili kuwafanya wawe na ufahamu katika kutambua umuhimu wa kujua hali ya afya zao.

MIAKA 20 JELA WOTE WALIOKUTWA NA MENO YA TEMBO

Posted: 02 Dec 2013 10:38 PM PST
Watu wawili akiwemo mlinzi wa nyumba moja mkoani Tanga, wamehukumumiwa kifungo cha miaka 20 gerezani kila mmoja baada ya kupatikana na hatia ya kupakua na kuhifadhi meno ya tembo 114 yenye thamani ya sh. milioni 44,044 kinyume cha sheria, anaripoti Mashaka Mhando, Tanga.
Washtakiwa hao ni Bw. Joseph Mwarabu na Bw. Richard Abdallah, ambapo hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Tanga, Mairasaanane Kashonde.
Hakimu Kashonde alisema, washtakiwa walitiwa hatiani chini ya Sheria ya Uhifadhi ya Wanyamapori kifungu cha 86 (i), (ii) C na Kifungu 14 D, cha sheria ya uhujumu uchumi sura 200 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.
Akisoma hukumu hiyo, alisema washtakiwa hao walishiriki kushusha meno hayo kutoka kwenye gari la jeshi na kuyahifadhi kwenye nyumba ambayo haikuwa mali yao.
“Mah a k ama ime s h in dwa kumhusisha mmiliki wa nyumba hiyo, Bw. Michael Kijangwa ambaye wakati huo hakuwepo, hivyo mshtakiwa wa kwanza na pili mnatiwa hatiani kwa kuhusika kikamilifu katika tukio hili,” alisema.
Kwa upande wake, Mwanasheria wa Serikali, Veridiana Mlenza akiwa na mwenzake Sabrina Joshi, waliiomba mahakama hiyo itoe adhabu kali kwa washtakiwa kwani matukio ya watu kukutwa na meno hayo yamekuwa yakiongezeka.
“Ni vyema mahakama itoe adhabu kali ili iwe fundisho kwa wengine kutokana na ongezeko la vitendo hivi,” walisema.
Washtakiwa hao walipotakiwa kujitetea, kila mmoja aliiomba mahakama isiwape adhabu kali kwani wana familia ambazo zinawategemea.
Hakimu Kashonde alisema kwa mujibu wa Sheria ya Wanyamapori, inatoa fursa kwa hakimu kutoza faini mara kumi ya thamani ya nyara inayokamatwa kwa mshtakiwa lakini aliwahukumu kifungo hicho iwe fundisho kwa wengine.
Washtakiwa hao wanadaiwa kutenda kosa hilo Januari Mosi 2010, katika Mtaa wa Chumbageni, kwenye nyumba inayomilikiwa na Bw. Kijangwa na walikutwa wakiwa na vipande hivyo.
Shtaka la pili ambalo lilikuwa likiwakabili washtakiwa hao, inadaiwa Desemba 31, 2009, huko Chumbageni, walishindwa kutoa taarifa juu ya uwepo wa nyara za serikali kwenye nyumba ambayo walikuwa wakifanya kazi.
Hata hivyo, washtakiwa hao walikana na kudai meno hayo hayakuwa ya kwao bali ya bosi wao Bw. Kijangwa ambaye kwa wakati huo alikuwa Lushoto na familia yake ambako walikwenda kula sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya.
Inadaiwa meno hayo yalipelekwa katika nyumba hiyo iliyopo jirani na Hospitali ya Tumaini, eneo la Chumbageni na gari la Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na maofisa wawili Desemba 31, 2009.


