TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, December 14, 2013

MIAKA 20 JELA WOTE WALIOKUTWA NA MENO YA TEMBO

Posted: 02 Dec 2013 10:38 PM PST
Watu wawili akiwemo mlinzi wa nyumba moja mkoani Tanga, wamehukumumiwa kifungo cha miaka 20 gerezani kila mmoja baada ya kupatikana na hatia ya kupakua na kuhifadhi meno ya tembo 114 yenye thamani ya sh. milioni 44,044 kinyume cha sheria, anaripoti Mashaka Mhando, Tanga.
Washtakiwa hao ni Bw. Joseph Mwarabu na Bw. Richard Abdallah, ambapo hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Tanga, Mairasaanane Kashonde.
Hakimu Kashonde alisema, washtakiwa walitiwa hatiani chini ya Sheria ya Uhifadhi ya Wanyamapori kifungu cha 86 (i), (ii) C na Kifungu 14 D, cha sheria ya uhujumu uchumi sura 200 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.
Akisoma hukumu hiyo, alisema washtakiwa hao walishiriki kushusha meno hayo kutoka kwenye gari la jeshi na kuyahifadhi kwenye nyumba ambayo haikuwa mali yao.
“Mah a k ama ime s h in dwa kumhusisha mmiliki wa nyumba hiyo, Bw. Michael Kijangwa ambaye wakati huo hakuwepo, hivyo mshtakiwa wa kwanza na pili mnatiwa hatiani kwa kuhusika kikamilifu katika tukio hili,” alisema.
Kwa upande wake, Mwanasheria wa Serikali, Veridiana Mlenza akiwa na mwenzake Sabrina Joshi, waliiomba mahakama hiyo itoe adhabu kali kwa washtakiwa kwani matukio ya watu kukutwa na meno hayo yamekuwa yakiongezeka.
“Ni vyema mahakama itoe adhabu kali ili iwe fundisho kwa wengine kutokana na ongezeko la vitendo hivi,” walisema.
Washtakiwa hao walipotakiwa kujitetea, kila mmoja aliiomba mahakama isiwape adhabu kali kwani wana familia ambazo zinawategemea.
Hakimu Kashonde alisema kwa mujibu wa Sheria ya Wanyamapori, inatoa fursa kwa hakimu kutoza faini mara kumi ya thamani ya nyara inayokamatwa kwa mshtakiwa lakini aliwahukumu kifungo hicho iwe fundisho kwa wengine.
Washtakiwa hao wanadaiwa kutenda kosa hilo Januari Mosi 2010, katika Mtaa wa Chumbageni, kwenye nyumba inayomilikiwa na Bw. Kijangwa na walikutwa wakiwa na vipande hivyo.
Shtaka la pili ambalo lilikuwa likiwakabili washtakiwa hao, inadaiwa Desemba 31, 2009, huko Chumbageni, walishindwa kutoa taarifa juu ya uwepo wa nyara za serikali kwenye nyumba ambayo walikuwa wakifanya kazi.
Hata hivyo, washtakiwa hao walikana na kudai meno hayo hayakuwa ya kwao bali ya bosi wao Bw. Kijangwa ambaye kwa wakati huo alikuwa Lushoto na familia yake ambako walikwenda kula sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya.
Inadaiwa meno hayo yalipelekwa katika nyumba hiyo iliyopo jirani na Hospitali ya Tumaini, eneo la Chumbageni na gari la Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na maofisa wawili Desemba 31, 2009.


No comments:

Post a Comment