TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, January 24, 2014

Rose Ndauka AKANUSHA MAHUSIANO YAKE NA TUNDA MAN


MSANII wa filamu nchini Rose Ndauka ashangazwa na kauli ya msanii wa muziki wa bongo Fleva Tunda Man ya kujitangazia kuwa alishawahi kuwa naye  katika mahusiano na kuwa ni mwanamke wa kwanza kuwa naye.
Mshangao huo umeibuka mara baada ya TundaMan kueleza kuwa, alishawahi kujihusisha kwenye mahusiano ya kimapenzi na msanii huyo mnamo mwaka 2006.
Tundaman alisema hayo kwenye mahojiano yaliyofanyika katika kipindi cha XXL kinachorushwa na Clouds Fm, ambapo aliweka wazi kuwa alishawahi kuwa na mahusiano na mwanadada huyo wakati wote wawili wakiwa bado hawajapata majina kwenye fani zao.
Aliendelea kueleza kuwa walikuwa wakikutana na Ndauka katika studio iliyokuwepo maeneo ya Kariakoo ambapo ndipo walipoanza mahusiano yao ya kimapenzi.
Akizungumza na jarida hili msanii huyo wa kike Rose Ndauka, ambaye sasa ni mama wa mtoto mmoja wa kike, alisema kuwa amechukizwa na habari hizo kwani hakuzitarajia kwa kipindi hiki ambapo yupo katika ulezi wa mtoto wake.
Kutokana na maneno hayo Ndauka aliweka wazi na kusema kuwa Tundaman anatafuta ugomvi kutokana na kauli yake aliyoiongea na kudai kuwa kwa nini asiongee habari hiyo tangu mwanzo kama inaukweli wowote.
"Alichoongea akina ukweli wowote na ninamshangaa kwa nini atoe kauli hiyo kwa kipindi hichi kama kuna ukweli alikuwa wapi kutotoa ukweli huo hapo mwanzo, ameniudhi sana sitaki maneno maneno na mtu yeyote yule" alisema Ndauka.
Aliongezea kuwa anatafuta kuanza kusomwa kwenye magazeti kwa  kuanza kuongea vitu ambavyo havina ukweli kwa lengo la kutaka kuchafuana

DIAMOND KUPUNGUZA UKIMWI GYM-BAADA YA KUWASILI JIJINI NAIROBI KENYA















New Mexico teen accused of gunning down family 'lost sense of conscience'

Police: Girl, 14, stabs sister 40 times because she felt unappreciated

By Lateef Mungin, CNN
Watch this video

Town in shock, disbelief

STORY HIGHLIGHTS
  • The 14-year-old called 911, police said
  • Officers found her sister upstairs stabbed 40 times
  • Neighbors say the sisters seemed close and played together
  • The 14-year-old is in a juvenile detention center
(CNN) -- An 11-year-old Illinois girl was stabbed 40 times by her 14-year-old sister, police say, and the reason why has many in the small Chicago-area community of Mundelein reeling in disbelief.
Police found the 11-year-old girl unconscious and in need of medical attention in an upstairs bedroom of the dwelling Tuesday morning. She later died.
Because the sister, who called police, initially told officers an intruder was to blame for the attack, authorities briefly placed three schools on lockdown.
The truth, when it emerged, was even more shocking.
Police: Teen killed younger sister
The 14-year-old, authorities say, repeatedly and fatally stabbed the victim -- her half sister -- with a kitchen knife because the teen thought she was ungrateful.
"This incident is a heartbreaking tragedy that defies understanding," said Mundelein Mayor Steve Lentz. "I am asking the Chicagoland area, please pray for us. Pray, first of all, for the family that has been devastated by this."
A group called "Mundelein Moms" is raising money for the girl's funeral and said it raised $6,381 in just one day. There also is an effort to have residents leave their lights on Friday night in remembrance.
Intruder in the house
Police received a 911 call about the incident at 8:30 a.m Tuesday. The call came from the 14-year-old girl, said Mundelein Police Chief Eric Guenther.
The teen told emergency dispatchers that an intruder had barged into the home, attacked her sister and then fled, CNN affiliate WLS reported.
Schools in area were immediately placed on lockdown, Guenther said.
"The area-wide school lockdown lasted only 15 minutes," he said.
But the teen's story unraveled quickly. Under police questioning, she admitted to the attack, authorities said.
Feeling unappreciated
The teen told police she was mad that her sister didn't appreciate all she did for her, prosecutors said at the suspect's detention hearing Wednesday. WLS was at the hearing.
The teen said she cooked dinner for her younger sibling and performed other chores. She was also angry that the 11-year-old girl had recently hit her.
The night before the attack, the teen thought about it for about 10 or 15 minutes, then went downstairs and grabbed a knife, according to prosecutors.
After the stabbing, she took a shower to wash off the blood, called police and made up the story about the intruder, prosecutors said.
The 14-year-old was arrested and was charged with murder.
The case is in juvenile court and a decision could be made in the future to move the case to adult court, the Lake County State Attorney's Office said.
Playing together
Those who knew the girls said they lived at the home with their mother. Neighbors said the siblings seemed close.
The girls were often seen playing together and practicing cheerleading routines, WLS reported.
"They would always be together," Mary Ann Gryder, a neighbor told the affiliate.
"The older one would be taking care of the younger one, and vice versa."

