TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, June 18, 2016

MADRASA RAHMAN GREASE MWISHO IMEFIWA NA MWANAFUNZI BI.SALAMA JUMA NYAMBI

RC WA MWANZA MHE JOHN MONGELLA APOKEA GARI LA WAGONJWA




DAWA ZA MILIONI 294 ZILIZOKAMATWA KATIKA OPERESHENI ZAKABIDHIWA KWA MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM.








KAMPUNI YA TING YATOA MAGETI YA CHUMA KUDHIBITI WEZI WA KOKI ZA MAJI UWANJA WA TAIFA



==========================================

KAMATI YA MPITO – TZUK YAKAMILISHA RASIMU YA KATIBA, KUUNDA SHIRIKISHO LA JUMUIYA NCHINI UINGEREZA, RASIMU TAYARI IMEIVA KWA KUIDHINISHWA NA MKUTANO MKUU WA WATANZANIA WOTE WANAOISHI NCHINI UINGEREZA (UK & NI)








Natanguliza shukurani, 
wenu katika ujenzi wa Jumuiya;
Abraham Sangiwa


Hospitali ya Amana yaboresha huduma zake

Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO

Hospitali ya Rufaa ya Amana Jijini Dar es Salaam imeboresha huduma za afya kwa kuweka mashine maalumu ya kutibu meno ijulikanayo kama (Ceramic dental machine) lengo ikiwa ni kuboresha huduma hizo katika hospitali za umma.

Akiongea katika mahojiano kwa njia ya simu Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo Bw.Meshack Simwela ameeleza kuwa kwa sasa wataweza pia kutoa huduma ya afya kwa viongozi wa serikali pamoja na wabunge kupitia wodi maalum iliyotengwa kwa ajili yao ili kupata huduma hiyo wanapokuwa jijini hapa.

"Tunaishukuru sana Serikali yetu kwa kutuletea mashine hii maalumu kwa ajili ya magonjwa yote ya meno na tunaishkuru pia kwa kutushauri kutenga wodi maalumu kwa ajili ya kuwatibia viongozi mbalimbali wakati wakiwa hapa Dar es Salaam,ushauri huo tumeupokea na tumeufanyia kazi", alisema Simwela.

Aliongeza kuwa maboresho hayo yatasaidia wananchi kupata huduma bora za afya na kupunguza gharama za matibabu na kuondoa usumbufu wa kwenda kutafuta huduma hiyo katika hospitali binafsi.

Bw. Simwela anabainisha kuwa mashine hiyo ilikuwa ikipatikana katika Hospitali chache za binafsi na matibabu yake huchukua muda mwingi na gharama kubwa jambo ambalo lilikuwa likiwaumiza wananchi wenye kipato cha chini, hivyo upatikanaji wa huduma hiyo imekuwa msaada mkubwa sana.

Vilevile aliongeza kwa kutolea ufafanuzi suala la huduma ya wodi maalumu itakayokuwa ikitoa huduma za afya kwa viongozi na wabunge tayari imeshaanza kufanya kazi tangu mwezi Machi mwaka huu ikiwa na vyumba viwili vya wagonjwa mahututi (ICU) pamoja na vyumba 24 ambavyo vina sehemu ya kukaa, kulala pamoja na choo.

Aidha, amefafanua kuwa matibabu katika wodi hiyo yanaweza kulipiwa kwa bima ya afya au kwa fedha taslimu pia ameongeza kuwa wodi hizo hazijatengwa kwa ajili ya viongozi pekee bali zinaweza kutumika pia kwa wananchi wa kawaida watakaoweza kulipia gharama za matibabu zilizopangwa katika wodi hiyo.

Naye Afisa Habari wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, David Langa amesema kuwa kufunguliwa kwa wodi hiyo kumesaidia sana waganga kuwepo katika vituo vyao vya kazi muda wote kwasababu huduma za afya kwenye wodi hiyo ni masaa 24 pia mganga anapomtibu mgonjwa anapatiwa asilimia 30 ya gharama za matibabu yale papo hapo,fedha hizo ni nje ya mshahara wa mwisho wa mwezi.

Ametoa rai kwa Serikali kuongeza mashine hizo maalumu kwa ajili ya magonjwa ya meno na kuziweka katika Hospitali mbalimbali ili kupunguza mlundikano wa wagonjwa wengi katika Hospitali moja.
==================================================

MERCY KITOMARI, MJASIRIAMALI KIJANA ANAYETAKA KUMUONA ‘ROLE MODEL’ WAKE RAIS MAGUFULI


Mjasiriamali kijana na mmiliki wa Nelwa’s Gelato, Mercy Kitomari wakati akizungumza na Meneja Uendeshaji wa mtandao wa Habari wa Modewjiblog, Zainul Mzige (hayupo pichani).

MJASIRIAMALI kijana na mmiliki wa Nelwa’s Gelato, Mercy Kitomari amesema anatamani kukutana na Rais John Pombe Magufuli kumwelezea haja ya kukutana na wanawake wajasiriamali vijana wamweleze matatizo yao.

