TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, December 12, 2013

MAKTABA YA SHULE YA MSINGI MZIMUNI ILIYOKO WILAYANI KINONDONI YAZINDULIWA RASMI NA MAMA SALMA KIKWETE

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwahutubia wanafunzi na walimu wa shule ya Msingi Mzimuni pamoja na wananchi wa eneo hili wakati wa sherehe za uzinduzi wa Maktaba ya shule hiyo tarehe 11.12.2013.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Msingi Mzimuni wakiimba nyimbo za mataifa ya Tanzania na Korea Kusini wakati wa sherehe za uzinduzi wa maktaba katika shule hiyo huko Magomeni katika wilaya ya Kinondoni tarehe 11.12.2013. IMG_0442 
Baadhi ya wazazi wa wanafunzi wanaosoma katika Shule ya Msingi Mzimuni nao wakishiriki katika sherehe ya uzinduzi wa maktaba ya shule hiyo.
Walimu ya Shule ya Msingi ya Mzimuni nao waliungana na wanafunzi wa shule hiyo kusherehekea uzinduzi wa maktaba ya shule uliofanywa na Mama Salma Kikwete tarehe 11.12.2013
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akikata utepe ikiwa ni ishara ya uzinduzi rasmi wa maktaba ya Shule ya Msingi ya Mzimuni iliyoko Magomeni. Kushoto kwa Mama Salma ni Mheshimiwa Balozi Young-Shim Dho, Mwanzilishi wa Step Foundation na Balozi wa Mradi wa Utalii endelevu kwa ajili ya kuondoa umasikini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii Duniani ambaye ndiye aliyefadhili maktaba hiyo. IMG_0535 
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwafuatilia kwa karibu baaqdhi ya wanafunzi wa shule ya Msingi Mzimuni waliokuwa wakitumia maktaba hiyo mara tu baaba ya kuizindua rasmi hapo tarehe 11.12.2013.
IMG_0548 
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwafuatilia kwa karibu baaqdhi ya wanafunzi wa shule ya Msingi Mzimuni waliokuwa wakitumia maktaba hiyo mara tu baaba ya kuizindua rasmi hapo tarehe 11.12.2013.

No comments:

Post a Comment