UCHAGUZI WA UDIWANI SOMBETINI ARUSHA MOTO MOTO

UCHAGUZI mdogo wa udiwani Kata ya Sombetini umeanza kwa vurugu baada ya wanachama watatu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kujeruhiwa na kundi la vijana walinzi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Green Guard.
Aidha, mgombea wa CCM kwenye kata hiyo, David Lesikari, akiwa na watu wengine  anadaiwa kuwashambulia na kitu chenye ncha kali wanachama wawili wa CHADEMA na kumjeruhi mwingine kichwani na mgongoni.
Mwenyekiti wa CHADEMA wilayani Arusha, Ephata Nanyaro, aliwaeleza waandishi wa habari jana kuwa vurugu hizo zilitokea Januari 20 mwaka huu na kwamba licha ya wanachama wao kuumizwa, Jeshi la Polisi liliwakamata na kuwageuzia kesi kuwa wao ndio waliofanya vurugu.
Alisema siku hiyo saa nane mchana mwanachama wao, Vitalis Bernad, alipigwa shoka la kichwa na kijana aliyedai kuwa kiongozi wa CCM wakati akipita kwenye kona ya Mbauda akiwa kwenye pikipiki yenye bendera ya CHADEMA wakielekea kwenye mkutano wa mgombea wa chama chao, Ally Bananga.
“Kwa bahati Bernard alikuwa amevaa kofia ngumu za waendesha pikipiki hivyo hakuumia sana lakini watu waliokuwa pale walijaribu kumkimbiza mhusika lakini hawakufanikiwa, kwani alikimbilia kwenye ofisi ya CCM ambapo walitokea kundi la watu wenye mapanga kutoka ndani ya ofisi hizo jambo lililowafanya wananchi kutawanyika kwa hofu,” alisema Nanyaro.
Alisema Bernard akiwa na viongozi wa CHADEMA walienda polisi kufungua taarifa namba Ar/RB/982/2014 kwenye kituo kidogo cha Mbauda karibu na ofisi hizo za CCM ambapo waliwaeleza polisi kuwa mtuhumiwa yuko ndani ya ofisi hizo lakini hawakutaka kwenda kumkamata.
Mwenyekiti huyo wa wilaya alisema siku hiyo hiyo saa 12 jioni Wanachadema wawili, Loserian Laisi na Mozec Joseph wakitokea kwenye mkutano wa kampeni wakiwa wamepakizana kwenye pikipiki walivamiwa na kundi la watu wakiongozwa na mgombea wa CCM ambapo waliwashambulia kwa mapanga na silaha za jadi.
Nanyaro alisema katika tukio hilo Loserian alikatwa kichwani na kiunoni kwa kitu chenye ncha kisha kutelekezwa migombani kabla ya kusaidiwa na wasamaria wema waliompeleka Kituo cha Polisi cha Sombetini kupata fomu ya matibabu (PF3) na kwenda hospitali.
“Polisi bila weledi walichukua maelezo kwa saa mbili huku Loserian akiwa kwenye maumivu na damu zikimtoka hata hivyo alipatiwa matibabu katika hospitali ya Kaloleni, akiwa anaendelea na matibabu polisi walifika hospitalini na kumchukua hadi Kituo Kikuu cha Polisi na kumweka rumande,” alilalamika Mwenyekiti huyo wa CHADEMA.
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, alikiri ofisi yake kupokea taarifa za vurugu za jioni huku akibainisha kwamba taarifa za tukio la mchana hakuzipata.
Akizungumza na Tanzania Daima, Kamanda Sabas alisema kwenye tukio hilo la jioni vijana wa CHADEMA wakiwa kwenye pikipiki mmoja alishuka na kumpiga vibao mgombea wa CCM, Lesikari, ambapo wananchi walioona walipandwa na hasira hivyo kuwashambulia na kukiri kwamba vijana wa CHADEMA kuhojiwa na polisi kuhusu tukio hilo.
“Unaweza kupigwa karibu ya kituo cha polisi haimaanishi waliokupiga ni polisi, hivyo huyo inawezekana kabisa alipigwa hapo kona ya Mbauda karibu na ofisi za CCM lakini wahusika si Wana CCM, kwenye kesi kinachotafutwa ni ushahidi si hisia,” alisema kamanda huyo.

