TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, March 8, 2014

MBEYA CITY YAICHAPA RHINO 3-1, WAGOSI WA KAYA NGOMA NZITO, RUVU SHOOTING WAFUFUKA LEO!!

WAGONGA nyundo wa Mbeya, klabu ya Mbeya City wameibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya maafande wa Rhino Rangers katika mchezo wa ligi kuu soka Tanzania bara ndani ya dimba lao la Sokoine jijini Mbeya.
Mabao ya Mbeya City yamefungwa na said Kipanga aliyefunga mawili , huku la tatu likitiwa kimiani na Deus Kaseke.
Baada ya kumalizika kwa mchezo huo, afisa habari wa Mbeya City, Fredy Jackson  amesema kuwa mchezo ulikuwa mgumu sana kwani Rhino waliingia uwanjani kwa lengo la kutafuta pointi tatu.
“Rhino wameonesha upinzani mkubwa sana katika mchezo wa leo. Walidhamiria sana kupata ushindi, lakini ubora wa wachezaji wetu umetusaidia”. Alisema Fredy.
IMG-20131029-WA0076Vijana wa kocha Juma Mwambusi wamewabamiza Rhino Rangers 3-1. Wasema safari yao bado inaendelea.
IMG_1615Coastal Union wakiwa katika dimba la nyumbani, CCM Mkwakwani jijini Tanga wameshindwa kutamba mbele ya wageni wao, Ashanti United wanaonolewa na kocha Abdallah King Kibaden `Mputa`.

MJUMBE WA KAMATI KUU YA (CCM) JERRY SILAA AMPIGIA DEBE GODFREY MGIMWA KUCHUKUA JIMBO LA KALENGA

1Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala na mjumbe wa Kamati kuu ya Chama chama Mapinduzi (CCM) Bw. Jerry Silaa kulia akiteta jambo na Mgombea ubunge wa jimbo la Kalenga kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi Bw. Godfrey Mgimwa wakati wa mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika kwenye kijiji cha ibumila kata ya Mgama halamashauri ya wilaya ya Iringa vijijini mkoani Iringa, Jerry Silaa amewaomba wana Ibumila kumchagua Godfrey Mgimwa ili kukamilisha mipango mbalimbali aliyoiacha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Marehemu Dr. William Mgimwa. 2Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala na mjumbe wa Kamati kuu ya Chama chama Mapinduzi (CCM) Bw. Jerry Silaa akihutubia katika mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye kijiji cha Ibumila kata ya Mgama leo 3Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala na mjumbe wa Kamati kuu ya Chama chama Mapinduzi (CCM) Bw. Jerry Silaa wa pili kutoka kushoto akiwa katika mkutano huo kushoto ni mgombea ubunge wa jimbo la Kalenga kupitia CCM Bw. Godfrey Mgimwa na kutoka kulia ni Mwenyekiti wa UVCCM, Mkoa wa Simiyu,Njalu Silanga, Anthony Mavunde kutoka UVCCM Dodoma, Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa Hassani Mtenga4Mmoja wa wananchi akiserebuka huku akiwa amebeba beseni lake la ndizi katika mkutano huo. 5Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala na mjumbe wa Kamati kuu ya Chama chama Mapinduzi (CCM) Bw. Jerry Silaa kushoto akishiriki kuimba nyimbo za kuhamasisha katika mkutano huo wa kampeni aliofanyika kwenye kijiji cha Ibumila kulia ni Mwenyekiti wa UVCCM, Mkoa wa Simiyu,Njalu Silanga na Anthony Mavunde kutoka Dodoma wakijumuika pamoja. nanWa 7Wananchi wakimlaki mgombea ubunge wa Kalenga kupitia CCM Bw. Godfrey Mgimwa wakati alipowasili katika kijiji cha Mgama kata ya Mgama. 9Jeshi la polisi likiimarisha ulinzi katika mikutano hiyo 10Wananchi wakimlaki mgombea ubunge wa Kalenga kupitia CCM Bw. Godfrey Mgimwa kwa kumbeba juu juu,  wakati alipowasili katika kijiji cha Mgama kata ya Mgama. 12 Kada wa chama cha Mapinduzi Bw. Fredrick Mwakalebela akipigia debe mgombea ubunge wa jimbo la Lalenga kupitia CCM Bw. Godfrey Mgimwa katika kijiji cha Mgama kata ya Mgama wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika kijijini hapo leo. 13 
Mgombea ubunge wa jimbo la Lalenga kupitia CCM Bw. Godfrey Mgimwa akivishwa mgorole na wazee wa kimila kama ishara ya heshima mara baada ya kuwasili katika  kijiji cha Mgama kata ya Mgama wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika kijijini hapo leo.

