TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, April 24, 2016

WAZIRI MKUU ALITAKA TAMASHA LA KRISMASI, PASAKA MIKOA YA KUSINI


WAZIRI MKUU wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa, amemuomba Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka Alex Msama, kupeleka huduma hiyo katika mikoa ya Kusini kwa sababu wanakosa huduma ya neno la Mungu.

Kampuni ya Msama huandaa Tamasha la Krismasi linalotarajia kufanyika Desemba mwaka huu na Pasaka linalotarajia kufanyika mwakani hapa nchini.

Majaliwa alisema kwa sasa tamasha hilo limekuwa na nguvu kubwa ya kuhakikisha inahamasisha jamii katika mambo mbalimbali hivyo ni wakati wa mikoa ya kusini kufaidika.

Alisema kuwa serikali yake imejipanga kuhakikisha kuwa kila Mtanzania ana haki ya kuona serikali yake inawajali na kuwapenda hivyo taasisi kama Msama Promotions, sasa inahitaji kujitanua na kufika mikoa mingi ya Tanzania.

Waziri Mkuu alisema kuwa amekuwa akifuatilia namna Tamasha la Pasaka linavyojitahidi katika kuelimisha na kupiga vita unyanyasaji wa kijinsia hasa wajane na yatima hivyo na mikoa kama Lindi na Mtwara nayo inahitaji huduma hiyo.

“Nimefarijika sana na namna kampuni ya Msama Promotions chini ya Mkurugenzi wake, Alex Msama namna inavyofanyakazi zake katika kutoa burudani na kuelimisha jamii kwa maana hivyo ningependa kuwaunga mkono katika hilo,” alisema Majaliwa.

Alisema mikoa mingi ikiwamo Lindi na Mtwara nayo inachangamoto nyingi hivyo wanahitaji ujumbe kama unatolewa katika Tamasha la Pasaka kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa.

“Kutoa misaada kwa yatima sio kitu kidogo lakini kubwa ni namna kampuni ya Msama Promotions chini ya Mkurugenzi wake Alex Msama, inavyofanyakazi zake kwa kufuata sheria katika hili nawapongeza lakini kubwa ni kukumbuka mikoa ya Kusini nayo inahitaji huduma hiyo.

Alisema kuwa kuna waimbaji wengi wakubwa ambao kwa sasa wamekuwa wakifanya kazi kwa ushirikiano na Msama lakini bado hawajawahi kufika katika mikoa ya kusini hivyo ni wakati wake kuhakikisha nao wananufaika na tamasha hilo.

Majaliwa amemtaka Msama kuendelea na huduma hiyo kwani serikali iko tayari kutoa msaada wa hali na mali.

Aidha Mkurugenzi wa Msama Promotions Alex Msama amemshukuru Waziri Mkuu Majaliwa na kusema kuwa atajitahidi kuboresha na kuhakikisha wananchi wote wa Tanzania wananufaika na huduma hiyo.

Msama amesema kuwa amesikia kilio cha Waziri Mkuu nakusema kuwa kamati yake iko makini na inajipanga kuhakikisha ombi hilo linafanyiwa kazi.

No comments:

Post a Comment