Snoop Dogg avuta Bangi za kufuru katika moja ya hoteli maarufu Australia

article-2544251-1ADC0EAB00000578-483_634x593
.aweka picha kadhaa kwenye mtandao wa Instagram
Na. MOblog Tanzania, Kwa msaada wa mtandao
Rapa maarufu nchini Marekani ametoa kali ya mwaka baada ya kupost picha kadhaa kwenye mtandao kuonyesha akivuta bangi kwenye moja ya hoteli Queensland Gold Coast maarufu kama Palazzo Versace nchini Australia.
Vyombo vya habari nchini Australia vimeripoti kuwa rapa huyo maarufu duniani alikwenda kufanya tamasha la mwaka la muziki lakini akaiishia kufanya vituko hotelini kwa kuvuta bangi siku nzima na kugonga vichwa vya habari vya Australia.
article-2544251-1AE333C100000578-841_634x512 
Rapa huyo mwenye umri wa miaka 42 aliweka picha nyingi akionyesha anavuta bangi kwa kwenda mbele na kwenye meza yake aliweka bangi nyingi kwenye bakuli tayari kuvuta lakini wachambuzi wa mambo wamesema ni kinyume cha sheria za Australia kuvuta bangi .
Nyota huyo ambaye anaonekana haguswi nchini marekani (untouchable) jina lake halisi ni Calvin Cordozar aka snoop dogg dogg akiwa amevaa shati la superman na rasta akivuta bangi kwenye moja ya hoteli hiyo maarufu nchini Australia.
Polisi nchini Australia wamethibitisha kwamba rapa huyo amevunja sheria za Australia kwa kuvuta bangi na kupiga picha na kuweka kwenye mitandao ya kijamii  na wanasubiri jinsi ya kumhoji kwa upepelezi zaidi.
article-2544251-1AE333C900000578-281_634x645
Afisa huyo wa Jeshi la Polisi nchini Australia amesema  ‘Hata kama sisi hatuna uwezo wa kupata mabaki ya bangi katika chumba cha hoteli, tunaweza kufanya upekuzi katika chumba chake kujiridhisha na tuhuma zake hizo,” amesema
Waziri uhamiaji wa Australia,  Scott Morrison ametishia kufuta visa ya rapa huyo maarufu kwa kukiuka sheria za nchi yao kwa kuvuta bangi na kuweka picha kwenye mitandao ya kijamii.

UJENZI DARAJA LA DUMILA LILILOSOMBWA NA MAJI -DK MAGUFULI AHAMIA MOROGORO KUSIMAMIA

Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli akiwa katika gari linaloendelea na ujenzi wa daraja la Dumila.

 
Sehemu ya barabara iliyozolewa na maji ya mto Mkundi.
 
Waziri wa Ujenzi akikagua maeneo yaliyoharibika.
 
Dk. Magufuli akiendelea na kazi katika daraja hilo.
 
Kazi za ujenzi zikiendelea eneo hilo la daraja lililoharibika.
 
Dk. Magufuli akiwapa hi mafundi wanaoendelea na ujenzi wa daraja hilo.
 
