Posted: 02 Dec 2013 10:58 PM PST
- NI WAKATI WA KUIVAA BURUNDI CHALLENGE
 
 Na Mwandishi Wetu, Nairobi
 Kocha
 Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars, Kim Poulsen 
alisema kwamba kuwasili katika kikosi chake kwa wachezaji Thomas 
Ulimwengu na Mbwana Samatta kungeongeza nguvu katika kikosi hicho hasa 
katika mchezo wao wa Kombe la Challenji dhidi ya Burundi
Samatta
 na Ulimwengu waliwasili jijini Nairobi wakitokea kuichezea timu yao, TP
 Mazembe ya DRC katika Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika, ambayo 
walifungwa jumla ya mabao 3-2 na timu ya CS Sfaxien ya Tunisia na hivyo 
kukosa kombe. 
 
Akizungumza
 jijini Nairobi, Kim alisema ujio wa wachezaji hao ingekuwa ni ahueni katika
 kikosi chake ambacho bado kilikuwa kinakabiliwa na mechi ngumu dhidi ya Burundi 
kwani aliiona timu hiyo na aliipa matumaini katika kuleta upinzani mkali. 
 
"Wachezaji
 niliokuwa nao walikuwa ni wazuri lakini kuongezeka kwa Samatta na Ulimwengu pia 
kuliongeza nguvu zaidi katika kikosi changu, hivyo nilitegemea mechi ya 
Jumatano ingekuwa nzuri zaidi," alisema kocha huyo. 
 
Alisema
 timu zote zilizoshiriki michuano hiyo hakuna timu kibonde, hivyo hata 
walipovuka robo fainali bado walikuwa na kazi ngumu katika kuhakikisha 
wanatwaa kombe hilo na kurudi nalo Tanzania. 
 
Kim
 alisema kuna kila sababu za kuboresha kikosi chake, kwani kuna
 mapungufu ambayo aliyagundua walipocheza na Somalia, hivyo anatakiwa 
kuyafanyia kazi haraka kabla ya michuano m ingine kuja. 
 
No comments:
Post a Comment