Amesema Rais baada ya kukutana na makundi mbalimbali ya wafanyabiashara , inafaa akutane na wajasiriamali wanawake vijana ambao wanapita katika magumu mbalimbali .

Alisema katika mahojiano hivi karibuni ambayo sehemu yake itachapishwa katika mtandao wa Modewjiblog muda wowote kwamba, rais Magufuli akiwa kama ‘Role Model wake’ katika kujituma, anaweza kuwasikiliza wanawake hao vijana na kusaidia kuwasukuma juu zaidi katika kampeni ya kuiweka Tanzania kuwa nchi ya viwanda.

“Nimekuwa nikikutana na wanawake wenzangu ambao wamekata tamaa na wamekuwa wakiniuliza ninawezaje kuendelea, nikawambia wasi-give up (wasikate tama) na kwamba serikali hii ni ya viwanda na kuchapa kazi “ alisema na kufafanua kwamba wanachohitaji wanawake hao ni mazingira mazuri ya kufanya ujasiriamali.

Mercy ambaye anatengeneza ‘ice cream’ zinazotumia matunda yote ya kitanzania kama vile fenesi, nanasi, bungo, ndizi, embe ana ndoto ya kumiliki kiwanda kikubwa kinachoweza kutengeneza na kufikisha ashkrimu kwa Tanzania na Afrika Mashariki ifikapo mwaka 2020.

Akiwa ameanza kazi hiyo mwaka 2010 kutoka ‘jiko’ la nyumbani Mercy amefanikiwa kutambua wigo wake wa biashara ambayo amesema ina changamoto nyingi hasa mifumo ya vibali na ulipaji kodi na ushuru.
Muonekano wa nje wa duka la Ice Cream la Nelwa’s Gelato lililopo ndani ya Petrol Station ya SOPCO barabara ya Morogoro-Magomeni Mwembechai karibu na kwa Sheikh Yahya.

Alisema uwapo wa kodi nyingi zenye viwango sawa kati ya anayeanza na aliyekuwepo; anayeingiza kidogo na kikubwa kunaleta athari kubwa kwa wajasiriamali wanaotaka kuchomoza.

“To be honest (nikiwa mkweli) zinavunja moyo… nyingi zinakwamisha kwani sisi waelewe tu kwamba tunatengeneza ajira na tunatengeneza soko kama mimi nanunua matunda natengeneza soko la mkulima.,.. natengeneza ashkrimu (Ice Cream) natengeneza ajira.. ipo haja ya kuangalia mambo mengi na hasa hili la kodi na ushuru” alisema.

Alisema ana mambo mengi ya kumwambia Rais Magufuli kama mjasiriamali mwanamke kijana.

“Atupe nafasi tukutane naye wanawake wajasiriamali vijana kisha tutamweleza mengi yakiwemo ya kodi na mifumo yake, mimi ningemweleza haja ya vyombo vyote vya huduma kutumia mtandao, kutoa huduma ,ningemweleza haja ya halmashauri na taasisi kutoa mafunzo mbalimbali ili kuinua wajasiriamali hawa na kuwasapoti si tu kuchukua kodi na ushuru” anasema Mercy.

Anasema wajasiriamali wengi wadogo hawaendelei kwa kukosa sapoti ya mafunzo na namna ya kufanya biashara zao zikue.

“Wasiwe wanachukua kodi na ushuru tu, halmashauri hizi lazima zianze kufikiria kukuza wajasiriamali kwa kuwapa elimu inayostahili katika biashara zao” anasisisitiza Mercy ambaye amesema angelipenda kumuona Role Model wake (Rais Magufuli) kumweleza mengi yanayohusu wanawake vijana na viwanda vidogo kuelekea viwanda vikubwa na hamu ya wajasiriamali wanawake vijana kuchangia pato la taifa na kulipa heshima.

Anasema anapokutana na wajasiriamali wa Uganda, Rwanda anaona jinsi serikali zao zinavyowasaidia kunyanyuka na anaona serikali ya awamu ya tano inaweza kuwasikia na wao wakanyanyuka. 
==================================================

==============================================

KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI AFUNGA MAFUNZO JIJINI TANGA

===================================================

Waziri Nape akutana na Wakuu wa Vitengo vya Mawasiliano Serikalini katika kuadhimisha wiki ya utumishi wa Umma



======================================================

MATUKIO MBALIMBALI YA MKUTANO WA BUNGE LA BAJETI LEO TAREHE 17 JUNI, 2016 MJINI DODOMA

Thursday, June 16, 2016

RAIS DKT MAGUFULI AKUTANA NA BALOZI WA QATAR NCHINI NA SPIKA MSTAAFU MHE ANNE MAKINDA IKULU DAR ES SALAAM LEO

MAKONDA AKANDIA SIMU FEKI ZIZIMWE KWANI SI SALAMA KWA MATUMIZI YA BINADAMU.

WATOTO WALIZALIWA LEO WASHEREKEA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA KWA KUZAWADIWA ZAWADI NA WAFANYAKAZI WA BENKI YA CRDB TAWI LA MLIMANI CITY JIJINI DAR LEO.