WAZIRI wa Ujenzi, Dk. John Pombe Magufuli amepiga kambi mkoani Morogoro kusimamia mwenyewe ujenzi wa Daraja la Dumila ambalo ni kiungo muhimu cha barabara ya Dodoma – Morogoro lililosombwa na mvua kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia tarehe 22.01.2014 na kusababisha magari kutopita kabisa ama yanayotoka upande wa Dodoma au Morogoro. Mbaya zaidi hakuna njia nyingine mbadala

Mwanamke afanyiwa ukatili Bukombe Geita.

Wanawake wa Tanzania tukimbilie wapi? Tukio hili limetokea kama wiki moja iliyopita...

Wilaya Ya BUKOMBE mkoa GEITA.   ILIRIPOTIWA NA RFA.
Ni matukioa yanayotokea Mara kawa mara. Wahanga(watendewa) ni WANAWAKE....See More
Wanawake wa Tanzania tukimbilie wapi? Tukio hili limetokea kama wiki moja iliyopita...

Wilaya Ya BUKOMBE mkoa GEITA.
ILIRIPOTIWA NA RFA.
Ni matukioa yanayotokea Mara kawa mara. Wahanga(watendewa) ni WANAWAKE.

Cha ajabu hakuna juhudi za makusudi za kutokomeza vitendo hivi....

Wanawake tusimame pamoja kusema inatosha Unyama huu tunaofanyiwa...

Poleni kwa picha mbaya sana, lakini tafakari maumivu aliyopata huyu mwanamke maskini ya Mungu...

Natamani hamasa ya kutokomeza ukatili ingefanyika kwa Chopa kama ....... malizia mwenyewe
  • Jackson B Derick Mungu apishe mbali na amsamehe huyu aliye fanya haya maana hakujua anafanya 
    nini Mungu yu anasema "hukumu ni juu yangu mimi" huyu aliyehukumu ameenda kinyume na sheria ya Mungu. Lets Turn on our backs tuache kujiondoa ufahamu na kufanya haya mabaya.
  • Godfrey Fidolin Otto Mhillu ninaiomba sanasana serikal ichukue hatua kali za kisheria dhidi ya watu wanaowafanyia wanawake unyama kama huo, tubadilike jamani tusiendelee kuvumilia haya maovu tuwachukulie hatua hawa watu wenye roho za kinyama na, tumuogope Mungu jaman
  • Mpalule Shaban

DR SLAA AKWAMA MBEYA MCHANA HUU



Picha kutoka maktaba ya Dr. Slaa akiwa Songea.
Dr Slaa amekwamba katika kijiji cha Jojo kata ya Santilya Mbeya vijiji baada ya helikopta kushindwa kuruka kutokana na ukungu mzito ulioambatana na mvua tangu saa 5 asubuhi. Amelazimika kwenda kwa gari hadi Ilembo saa 6:25 mchana huu.

