Posted: 02 Dec 2013 10:38 PM PST
Watu
 wawili akiwemo mlinzi wa nyumba moja mkoani Tanga, wamehukumumiwa 
kifungo cha miaka 20 gerezani kila mmoja baada ya kupatikana na hatia ya
 kupakua na kuhifadhi meno ya tembo 114 yenye thamani ya sh. milioni 
44,044 kinyume cha sheria, anaripoti Mashaka Mhando, Tanga. 
Washtakiwa
 hao ni Bw. Joseph Mwarabu na Bw. Richard Abdallah, ambapo hukumu hiyo 
ilitolewa na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Tanga, Mairasaanane 
Kashonde. 
Hakimu
 Kashonde alisema, washtakiwa walitiwa hatiani chini ya Sheria ya 
Uhifadhi ya Wanyamapori kifungu cha 86 (i), (ii) C na Kifungu 14 D, cha 
sheria ya uhujumu uchumi sura 200 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002. 
Akisoma
 hukumu hiyo, alisema washtakiwa hao walishiriki kushusha meno hayo 
kutoka kwenye gari la jeshi na kuyahifadhi kwenye nyumba ambayo haikuwa 
mali yao. 
“Mah
 a k ama ime s h in dwa kumhusisha mmiliki wa nyumba hiyo, Bw. Michael 
Kijangwa ambaye wakati huo hakuwepo, hivyo mshtakiwa wa kwanza na pili 
mnatiwa hatiani kwa kuhusika kikamilifu katika tukio hili,” alisema. 
Kwa
 upande wake, Mwanasheria wa Serikali, Veridiana Mlenza akiwa na 
mwenzake Sabrina Joshi, waliiomba mahakama hiyo itoe adhabu kali kwa 
washtakiwa kwani matukio ya watu kukutwa na meno hayo yamekuwa 
yakiongezeka. 
“Ni vyema mahakama itoe adhabu kali ili iwe fundisho kwa wengine kutokana na ongezeko la vitendo hivi,” walisema. 
Washtakiwa
 hao walipotakiwa kujitetea, kila mmoja aliiomba mahakama isiwape adhabu
 kali kwani wana familia ambazo zinawategemea. 
Hakimu
 Kashonde alisema kwa mujibu wa Sheria ya Wanyamapori, inatoa fursa kwa 
hakimu kutoza faini mara kumi ya thamani ya nyara inayokamatwa kwa 
mshtakiwa lakini aliwahukumu kifungo hicho iwe fundisho kwa wengine. 
Washtakiwa
 hao wanadaiwa kutenda kosa hilo Januari Mosi 2010, katika Mtaa wa 
Chumbageni, kwenye nyumba inayomilikiwa na Bw. Kijangwa na walikutwa 
wakiwa na vipande hivyo. 
Shtaka
 la pili ambalo lilikuwa likiwakabili washtakiwa hao, inadaiwa Desemba 
31, 2009, huko Chumbageni, walishindwa kutoa taarifa juu ya uwepo wa 
nyara za serikali kwenye nyumba ambayo walikuwa wakifanya kazi. 
Hata
 hivyo, washtakiwa hao walikana na kudai meno hayo hayakuwa ya kwao bali
 ya bosi wao Bw. Kijangwa ambaye kwa wakati huo alikuwa Lushoto na 
familia yake ambako walikwenda kula sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya. 
Inadaiwa
 meno hayo yalipelekwa katika nyumba hiyo iliyopo jirani na Hospitali ya
 Tumaini, eneo la Chumbageni na gari la Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa 
Tanzania (JWTZ) na maofisa wawili Desemba 31, 2009.
No comments:
Post a Comment