MATAJIRI WA MAGARI WAMHOFIA MAGUFULI

Posted: 02 Dec 2013 10:35 PM PST
Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli, amesema ataendelea kusimamia sheria ya barabara namba 30 ya mwaka 1973 hadi anaingia kaburini kwa kuhakikisha hakuna magari ambayo yanazidisha uzito na kuharibu barabara, anaripoti Goodluck Hongo.
Dkt. Magufuli aliyasema hayo Dar es Salaam jana katika hafla ya kutilia saini mikataba mitatu ya ujenzi wa barabara za Dodoma- Manyara inayopita Mayamaya- Babati-Bonga.
Barabara nyingine ni Tunduru- M a n g a k a - Mtambaswala na kusema kuwa, barabara hizo z i n a j e n gwa kwa gharama kubwa hivyo watendaji wote wa Wizara ya Ujenzi kupitia
 Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), wanapaswa kusimamia sheria.
Alisema usimamizi makini wa sheria za barabara, utasaidia kuzifanya zidumu zaidi kwani Rais Jakaya Kikwete ameiagiza Wizara hiyo kusimamia sheria ambapo kitendo cha wamiliki wa magari kuzidisha uzito, kinamchukiza sana.
“Sipo tayari kuona matajiri wachache wakiharibu barabara na kujipatia faida kubwa wakati barabara hizi zinajengwa kwa mkopo unaolipwa na kodi za wananchi.
“Msema kweli ni mpenzi wa Mungu, mimi nitaendelea kusimamia sheria hadi naingia kaburini kwa kuhakikisha hakuna magari yanayozidisha uzito na kuharibu barabara,” alisema Dkt. Magufuli.
Aliongeza kuwa, kama matajiri hao wataachiwa waendelee kuzidisha uzito, barabara zilizopo hazitadumu kwa muda mrefu na wananchi maskini wataendelea kulipa kodi.
“Nchini Ujerumani, uzito wa magari yote ni tani 40, Uingereza tani 40, Ufaransa 40, Urusi 38 lakini Tanzania tani 56, wakati mwingine tunakamata hadi tani 96,” alisema.
Akiwazungumzia wakandarasi waliochukua zabuni ya ujenzi wa barabara hizo, Dkt. Magufuli aliwaonya na kusisitiza kama hawawezi kazi ni bora wasisaini mikataba hiyo ili watafute wakandarasi wengine wenye uwezo.
Alisema kama wamekubali kusaini, wanapaswa kuanza kazi mara moja kwani Serikali ndio iliyokopa na walipakodi ni Watanzania hivyo si kukaa miezi sita ndio waanze kazi.
“Mameneja wa TANROADS katika mikoa ambayo miradi hii inafanyika, lazima msimamie kikamilifu ujenzi huu na kama mradi ukisuasua katika eneo lako ujue hutufai kufanya kazi hivyo uondoke mara moja,” alisema.
Kwa upande wake, mbunge wa Kasulu Mjini, mkoani Kigoma, Bw. Moses Machali (NCCR-Mageuzi), aliipongeza Serikali kwa kusikia kilio cha wananchi na kuwajengea barabara na daraja la Mto Malagarasi ambapo yeye si mhafidhina; bali kama serikali imefanya mema inapaswa kupongezwa.
“Jema ni jema tu hata kama likifanywa na nani hivyo mimi si mhafidhina, kama Serikali imefanya mema basi inapaswa kupongezwa,” alisema.
Aliongeza kuwa, licha ya Serikali kuwajengea Daraja la Mto Malagarasi, bado barabara zingine ikiwemo ya Nyakanazi ina hali mbaya, hivyo pamoja na kuipongeza serikali kwa kusaini mikataba hiyo, utekelezwaji wake ni jambo lingine.
“Kusaini mkataba ni jambo moja na Mkandarasi kufika eneo la mradi ni hatua nyingine, Daraja la Mto Malagarasi halitoshi bali tunaomba Barabara ya Nyakanazi nayo iwekwe lami,” alisema.
Naye Mbunge wa Viti Maalumu, Mkoa wa Dodoma kwa tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF), Bi. Moza Abeid Said, alisema anaipongeza serikali ya CCM kwa kutekeleza ahadi zake, lakini zisifanywe karibu na uchaguzi kwani kilio cha barabara hizo ni cha muda mrefu.
Alisema ingawa yeye ni Mbunge kutoka upinzani, anaipongeza Serikali hasa inapotatua kero za wananchi bali wasiwasi mkubwa ni utekelezaji wake kwani wabunge wamekuwa wakilalamikia miradi mingi ambayo imesainiwa lakini haijatekelezwa.
“Waziri Magufuli ameweza kutekeleza ilani ya CCM katika sekta ya miundombinu ya barabara... amefanya kazi nzuri, barabara ya Babati-Iringa ikijengwa kama walivyosaini mikataba, itawasaidia sana wananchi wa Mkoa wa Dodoma,” alisema.
Naye Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Mhandisi Patrick Mfugale, alisema mradi huo unatekelezwa kwa awamu ya pili ambapo awamu ya kwanza ulitekelezwa kwa mkopo wa sh. bilioni 472 na awamu ya utatekelezwa kwa gharama ya sh. bilioni 538.88.
Alisema fedha zimetoka katika Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) na nyingine kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) ambapo fedha nyingine zimetoka serikalini. Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na wabunge wote kutoka mikoa ya Manyara, Dodoma, Mtwara na Ruvuma ambao miradi hiyo inapita katika majimbo yao.


