TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, December 14, 2013

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI

DSC004611
WILAYA YA MBARALI – MAUAJI.
MNAMO TAREHE 1.12.2013 MAJIRA YA SAA 12:00HRS HUKO KATIKA KIJIJI CHA MPAKANI BARABARA KUU YA MBEYA/NJOMBE KATA YA IGAWA TARAFA YA   RUJEWA WILAYA YA MBARALI MKOA WA MBEYA.  MTU MMOJA ASIYEFAHAMIKA JINA WALA MAKAZI YAKE, JINSI YA  KIUME MWENYE UMRI KATI YA  MIAKA 37-40 ALIKUTWA AMEUAWA KWA KUCHOMWA KISU KICHWANI NA SHINGONI NA MTU/WATU WASIOFAHAMIKA KISHA MWILI WAKE KUTUPWA KANDO YA  BARABARA HIYO. CHANZO CHA MAUAJI KINACHUNGUZWA. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA HOSPITALI YA WILAYA YA MBARALI KWA UCHUNGUZI. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA NAIBU KAMISHNA WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA YA MAHALI ALIPO MTU/WATU WALIOHUSIKA NA TUKIO HILI AZITOE KATIKA MAMLAKA HUSIKA ILI WAKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE.
WILAYA YA MOMBA – AJALI YA GARI KUMGONGA MTEMBEA KWA MIGUU NA
                                        KUSABABISHA KIFO.
MNAMO TAREHE 13.12.2013 MAJIRA YA SAA 14:30HRS HUKO MAENEO YA MTAA WA MWAKA   BARABARA YA TUNDUMA/SUMBAWANGA KATA YA TUNDUMA, TARAFA YA TUNDUMA, WILAYA YA MOMBA, MKOA WA MBEYA. GARI T. 904 BXV AINA YA M/CANTER LIKIENDESHWA NA DEREVA MAAMZEE S/O MOHAMED, MIAKA 21, MNYIHA, MKAZI WA MTAA WA MWAKA – TUNDUMA  LILIMGONGA MTEMBEA KWA MIGUU ASIYEFAHAMIKA JINA WALA MAKAZI YAKE, JINSI YA  KIKE, UMRI KATI YA  MIAKA 25-30 NA KUSABABISHA KIFO CHAKE PAPO HAPO. CHANZO CHA AJALI NI MWENDO KASI. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KITUO CHA AFYA TUNDUMA KWA AJILI YA UCHUNGUZI. MTUHUMIWA AMEKAMATWA NA TARATIBU ZA KUMFIKISHA MAHAKAMANI ZINAENDELEA.  KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA NAIBU KAMISHNA WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA MADEREVA KUWA MAKINI WANAPOTUMIA VYOMBO VYA MOTO KWA KUFUATA SHERIA NA ALAMA ZA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUKA AJALI ZINAZOWEZA KUEPUKIKA HASA KATIKA KIPINDI HIKI CHA KUELEKEA MWISHO WA MWAKA.
Signed by:
[DIWANI ATHUMANI – DCP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

No comments:

Post a Comment