JOHARI MAMBO SI SHWARI..ALAZWA HOI HOSPITALINI

Na: Hamida Hassan na Gladness Mallya
MASKINI! Ndiyo neno linaloweza kumtoka mtu yeyote mwenye mapenzi mema na staa wa filamu za Kibongo, Blandina Chagula ‘Johari’ ambaye kwa sasa afya yake si ya kuridhisha, Ijumaa lina kila kitu.
Blandina Chagula ‘Johari’.
Johari ni mgonjwa kwa zaidi ya siku tano sasa akiwa mtu wa kwenda hospitali mara kwa mara kwa ajili ya kuendelea na matibabu.
TAARIFA ZA AWALI
Shostito wa karibu na staa huyo alipiga simu chumba cha habari cha gazeti hili, wiki iliyopita akieleza kwamba Johari ni mgonjwa na amekuwa mtu wa kupumzika ndani.
Rafiki huyo ambaye aliomba hifadhi ya jina lake alisema: “Najua mtakuwa hamna hii habari, lakini kiukweli Johari anaumwa, jana (Jumanne iliyopita) nilikwenda kwake, hali niliyomkuta nayo kwa kweli nilimhurumia, yawezekana pia ile ishu yake na Ray inamchanganya, ukimuona amepungua, siyo yule unayemjua.”
Blandina Chagula ‘Johari’.
JOHARI ATAFUTWA
Katika kutaka kujiridhisha, mmoja wa wahariri wa Global Publishers, alimvutia waya Johari Jumanne iliyopita, ambapo alipokea na kuzungumza kwa shida huku sauti ikiwa chini sana.
“Siwezi kuzungumza vizuri, sauti yangu iko chini sana... nahisi kama inakauka. Naumwa sana. Nina fluu,” alisema Johari.
Baada ya mazungumzo hayo, gazeti hili lilipata uhakika kuwa ni kweli Johari ni mgonjwa lakini hakuwa ‘siriazi’ kivile, likachukulia poa.
HALI YABADILIKA
Siku mbili baadaye, chanzo chetu kilekile cha awali kilipiga tena simu na kutoa taarifa kuwa hali ya Johari ilibadilika ghafla na kwamba alifikishwa hospitalini.
Hata hivyo, alipoulizwa ni hospitali gani amelazwa, alisema hana uhakika lakini alisikia kama amepelekwa AAR ya Sinza. Simu ya Johari ilipopigwa, haikupatikana achilia mbali marafiki zake wa karibu.
MAPAPARAZI HOSPITALINI
Timu yetu ilifunga safari hadi Hospitali ya AAR (Sinza) na ile nyingine ya Posta na kujaribu kudodosa kama alifikishwa hospitalini hapo, likaambulia patupu.
STEVE NYERERE AANZA KAZI
Katika kuonyesha kuwa mwenyekiti mpya wa Klabu ya Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Nyerere’ amedhamiria kuweka umoja na ushirikiano kwa wasanii walio kwenye klabu hiyo kwenye shida na raha, ndiye aliyemtoa Johari hospitalini.
Steve Nyerere aliweka picha kwenye ukurasa wake wa Instergram inayomwonesha Johari akiwa katika hali ya kuugua, huku mkononi mwake akiwa na plasta iliyoonyesha kuwa alitundikiwa drip na kuandika: “Johari haya ndiyo maisha, usijali utapona.”
MAPAPARAZI NYUMBANI KWA JOHARI
Juzi Jumatano, timu ya waandishi wetu ilifunga safari hadi nyumbani kwa Johari, Ubungo – External, Dar ili kujua hali yake.
Hatua chache kabla ya kufika nyumbani kwake, gazeti hili lilimpigia simu, lakini hakupokea badala yake alilitumia ujumbe mfupi uliosema: “Siwezi kuongea, naomba unitumie meseji, naumwa sana na fluu, naamini nitapona. Nitakutafuta.”
Ijumaa: Nipo na karibu na kwako, nakuja kukuona.
Johari: Sipo nyumbani, nipo hospitalini.
Ijumaa: Hospitali gani?
Johari: AAR.
UHAKIKA
Pamoja na majibu ya Johari, bado gazeti hili lilitaka kujiridhisha zaidi, halikuishia njiani, lilifika hadi nyumbani kwake ambapo lilipokelewa na kijana wa kiume aliyekataa kutaja jina lake lakini alijitambulisha kama mdogo wake na Johari.
Alipoulizwa kuhusu Johari, haraka alisema: “Dada anaumwa, amekwenda hospitali. Kwa nini msiwasiliane naye kwenye simu?”
POLE JOHARI
Kuugua ni sehemu ya maisha Johari. Ni mitihani ambayo binadamu wote tumeumbiwa hivyo jipe moyo, utapona. Mungu aisimamie afya yako, upone haraka – Amina

Maandamano ya himo kuelekea kwenye operesheni ya #M4CPamojaDaima

  1. Kanda ya Magharibi Imeanza na Sikonge tayari imemaliza. Inaelekea Inyonga; ni jimbo la Mpanda Mashariki. Jimboni kwa Pinda
  2. . Imetisha kila mahala makamanda wanawakilisha.kwa damage waliyofanya kina MMs hii ndo inatakiwa! this mia mia!
  3. wasaliti wasipewe nafasiTena!Mbona hamumfukuzi yule Juha?
  4. Kuna jipya au stori zilezile za ufisadi? : Timu tatu za zitakuwa ...
  5. Timu tatu za zitakuwa zikishambulia kutokea angani na timu tatu zitakuwa zikisonga mbele nchi kavu ktk kuiteka Tz
  6. Msigwa na dr slaa wapo kusini na heche na lisuu kaskazini,
  7. Mkt Mbowe ataanza baada ya siku mbili zijazo kwenye timu yake anaendelea mnyika na makamu zanzibar

