Posted: 02 Dec 2013 10:35 PM PST
Waziri
 wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli, amesema ataendelea kusimamia sheria ya 
barabara namba 30 ya mwaka 1973 hadi anaingia kaburini kwa kuhakikisha 
hakuna magari ambayo yanazidisha uzito na kuharibu barabara, anaripoti Goodluck Hongo.
Dkt.
 Magufuli aliyasema hayo Dar es Salaam jana katika hafla ya kutilia 
saini mikataba mitatu ya ujenzi wa barabara za Dodoma- Manyara inayopita
 Mayamaya- Babati-Bonga. 
Barabara
 nyingine ni Tunduru- M a n g a k a - Mtambaswala na kusema kuwa, 
barabara hizo z i n a j e n gwa kwa gharama kubwa hivyo watendaji wote 
wa Wizara ya Ujenzi kupitia
 Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), wanapaswa kusimamia sheria. 
Alisema
 usimamizi makini wa sheria za barabara, utasaidia kuzifanya zidumu 
zaidi kwani Rais Jakaya Kikwete ameiagiza Wizara hiyo kusimamia sheria 
ambapo kitendo cha wamiliki wa magari kuzidisha uzito, kinamchukiza 
sana. 
“Sipo
 tayari kuona matajiri wachache wakiharibu barabara na kujipatia faida 
kubwa wakati barabara hizi zinajengwa kwa mkopo unaolipwa na kodi za 
wananchi. 
“Msema
 kweli ni mpenzi wa Mungu, mimi nitaendelea kusimamia sheria hadi 
naingia kaburini kwa kuhakikisha hakuna magari yanayozidisha uzito na 
kuharibu barabara,” alisema Dkt. Magufuli. 
Aliongeza
 kuwa, kama matajiri hao wataachiwa waendelee kuzidisha uzito, barabara 
zilizopo hazitadumu kwa muda mrefu na wananchi maskini wataendelea 
kulipa kodi. 
“Nchini
 Ujerumani, uzito wa magari yote ni tani 40, Uingereza tani 40, Ufaransa
 40, Urusi 38 lakini Tanzania tani 56, wakati mwingine tunakamata hadi 
tani 96,” alisema. 
Akiwazungumzia
 wakandarasi waliochukua zabuni ya ujenzi wa barabara hizo, Dkt. 
Magufuli aliwaonya na kusisitiza kama hawawezi kazi ni bora wasisaini 
mikataba hiyo ili watafute wakandarasi wengine wenye uwezo. 
Alisema
 kama wamekubali kusaini, wanapaswa kuanza kazi mara moja kwani Serikali
 ndio iliyokopa na walipakodi ni Watanzania hivyo si kukaa miezi sita 
ndio waanze kazi. 
“Mameneja
 wa TANROADS katika mikoa ambayo miradi hii inafanyika, lazima msimamie 
kikamilifu ujenzi huu na kama mradi ukisuasua katika eneo lako ujue 
hutufai kufanya kazi hivyo uondoke mara moja,” alisema. 
Kwa
 upande wake, mbunge wa Kasulu Mjini, mkoani Kigoma, Bw. Moses Machali 
(NCCR-Mageuzi), aliipongeza Serikali kwa kusikia kilio cha wananchi na 
kuwajengea barabara na daraja la Mto Malagarasi ambapo yeye si 
mhafidhina; bali kama serikali imefanya mema inapaswa kupongezwa. 
“Jema
 ni jema tu hata kama likifanywa na nani hivyo mimi si mhafidhina, kama 
Serikali imefanya mema basi inapaswa kupongezwa,” alisema. 
Aliongeza
 kuwa, licha ya Serikali kuwajengea Daraja la Mto Malagarasi, bado 
barabara zingine ikiwemo ya Nyakanazi ina hali mbaya, hivyo pamoja na 
kuipongeza serikali kwa kusaini mikataba hiyo, utekelezwaji wake ni 
jambo lingine. 
“Kusaini
 mkataba ni jambo moja na Mkandarasi kufika eneo la mradi ni hatua 
nyingine, Daraja la Mto Malagarasi halitoshi bali tunaomba Barabara ya 
Nyakanazi nayo iwekwe lami,” alisema. 
Naye
 Mbunge wa Viti Maalumu, Mkoa wa Dodoma kwa tiketi ya Chama cha Wananchi
 (CUF), Bi. Moza Abeid Said, alisema anaipongeza serikali ya CCM kwa 
kutekeleza ahadi zake, lakini zisifanywe karibu na uchaguzi kwani kilio 
cha barabara hizo ni cha muda mrefu. 
Alisema
 ingawa yeye ni Mbunge kutoka upinzani, anaipongeza Serikali hasa 
inapotatua kero za wananchi bali wasiwasi mkubwa ni utekelezaji wake 
kwani wabunge wamekuwa wakilalamikia miradi mingi ambayo imesainiwa 
lakini haijatekelezwa. 
“Waziri
 Magufuli ameweza kutekeleza ilani ya CCM katika sekta ya miundombinu ya
 barabara... amefanya kazi nzuri, barabara ya Babati-Iringa ikijengwa 
kama walivyosaini mikataba, itawasaidia sana wananchi wa Mkoa wa 
Dodoma,” alisema. 
Naye
 Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Mhandisi Patrick Mfugale, alisema mradi huo 
unatekelezwa kwa awamu ya pili ambapo awamu ya kwanza ulitekelezwa kwa 
mkopo wa sh. bilioni 472 na awamu ya utatekelezwa kwa gharama ya sh. 
bilioni 538.88. 
Alisema
 fedha zimetoka katika Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) na nyingine 
kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) ambapo fedha nyingine zimetoka
 serikalini. Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na wabunge wote kutoka mikoa ya
 Manyara, Dodoma, Mtwara na Ruvuma ambao miradi hiyo inapita katika 
majimbo yao.
No comments:
Post a Comment