TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, April 27, 2016

RAIS DKT. MAGUFULI AWAAPISHA MAKATIBU TAWALA WAPYA WA MIKOA 10 IKULU JIJINI DAR ES SALAAM



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewaapisha Makatibu Tawala wapya kumi aliowateua tarehe 25 Aprili, 2016 na kuwapangia vituo vyao vya kazi.
Makatibu Tawala hao wameapishwa leo tarehe 27 Aprili, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam na kisha wametia saini hati ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma, zoezi lililoendeshwa na Kamishna wa maadili Sekreatieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Mheshimiwa Jaji Salome Kaganda na kushuhudiwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.
Makatibu Tawala walioapishwa ni;
1. Arusha - Richard Kwitega
2. Geita - Selestine Muhochi Gesimba
3. Kagera - Armatus C. Msole
4. Kilimanjaro - Eng. Aisha Amour
5. Pwani - Zuberi Mhina Samataba
6. Shinyanga - Albert Gabriel Msovela
7. Singida - Dr. Angelina Mageni Lutambi
8. Simiyu - Jumanne Abdallah Sagini
9. Tabora - Dkt. Thea Medard Ntara
10. Tanga - Eng. Zena Said
Makatibu Tawala wengine wa Mikoa ambao hawakuapishwa leo, ni wale waliohamishwa vituo vya kazi na wale waliobaki katika vituo vya kazi walivyokuwep,o ambao tayari walishakula kiapo cha kuwa Katibu Tawala wa Mkoa.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
27 Aprili, 2016

No comments:

Post a Comment