TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, March 30, 2016

MWANZA NA ARUSHA YAONGOZA WATUMISHI HEWA.





 Waziri wanchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, George Simbachawene akizungumza na Wakuu wa Mikoa leo jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla akizungumza baada ya kukabidhi majina hewa kwa Waziri wa nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, George Simbachawene leo jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Said Meck Sadik  akikabidhi majina hewa kwa kwa Waziri wa nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, George Simbachawene leo jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam  akizungumza Waziri wanchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, George Simbachawene  baada ya kumkabidhi majina watumishi hewa , jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Mkoa wa Tabora , Aggrey Mwanri akikabidhi majina ya watumishi hewa kwa Waziri wa nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, George Simbachawene leo jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Mkoa wa Lindi ,Godfrey Zambi akikabidhi majina ya watumishi hewa kwa Waziri wa nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, George Simbachawene leo jijini Dar es Salaam.

ASKARI POLISI ANATAFUTWA NA JESHI LA POLISI BAADA YA KUGUNDULIKA ALIJIPATIA AJIRA KWA VYETI VYA KUGUSHI.

Askari wa kikosi cha kuzuia ghasia katika jeshi la Polisi mkaoni Ruvuma F 5425 PC Emmanuel Nyagoli ( 35), anatafutwa na Jeshi hilo kwa kosa la kujipatia ajira kwa vyeti vya Kugushi, Na kwasasa hajulikani alipokimbilia. Taarifa zaidi hii hapa RUVUMA TV.

GSM YASAIDI WATOTO WENYE UGONJWA WA MOYO KATIKA HOSPITALI YA TAIFA YA MHIMBILI.





WATAALAMU WA MOYO KUJADILI JINSI YA KUKABILI, APRILI 21 NA 22 KATIKA UKUMBI WA MWALIMU NYERERE JIJINI DAR.


MPALULEBLOGS: Daktari Bingwa ya moyo katika hospitali ya Mhimbili katika Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete,Tulizo Sanga akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari( hawapo pichani) jijini Dar es Salaam leo.

UGONJWA WA ENDOMETROSIS WAWATESA WANAWAKE.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dk. Hamis Kigwangalla akizungumza na wanafunzi wa sekondari (hawapo pichani) juu ya ugonjwa wa Endometrosis katika semina hiyo kutoa elimu ya ugonjwa iliyoratibiwa na Miss Tanzania 2001, Millen Magese ambaye ni Mhanga wa Ugonjwa huo leo jijini Dar es Salaam.


Mkuruenzi Millen Magese Foundation na Miss Tanzania 2001, Millen Magese akizungumza wakati wa semina ya wanafunzi wa sekondari juu ya ugonjwa wa Endometrosis ambapo yeye ni mhanga wa ugonjwa huo iliyofanyika leo katika shule sekondari Tulian Jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, watoto na Wazee, Dk. Hamis Kigwangalla akiwa katika picha ya pamoja na Miss Tanzania 2001, Millen Magese na wageni walikwa katika semina ya utoaji wa elimu ya ugonjwa wa endometrosis leo jijini Dar es Salaam.


Na:Mwandishi Wetu,
 
IMEELEZWA kuwa kutibu ugonjwa wa Endometrosis ni gharama kubwa na serikali pekee yake haiwezi kushughulikia tatizo hilo.

Ugonjwa huo huwapata wanawake wakati wa hedhi na kufanya mwanake kukosa furaha na kutibu kwake ni gharama kubwa.

Akizungumza na leo katika semina kutoa uelewa kwa wasichana 400 iliyoandaliwa na Taasisi ya Miss Tanzania 2001 Millen Magese, Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamis Kigwangalla amesema kuwa ugonjwa wa Endometrosis unasababisha ugumba kwa wanawake.

Amesema kugundua ugonjwa huo unachukua kati ya miaka sita hadi 10 na kati ya wanawake 100 wenye ugonjwa huo nusu hawawezi kupata watoto.

Dk.Kigwangalla amesema kutambua ugonjwa huo kwa wataalam inachukua miaka saba hadi 10 hivyo kunahitajika elimu hata maeneo vijijini wanawake wanaweza wanaugua lakini hawajui.

“Wahenga wanasema raha ya mwanamke na kuzaa mtoto wake mwenye hivyo kuwa na ugonjwa unafanya mwanamke akose furaha katika maisha yake”amesema Kigwangalla.

Mkurugenzi wa Millen Magese Foundation,Miss Tanzania 20O1, Millen Magese amesema kuwa amefanyiwa operesheni mara 13 na kuamua kutoa elimu juu ya ugonjwa huo.

Amesema kuwa wanawake wengi wanasumbuliwa na ugonjwa huo lakini wanasema ni siri wakati ni ugonjwa wenye maumivu makali..

Tanzania yapokea msaada wa shilingi bilioni 116.4 kutoka Japan.