Thursday, January 23, 2014

Israeli Jet Parked Next to Iranian Sparks Davos Thaw

Photographer: Gwen Ackerman/Bloomberg
The aircraft of Iran's President Hassan Rouhani, left, stands alongside the aircraft of... Read More
Zurich air traffic controllers may have inadvertently succeeded where diplomats have failed for decades: to bring Israelis and Iranians together.
As the jets of Iranian President Hassan Rouhani and Israeli Prime Minister Benjamin Netanyahu arrived in Switzerland today to take their leaders to the World Economic Forum, their planes were parked side-by-side under cloudy skies.
Rouhani, the first Iranian leader in a decade to visit Davos for the World Economic Forum, will be looking for deals to boost an economy that shrank more than 5 percent in the last fiscal year through March under the weight of international sanctions. He’s due to address the forum in the ski resort tomorrow during a session called “Iran in the World.”
Netanyahu, among the most outspoken critics of the Iranian government, is seeking to keep the sanctions in place. He has called Rouhani a “wolf in sheep’s clothing” and urged the world to be wary of his “charm offensive.”

MAHABUSU MWANZA AJIPAKA KINYESI AKIJARIBU KUTOROKA.

Hatua kwa hatua chini ya ulinzi mkali wa askari shupavu.
Askari akiwa amemnasa mahabusu aliye kimbia mara baada ya kujipaka kinyesi katika mahabusu ya mahakama ya wilaya ya Nyamagana na Mahakama ya Mwanza.
 Baada ya kumkamata na kumrejesha katika chumba cha mahabusu mahakamani hapo, kwanza mtuhumiwa huyo aliamriwa kuzoa mtondoro wa kinyesi cha binadamu alichokuwa amejimwagia na kutapakaa chini na mara baada ya kumaliza kuzoa uchafu huo, alipelekwa kwa hakimu ambapo alisomewa kosa la kula njama za kutoroka na kukumbana na adhabu nyingine ya kuhukumiwa kifungo cha miezi sita (6) jela, huku kesi yake iliyokuwa ikimkabili awali ikiahirishwa.
"Kama alivyojipaka ndivyo alivyo yazoa..."
Moja baada ya jingine

Hatua kwa hatua chini ya ulinzi mkali wa askari shupavu.
Huku akiweka kinyesi hicho kwenye ndoo mahabusu huyo alilazimika kukizoa kwa mikono kama muuza mkaa apimavyo mkaa kwenye kopo kuwauzia wateja wake. 
Mchafuzi wa mazingira akiadabishwa kabla ya kwenda kusomewa kesi nyingine ya kula njama za kutaka kutoroka.
 HUWA YANASIKIKA KUTOKEA LAKINI LEO NI LAIVU BILA CHENGA Mahabusu mmoja aliyekuwa mahabusu ya mahakama ya wilaya ya Nyamagana na Mahakama ya Mwanzo iliyopo eneo la jirani na Mamlaka ya maji safi na Hifadhi ya Mazingira (MWAUWASA) jijini Mwanza alitoa vioja vya mwaka kwa kujaribu kutoroka kwa kujipaka kinyesi ili asiguswe wala kukamatwa.

Mtuhumiwa huyo ambaye jina lake halikufahamika alijimwagia kinyesi kilichokuwa kwenye ndoo iliyokuwa ndani ya sero ya Mahakamani hapo na askari alipokwenda kufungua ili kuwapeleka watuhumiwa kwenye chumba cha Mahakama kusomewa kesi yake baada ya kutajwa na karani wa Mahakama ya mwanzo, baada ya kutajwa ndipo mahabusu huyo alipopata mwanya wa kukimbia na kutoa tahadhari kwa atakaye mgusa au kumshika atakumbana na kadhia ya kuchafuliwa kwa kupakwa kinyesi.
Askari mwingine mwenye cheo cha sajenti, ambaye alikuwa akihushughulika na huduma nyingine mahakamani hapo, kwa kuwa alikuwa na uzoefu wa kupambana na mikasa na vioja kama hivyo vya mahabusu wanao kula njama za kutaka kutoroka aliamua kula naye sahani moja kwa kumkimbiza na kufanikiwa kumkamata.