WAUMINI WAMFUNGUA LOWASSA

Posted: 02 Dec 2013 10:33 PM PST

Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Bw. Edward Lowassa (mwenye suti),akiwaaga waumini wa Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Mtandi,Wilaya ya Masasi,mkoani Mtwara,baada ya kuendesha harambee ya kuchangia shughuli za maendeleo ya Ushirika wa Mama wa Kikristo (UMAKU),mwishoni mwa wiki ambapo sh.milioni 103 zilichangwa katika harambee hiyo. Kulia kwake ni Askofu wa Kanisa hilo,Dayosisi ya Newala,Oscar Mnung'a.

  •   ACHANGISHA MILIONI 103/-,AMMWAGIA  SIFA MKAPA

Na Mwandishi Wetu, Masasi

  Waziri Mkuu aliyejiuzulu ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Bw. Edward Lowassa, amesema yuko tayari kushirikiana na mtu yeyote katika mapambano ya kuondoa umaskini kwenye jamii.

Bw. Lowassa aliyasema hayo mwishoni mwa wiki Mjini Masasi mkoani Mtwara, katika harambee iliyofanyika kwenye Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Masasi, mkoani humo.

Harambee hiyo ilikuwa na lengo la kuchangia shughuli za maendeleo za Ushirika wa Mama wa Kikristo (UMAKI) na kusisitiza kuwa, yeye ni mdau wa mapambano hayo.

“Mtu yeyote anayepambana kuondoa umaskini katika jamii, niko tayari kushirikiana naye katika harambee za harakati hizi,” alisema Bw. Lowassa na kuongeza kuwa, wanawake ni jamii inayochukia sana suala zima la umaskini.

“Wanawake ni wadau wakubwa wa kupambana na umaskini ndiyo maana chama changu CCM, katika rasimu ya Katiba Mpya inataka kuwe na asilimia 50 kwa 50 ya uwakilishi bungeni kati ya wanawake na wanaume kwa sababu kinawapenda,” alisema.

Alisema kwa sababu hiyo, ndiyo maana ameridhia kushiriki harambee hiyo ambapo kufika kwake kanisani hapo kumetokana na Wilaya hiyo kutoa kiongozi makini, mwadilifu na shupavu mkubwa Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Bw. Benjamin Mkapa.

“Hapa pana historia ya kutoa kiongozi aliyeiongoza nchi yetu kwa uadilifu na umakini mkubwa, walikuwepo watu waliyojaribu kumsema sema katika vyombo vya habari.

“Mwisho wa siku watu hao wamekiri kuwa Bw. Mkapa alikuwa kiongozio makini,” alisema Bw. Lowassa ambaye wakati kiongozi huyo akiwa madarakani, alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano kabla ya kupelekwa Wizara ya Maji na Mifugo.

Katika harambee hiyo, zaidi ya sh. milioni 103 zilipatikana ambapo Bw. Lowassa na marafiki zake alichangia sh. milioni 10 na kuvuka lengo ambalo lilikuwa sh. milioni 100.

HABARI ZA ZITTO KUKATISHA ZIARA YA SLAA

Posted: 02 Dec 2013 10:09 PM PST
  • CHADEMA KIGOMA YASHTUKIA MCHEZO MCHAFU
  • HOFU YA KUTOKEA VURUGU YATANDA MAJIMBONI 
Na Mwajabu Kigaza, Kigoma
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), mkoani Kigoma, kimesitisha ziara ya Katibu Mkuu wa chama hicho Taifa, Dkt. Wilbrod Slaa, ambayo ilipangwa kufanyika mkoani humo kuanzia Desemba 5 hadi 13 mwaka huu, kutokana na hofu ya usalama miongoni mwa wanachama wake.