 Balozi wa Japan nchini Tanzania Bw. Masaharu Yoshida akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) mara baada ya kusaini hati ya makubaliano kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Japan leo jijini Dar es salaam ambao utaiwezesha Tanzania kupata kiasi Yen Bilioni 6 ambazo ni sawa na Sh. Bilioni 116.4 za Kitanzania.(Na Eleuteri Mangi-MAELEZO).
 Na Eleuteri Mangi-MAELEZO









CHUO CHA UTALII KUANZA KUDAHILI WANAFUNZI WAPYA.

JAJI MKUU WA TANZANIA AFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA MAHAKAMA KATIKA MIKOA YA IRINGA, NJOMBE NA RUVUMA, AISIFU MAHAKAMA KANDA YA SONGEA KWA KUFANYA VIZURI.










AIRTEL FURSA YAFIKIA VIJANA WILAYANI NGARA

Profesa Muhongo: Kamilisheni miradi ya umeme vijijini kwa wakati


Na Latifah Boma Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amewataka wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) awamu ya pili kufanya kazi kwa kasi zaidi ili umeme uweze kuwafikia walengwa kabla ya mwezi Juni mwaka huu.Akizungumza na watendaji kutoka kampuni ya CCC International Nigeria Limited, inayosambaza umeme katika mkoa wa Manyara, Profesa Muhongo alisema kuwa hajaridhishwa na kasi ya kampuni hiyo katika utekelezaji wa miradi ya umeme katika wilaya ya Simanjiro ambapo hakuna wateja waliounganishiwa umeme. Pia, Profesa Muhongo amelitaka Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kufanya kazi kwa karibu na wakandarasi hao katika kutatua changamoto zinazowakabili ili waweze kukamilisha miradi hiyo kwa wakati. Aliwataka mameneja wa TANESCO kuongeza juhudi katika kazi zao ikiwa ni pamoja na makusanyo, utatuaji wa changamoto na uunganishaji wa umeme kwa wateja, na kusisitiza kuwa meneja atakayeshindwa kutekeleza majukumu yake ataondolewa katika nafasi yake. Awali, akielezea changamoto katika utekelezaji wa miradi ya umeme meneja mradi kutoka CCC International Nigeria Limited.Zhang Jiangaang, alieleza kuwa wamekuwa wakiibiwa vifaa vyao vya kazi kutokana na kuwepo kwa usalama mdogo hivyo kupelekea kutokamilisha mradi kwa wakati kutokana na hasara wanayoipata. 

WADAU WA SEKTA YA USAFIRI WA ANGA WAKUTANA KUJADILI MPANGO KAMAMBE WA USAFIRI WA ANGA ( CIVIL AVITIATION MASTER PLAN) JIJINI DAR ES SALAAM LEO



Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dkt Leonard Chamuriho akifungua warsha ya kujadili rasimu ya Mpango Kamambe wa Sekta ya Usafiri wa Anga( The Civil Aviation master Plan) iliyofanyika makao makuu ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania(TCAA). Banana - Ukonga jijini Dar es Salaam leo. 

Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dkt Leonard Chamuriho(katikati) Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Hamza Johari(Kulia) na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Mhandisi George Sambali (kushoto) wakiwa kwenye warsha ya kujadili rasimu ya Mpango Kamambe Sekta ya Usafiri wa Anga( The Civil Aviation master Plan) warsha hiyo ilifanyika katika ofisi za Makao makuu ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania(TCAA) ), Banana - Ukonga jijini Dar es Salaam leo.

Baadhi ya wadau mbali mbali wa sekta ya usafiri wa anga wakishiriki warsha ya kujadili rasimu ya Mpango wa Sekta ya Usafiri wa Anga( The Civil Aviation master Plan) uliofanyika makao makuu ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania(TCAA), Banana - Ukonga jijini Dar es Salaam leo.

WANAWAKE DODOMA WANUFAIKA NA ELIMU YA UJASILIAMALI INAYOTOLEWA NA MANJANO FOUNDATION

Ziara ya Mafuzo ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa

 Leo Jumatano tarehe 30 Machi 2016 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa chini ya Makamu Mwenyekiti Mh. Dkt. Pudenciana Kikwembe walipata fursa ya kutembelea ofisi za MKURABITA kwa ajili ya kujifunza juu ya madhumuni na shughuli za MKURABITA nchini.

Prof. Mbarawa afanya ziara kushtukiza KOJ Kurasini

 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akiongea na baadhi ya wafanyakazi wa TPA eneo la kupakulia mafuta yanayoingia nchini (KOJ) Kurasini leo jijini Dar es salaam. Wa kwanza kulia Mhandisi anayefanya kazi eneo la KOJ Jabiri Muyones.
 Kapteni Abdulla Mwingamno (kulia) akimuonesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (kushoto) baadhi ya vifaa vya kituo cha kupakulia mafuta yanayoingia nchini (KOJ) Kurasini leo jijini Dar es salaam.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akiongozana na Mhandisi anayefanya kazi eneo la KOJ Jabiri Muyones alipotembelea TPA eneo la kupakulia mafuta yanayoingia nchini (KOJ) Kurasini leo jijini Dar es salaam.

China yaonesha nia ya kuwekeza kwenye sekta ya nishati