Posted: 02 Dec 2013 10:47 PM PST
 Kampuni
 na taasisi mbalimbali nchini zimeshauriwa kujua hali ya afya za 
wafanyakazi kwa sababu itasaidia pia kuongeza mchango wao uzalishaji 
katika sehemu zao za kazi, anaripoti Mwandishi Wetu. 
Kauli
 hii ilitolewa hivi karibuni jijini Dar es Salaam na Katibu Tawala wa 
Mkoa wa Dar es Salaam (RAS),Teresia Mbando wakati wa maadhimisho ya Siku
 ya UkimwiDuniani katika makao makuu ya Kampuni ya Bia Tanzania (TBL). 
Bi.Mbando
 alisema huku suala la maambukuzi ya VVU / Ukimwi yakiwa yanaongezeka, 
ni muhimu kwa kampuni na taasisi kuchukua hatua ya kujua hali ya afya za
 wafanyakazi wake akisema kuwa kwa kufanya hivyo itakuwa ni kutekeleza 
harakati na mpango wa serikali wa mapambano dhidi ya Ukimwi. 
Alisema
 Serikali imekuwa mstari wa mbele katika kutokomeza ugonjwa huo na 
kusema kuwa kwa 'kauli mbiu ya mwaka huu katika maadhimisho ya siku ya 
Ukimwi ya " kufikia asilimia sifuri katika maambukizi mapya,unyanyapaa 
na idadi ya vifo vinavyotokana na Ukimwi, inaonyesha kwamba juhudi zaidi
 zimeelekezwa kwenye mapambano dhidi ya ugonjwa huo. 
Mbando
 aliipongeza TBL kwa kuweka mbele suala la afya ya wafanyakazi wake na 
kutoa wito kwa kampuni na taasisi nyingine kuiga mfano huo, kwani kwa 
kufanya hivyo kutapunguza kwa kiasi kiwango kikubwa cha maambukizi 
mapya. 
Kwa
 upande wake, Meneja Rasilimali wa TBL, David Magesa alisema tokea mwaka
 1990, kampuni hiyo ilikuwa na mpango ambao unawawezesha kupata huduma 
ya upimaji wa hiari na Ushauri nasaha. 
Magesa
 alisema pia hadi sasa asilimia 80 ya wafanyakazi wa TBL wanajua hali ya
 afya zao, akibainisha kuwa mpango huu unafanyika kutokana na kuungwa 
mkono na utawala wa kampuni hiyo. 
"Mbali
 na upimaji wa hiari na Ushauri nasaha, kampuni kupitia kliniki yake 
ambayo imejitosheleza inatoa bure dawa za kurefusha maisha (ARVs) na 
mpango huo pia unashirikisha zaidi ya asilimia 40 ya wanafamilia wa 
wafanyakazi," alisema. 
Aidha,
 Magesa alisema kupitia programu hiyo wameweza kupunguza idadi ya vifo 
kwa asilimia 99.9 pamoja na kupunguza kesi za maambukizi ya magonjwa ya 
zinaa (STDs) na kuongezea kuwa programu hiyo imekuwa ya manufaa makubwa 
si tu klwa wafanyakazi bali hata wasio wafanyakazi wa kampuni hiyo. 
Mbali
 na hayo alisema kuwa kampuni hiyo hadi sasa ina waelimishaji rika 116 
ambao wanashiriki katika kutoa ushauri kwa wafanyakazi wenzao ili 
kuwafanya wawe na ufahamu katika kutambua umuhimu wa kujua hali ya afya 
zao.
No comments:
Post a Comment