TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, April 28, 2016

DC HAPI ATEMBELEA WANANCHI BUNJU, MBWENI WALIOKUMBWA NA MAFURIKO



Akipokea maelezo ya Mwenyekiti wa serikali ya mtaa na baadae kuzungumza na wananchi wa eneo hilo, mkuu wa wilaya aliambiwa na baadhi ya wakazi wa asili wa eneo hilo kuwa sehemu hiyo ilikua ni bwawa la maji miaka yote.
Wakazi hao ambao nyumba zao zimezungukwa na maji walimuomba Mkuu wa wilaya kusaidiwa pampu kubwa ili maji hayo yavutwe na kupelekwa kwenye mitaro upande wa pili wa barabara.

Akijibu maombi hayo Mh. Hapi aliwaagiza mainjinia wa manispaa kuhakikisha kuwa wanafanya utaratibu wa kupata pampu kubwa ya kuvuta maji hayo. Aidha, Mkuu huyo wa wilaya ya Kinondoni aliwaambia wananchi kuwa wale wote waliojenga  katika eneo hilo ambalo ramani inaonesha kuwa ni eneo la wazi wajiandae kuondoka.
"Serikali itawasaidia kutoa haya maji kama hatua ya dharura. Lakini suluhu ya kudumu ni kuwa waliojenga hapa wote wamejenga eneo la wazi tena ni bwawa. Hivyo lazima wajiandae kuhama.
Serikali kazi yake ni kuwaambia wananchi ukweli, hata kama ukweli huo utakua na maumivu. Hivyo ukweli wa jambo hili ni kuwa waliojenga hapa wahame."
Akitoa rai kwa viongozi wa serikali ya mtaa ambao wameshiriki katika kuuza eneo hilo kinyume na taratibu mh. Mkuu wa Wilaya aliagiza na kusema
" kila Mwananchi aliyejenga hapa aende ofisi ya mtaa kujisajili akiwa na vielelezo vyote vya kumiliki eneo hili na alikonunua. Kisha nipewe taarifa na uhakiki utafanyika. Kama kuna viongozi wa serikali ya mtaa walishiriki kuuzia watu viwanja hapa kinyume na ramani ambayo wao wana nakala yao basi wajiandae kuwajibishwa."
Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya alitembelea eneo la Mbweni ambako Mwananchi asiyefahamika amejenga ukuta kuzunguka eneo la wazi. Hapi alifika eneo hilo na kujionea ukuta huo kisha akaagiza mtendaji wa mtaa pamoja na anayejenga ukuta huo kufika ofisini kwake kesho Ijumaa mchana wakiwa na vielelezo vyote na vibali vya ujenzi kama wanavyo.
Ziara ya mkuu wa wilaya inaendelea muda huu katika maeneo ya barabara za Sinza ambazo wakandarasi walipewa kujenga.

GSM FOUNDATION NA MOI WAANZA KAMBI ZA UPASUAJI BUGANDO.





Serikali kuwachukulia hatua kali za kisheria wananchi waliobadili matumizi ya Ardhi ya makazi na kuyageuza kuwa maeneo ya biashara


MAJALIWA AKUTANA NA MKURUGENZI MKUU WA NSSF.


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF).

RAIS DKT MAGUFULI ATENGUA UTEUZI WA MKURUGENZI MTENDAJI WA TIC

WAZIRI NAPE APANIA KUIBORESHA TASNIA YA HABARI





JE WAJUA? SIO KILA HOMA NI MALARIA, NENDA UKAPIME




WADAU WA KAMPENI YA OKOA TEMBO WA TANZANIA WAMWANGUKIA RAIS MAGUFULI.












-MWANZILISHI WA TAASISI YA MAN AT WORK YAKUTANA NA WADAU WAKE JIJINI ARUSHA










MKAKATI WA UTOZAJI WA FAINI KWA WAMILIKI WA ARDHI.

BOSTON CITY CAMPUS TANZANIA, BRANCH NOW OPEN

Boston City Campus and Business College carries a legacy of over 20 years in South Africa. It currently has 44 branches with over 25000 students studying every year. In Tanzania, Boston has opened its first branch outside South Africa, 45th Branchin total this year.




MATUKIO BUNGENI LEO.

MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI MSAAFU AZINDUA RIPOTI YA MPANGO WA UHAMASISHAJI UWAZI KATIKA MAPATO YA MADINI, GESI ASILIA NA MAFUTA (TEITI)

MONGELLA AZINDUA MRADI WA UZINDUZI WA MRADI WA UIMARISHAJI WA MIFUMO YA SEKTA ZA UMMA KATIKA MKOA WA MWANZA

Wanafunzi International School of Tanganyika watembelea UN Tanzania

WAKAZI 267 WA MKOANI NJOMBE WANUFAIKA NA HUDUMA ZA MADAKTARI BINGWA

Na Jacquiline Mrisho-MAELEZO-Dar es salaam

Jumla ya wagonjwa 267 wa mkoani Njombe wamenufaika na huduma za matibabu za madaktari bingwa kutoka hospitali mbalimbali za hapa nchini.

Takwimu hizo zimetolewa leo mkoani Njombe na Afisa Mawasiliano Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Luhende Singu wakati akitoa taarifa za maendeleo ya zoezi la utoaji wa huduma za afya kwa wananchi chini ya ufadhili wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.

Amesema kuwa kati ya wagonjwa hao, 13 wamepatiwa huduma ya upasuaji kutoka kwa madaktari bingwa pia huduma hizo zinaendelea kutolewa katika Hospitali ya Kibena mkoani humo.

