TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, December 14, 2013

ULIMWENGU, SAMATTA, WAPATA SHAVU LA KIM

Posted: 02 Dec 2013 10:58 PM PST
  • NI WAKATI WA KUIVAA BURUNDI CHALLENGE
 Na Mwandishi Wetu, Nairobi
 Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars, Kim Poulsen alisema kwamba kuwasili katika kikosi chake kwa wachezaji Thomas Ulimwengu na Mbwana Samatta kungeongeza nguvu katika kikosi hicho hasa katika mchezo wao wa Kombe la Challenji dhidi ya Burundi
Samatta na Ulimwengu waliwasili jijini Nairobi wakitokea kuichezea timu yao, TP Mazembe ya DRC katika Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika, ambayo walifungwa jumla ya mabao 3-2 na timu ya CS Sfaxien ya Tunisia na hivyo kukosa kombe.
Akizungumza jijini Nairobi, Kim alisema ujio wa wachezaji hao ingekuwa ni ahueni katika kikosi chake ambacho bado kilikuwa kinakabiliwa na mechi ngumu dhidi ya Burundi kwani aliiona timu hiyo na aliipa matumaini katika kuleta upinzani mkali.
"Wachezaji niliokuwa nao walikuwa ni wazuri lakini kuongezeka kwa Samatta na Ulimwengu pia kuliongeza nguvu zaidi katika kikosi changu, hivyo nilitegemea mechi ya Jumatano ingekuwa nzuri zaidi," alisema kocha huyo.
Alisema timu zote zilizoshiriki michuano hiyo hakuna timu kibonde, hivyo hata walipovuka robo fainali bado walikuwa na kazi ngumu katika kuhakikisha wanatwaa kombe hilo na kurudi nalo Tanzania.
Kim alisema kuna kila sababu za kuboresha kikosi chake, kwani kuna mapungufu ambayo aliyagundua walipocheza na Somalia, hivyo anatakiwa kuyafanyia kazi haraka kabla ya michuano m ingine kuja.

No comments:

Post a Comment