Mwenyekiti wa chama hicho mkoani humo, Jafari Kasisiko, aliyasema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa, usalama katika baadhi ya majimbo mkoani humo ni mdogo sana.
Alisema kutokana na hali hiyo, wameona ni bora ziara hiyo isitishwe kwanza ili kuepusha machafuko yaliyoandaliwa na wanachama dhidi ya Dkt. Slaa kama atafika mkoani humo.
“Uamuzi wa kusitisha ziara hii umefikiwa katika Kikao cha Baraza la Uongozi mkoani hapa kilichofanyika Desemba Mosi, mwaka huu na kushirikisha viongozi wa majimbo mengine.
“Majimbo haya ni Kigoma Mjini, Kaskazini na Kusini ambao kwa pamoja walielezea uwepo wa njama za kuhujumu ziara hii ili kumdhalilisha Dkt. Slaa,” alisema.
Aliyataja majimbo yaliyodaiwa kuchafuka kisiasa kutokana na maamuzi ya Kamati Kuu ya CHADEMA kumvua nyadhifa za uongozi aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Bara, Bw. Zitto Kabwe kuwa ni Kigoma Mjini, Kaskazini na Kusini, wakati ambapo majimbo ya Buhigwe, Kasulu, Muhambwe na Buyungu pia hali ya usalama imedaiwa kuwa ya mashaka.
Akizungumzia msimamo wa chama hicho mkoani humo kuhusu uamuzi wa Kamati Kuu kumvua uongozi Bw. Kabwe kwa madai ya kutaka kukisaliti chama, alisema kikao hicho kilikuwa halali.
“Hatua zote za kumvua uongozi Bw. Kabwe na wenzake Dkt. Kitila Mkumbo na Bw. Samson Mwigamba, zilifuatwa sasa kama anadhani ameonewa, ana haki ya kukata rufaa Baraza Kuu.
“Ziara ya Dkt. Slaa hapa Kigoma, haina uhusiano na maamuzi ya Kamati Kuu kwani ilipangwa muda mrefu na kusitishwa kutokana na vikao vya Kamati Kuu, lengo la ziara hii ni maandalizi ya uchaguzi ujao ngazi za chini,” alisema.
Aliwataka baadhi ya wanachama wanaoendesha vitendo vya vurugu na kuhujumu miundombinu ya chama kuacha kufanya hivyo kwani ni kinyume cha maelekezo ya chama kwani palipo na vurugu hakuna haki.
Baadhi ya wanachama wa chama hicho kutoka majimbo yaliyotajwa kuwa na vurugu, walikutana Mjini Kigoma katika moja ya kumbi za mikutano kupinga ujio wa Dkt. Slaa, Desemba 5 mwaka huu.
Akisoma tamko la wanachama hao, Fanuel Sindika alisema wameikataa ziara hiyo kwa sababu CHADEMA kimekuwa kikiwaonea baadhi ya viongozi hasa kutoka mikoa ya Magharibi na wapo tayari kufanya vurugu ili kumdhalilisha kiongozi huyo.
Alisema hawakubaliani na maamuzi yaliyotolewa na Kamati Kuu dhidi ya Bw. Kabwe ambayo hayajazingatia haki kwa mujibu wa katiba.
Aliongeza kuwa, kwa muda mrefu chama hicho kimekuwa na mgogoro unaotokana na hofu ya madaraka katika nafasi ya Mwenyekiti wa chama ambayo inadaiwa kuwaniwa na Bw. Kabwe akisaidiwa na rafiki zake kwenye kampeni ili kuhakikisha anashinda kiti hicho.
Hivi karibuni, baadhi ya vijana kutoka Tawi la Mwandiga, Jimbo la Kigoma Kaskazini, walifanya maandamano ya pikipiki na kuburuza bendera barabarani, kuchoma kadi, bendera na kuvunja bango la Tawi la Msingi katika kijiji hicho