"Tunawashukuru sana wananchi wa Mkoa wa Njombe kwa kuitikia wito wetu, leo ni siku ya tatu lakini tumeshawapatia matibabu jumla ya wananchi 267 kati ya hao wagonjwa 13 wamepatiwa huduma ya upasuaji, tunawasihi waendelee kuja kwakua bado tuna siku mbili za kuendelea kuwapatia huduma za afya"alisema Singu.

Amefafanua kuwa asilimia kubwa ya wagonjwa waliopatiwa matibabu mkoani hapo ni wanawake ambao wengi wao wanasumbuliwa na magonjwa ya moyo pamoja na mfumo wa mkojo.

Lengo wa mpango huu wa kutumia madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Hospitali za Rufaa za Kanda ni kuhakikisha kuwa huduma za matibabu kutoka kwa madaktari bingwa zinawafikia wanachama wa Mfuko huo na Watanzania kwa ujumla popote walipo.

Mpaka sasa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya umepeleka huduma ya madaktari bingwa katika Mikoa 14 ikiwa na lengo la kuhakikisha huduma bora za matibabu zinatolewa kwa usawa.Singu ametoa wito kwa wananchi wa mkoani Njombe kuendelea kujitokeza kwa wingi kujipatia matibabu kwa kuwa huduma hizo zinatolewa kwa gharama nafuu.

MKUU WA WILAYA YA MOSHI ,NOVATUS MAKUNGA AAJIONEA ATHARI YA MAFURIKO .

BAADHI YA VICHWA VYA MAGAZETI YA LEO APRIL 28

MJANE WA BABA WA TAIFA, MAMA MARIA ATEMBELEA DARAJA LA NYERERE KIGAMBONI LEO

SERIKALI YAZUIA UINGIZAJI HOLELA WA MCHELE











BAJETI YA OFISI YA WAZIRI MKUU YAPITISHWA NA BUNGE MJINI DODOMA

BANDARI YA DAR KUUNGANISHA SINGAPORE NA EAC’‘BANDARI YA DAR KUUNGANISHA SINGAPORE NA EAC

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Biashara na Viwanda wa Singapore, Dkt. Koh Poh Koon (kulia kwake) na ujumbe wake, Ofisini kwake bungeni mjini Dodoma Aprili 27, 2016. Kulia ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WANDISHI ZANZIBAR WAPEWA SEMINA JUU YA GONJWA LA KIPINDUPINDU

PROF.MUHONGO ASAINI KIBALI CHA KUHAMISHA LESENI YA MADIN

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA NCHINI AFUNGA RASMI MAFUNZO YA MAAFISA WATEULE DARAJA LA KWANZA , MKOANI MOROGORO

WANAMUZIKI NA WADAU WA MUZIKI KUKUTANA NA MKUU WA MKOA DSM ALHAMISI HII

WAKAZI 267 WA MKOANI NJOMBE WANUFAIKA NA HUDUMA ZA MADAKTARI BINGWA

 

Jumla ya wagonjwa 267 wa mkoani Njombe wamenufaika na huduma za matibabu za madaktari bingwa kutoka hospitali mbalimbali za hapa nchini.
Takwimu hizo zimetolewa leo mkoani Njombe na Afisa Mawasiliano Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Luhende Singu wakati akitoa taarifa za maendeleo ya zoezi la utoaji wa huduma za afya kwa wananchi chini ya ufadhili wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.
Amesema kuwa kati ya wagonjwa hao, 13 wamepatiwa huduma ya upasuaji kutoka kwa madaktari bingwa pia huduma hizo zinaendelea kutolewa katika Hospitali ya Kibena mkoani humo.
“Tunawashukuru sana wananchi wa Mkoa wa Njombe kwa kuitikia wito wetu, leo ni siku ya tatu lakini tumeshawapatia matibabu jumla ya wananchi 267 kati ya hao wagonjwa 13 wamepatiwa huduma ya upasuaji, tunawasihi waendelee kuja kwakua bado tuna siku mbili za kuendelea kuwapatia huduma za afya”alisema Singu.
Amefafanua kuwa asilimia kubwa ya wagonjwa waliopatiwa matibabu mkoani hapo ni wanawake ambao wengi wao wanasumbuliwa na magonjwa ya moyo pamoja na mfumo wa mkojo.
Lengo wa mpango huu wa kutumia madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Hospitali za Rufaa za Kanda ni kuhakikisha kuwa huduma za matibabu kutoka kwa madaktari bingwa zinawafikia wanachama wa Mfuko huo na Watanzania kwa ujumla popote walipo.
Mpaka sasa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya umepeleka huduma ya madaktari bingwa katika Mikoa 14 ikiwa na lengo la kuhakikisha huduma bora za matibabu zinatolewa kwa usawa.
Singu ametoa wito kwa wananchi wa mkoani Njombe kuendelea kujitokeza kwa wingi kujipatia matibabu kwa kuwa huduma hizo zinatolewa kwa gharama nafuu.

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AKUTANA NA UONGOZI WA BARAZA LA TAWLA NA UONGOZI WA SKAUT .

Waajiri Wote Wanaodaiwa Malimbikizo Ya Michango Ya NSSF watakiwa Kulipa Michango Kabla Ya Tarehe 30.06.2016

GHARAMA ZA UENDESHAJI BAKHRESA KUPUNGUZWA NA KAMPUNI YA “GE POWER”