Dkt Fenella aadhimisha siku ya wanawake dunia kwa kushiriki bonanza la mpira kikapu!!

DUCE 1 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akizungumza na wanawake mbalimbali (hawapo pichani) wakati wa ufunguzi wa Bonanza la Mpira wa Kikapu lililoandandiliwa na Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania (TBF) leo jijini Dar es Salaam katika viwanja vya DUCE. Kushoto ni Mkuu wa Kitivo cha Sayansi chuoni hapo Dkt. Constansia Rugumamu na kuli ni Kamishina wa wanawake TBF Bi. Angella Grolia Bondo.DUCE 2 Kamishina wa wanawake TBF Bi. Angella Grolia Bondo akitoa maelezo kuhusu Bonanza la Mpira wa Kikapu lwaliloandaa kwa ajili ya kuadhimisha siku ya wanawake dunia,Mwenye koti jeupe ni jijini Dar es Salaam katika viwanja vya DUCE. Kushoto ni Mkuu wa Kitivo cha Sayansi chuoni hapo Dkt. Constansia Rugumamu na kulia ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi katika bonanza hilo.DUCE 4 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara (kushoto)akifurahia zawadi ya picha yake ambayo imetolewa na Mwenyekiti wa Baraza la Miochezo la Taifa Bw. Dioniz Malinzi (hayupo pichani) na kukabidhiwa kwa niaba yake na Kamishina wa wanawake TBF Bi. Angella Grolia Bondo leo jijini Dar es Salaam.DUCE 6 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara uwanjani tayari kwa kuzindua rasmi bonanza hiloDUCE 7 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara kwa makini maelezo kuhusu huduma za NSSF (ambao ndiyo wadhamini wa bonanza hilo)kutoka kwa Afisa Uhusiano wa shirika hilo Bi. Maife Kapinga mara baada ya kuwasili uwanjani tayari kwa kufungua bonanza leo jijini Dar es Salaam.. NSSF ndiyo wadhamini wakuu wa bonanza hiloDUCE 8 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akikagua wachezaji wa timu ya Don Bosco Lioness kabla ya mchezo wao kuanza. Mechi ya ufunguzi wa bonanza ilikuwa kati ya Jeshi Star na Don Bosco Lioness ambapo hadi mchezo unamalizika Don Bosco Lioness waliibuka kidedea kwa jumla ya Vikapu 23 dhidi ya 19 vya Jeshi Star.DUCE 10Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akipiga shot kuashiria ufunguzi rasmi wa bonanza hilo 
Picha zote na Frank Shija – WHVUM

NBS YATOA TAARIFA YA MFUMUKO WA BEI NCHINI

NBS - 2 NBS - 1Mkurugenzi wa Takwimu za Jamii na sensa ya Watu na Makazi Bw. Ephraimu Kwesigabo akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu  mfumuko wa bei nchini..
…………………………………………………
Na  Aron Msigwa – MAELEZO, Dar es salaam.
 
Ofisi ya Taifa ya Takwimu imesema kuwa hali ya mfumuko wa bei nchini imeendelea kuwa katika kiwango kisichobadilika katika kipindi cha mwezi Januari na Februari mwaka huu kutokana na kupungua kwa kasi ya upandaji wa bei za bidhaa na huduma mbalimbali. 
 
 Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa Takwimu za Jamii na sensa ya Watu na Makazi Bw. Ephraimu Kwesigabo amesema kuwa mfumuko wa bei wa Taifa kwa mwezi Februari 2014 umeendelea kubaki katika kiwango cha  asilimia 6.0 kama ilivyokuwa mwezi Januari mwaka huu.
 
Amesema  kuwa kasi ya upandaji wa bei za bidhaa na huduma kwa mwezi Februari 2014 imebakia kuwa sawa na ile iliyokuwepo mwezi Januari  huku kukiwa na ongezeko dogo la upandaji wa bei  kwenye baadhi ya bidhaa na huduma mwezi kwa mwezi Februari 2014 ikilinganishwa na bei za mwezi Februari mwaka jana.
 
 Ameeleza kuwa mfumuko wa bei za bidhaa za vyakula na migahawa kwa mwezi Februari umeongezeka hadi asilimia 6.9 kutoka asilimia 6.6 za mwezi Januari mwaka huu huku bidhaa zisizo za vyakula kasi ya ongezeko la bei ikipungua hadi asilimia 6.3 mwezi Februari 2014 kutoka asilimia 6.7 za mwezi Januari mwaka jana.
 
Amefafanua kuwa mwenendo wa bei za bidhaa za vyakula kama samaki, mbogamboga, ulezi na matunda zimeonyesha kuongezeka kwa kiwanga kikubwa kwa mwezi Februar ikilinganishwa na bei za bidhaa hizo kwa mwaka uliopita huku bei za bidhaa zisizo za vyakula za vitambaa vya suti za wanaume, kodi za pango la kuishi, mkaa, na nauli za bajaji zikionyesha ongezeko.
 
Kwa upande wa  mfumuko wa bei unaopimwa kwa kipimo cha mwezi,ameeleza kuwa kumekuwa na ongezeko kwa asilimia 1.4 ikilinganishwa na ongezeko la asilimia 1.8  kwa Januari mwaka huu, huku fahirisi za bei za taifa zikiongezeka hadi kufikia 148.62 kati ya Februari mwaka uliopita na Februari mwaka huu.
 
Amezitaja bidhaa zilizochangia ongezeko la fahirisi za bei nchini  kuwa ni pamoja na dagaa,samaki wakavu, mbogamboga na viazi mviringo  huku bidha zisizo za vyakula zikiwa pombe za kienyeji, vitambaavya suruali, viatu vya wazi vya plastic, mafuta ya dizeli na  Petroli pamoja na huduma za unyoaji na usafi wa nywele.
 Aidha kufuatia hali hiyo  ya mfumuko wa bei Bw. Kwesigabo ameeleza kuwa  uwezo wa shilingi 100 ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma za jamii kwa mwezi Februari  umeonyesha kupungua na kufikia shilingi 67 na senti 29.
 
“Kupungua kwa thamani ya Shilingi kunamaanisha kwamba, kama mtu alikuwa na uwezo wa kununua bidhaa kwa Shilingi 100 mwaka jana, basi kwa mwaka huu itampasa aongeze zaidi ili aweze kununua kitu kama kile kile, kwa mfano badala ya shilingi 100 inabidi atumie Shilingi 132”
 
Kuhusu ulinganifu  mfumuko wa bei wa Tanzania na baadhi ya nchi za Afrika Mashariki amesema kuwa una mwelekeo unaofanana na kueleza kuwa mfumuko wa bei nchini Kenya umepungua kidogo na kufikia asilimia 6.86 kwa mwezi Februari  kutoka asilimia 7.21 za mwezi Januari ,  huku  Uganda ikiwa na asilimia 6.7 kwa mwezi uliopita  kutoka asilimia 6.9  za mwezi Januari.

Rais Dkt. Kikwete Amfariji Sophia Simba

D92A3483 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini katika kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Waziri wa Maendeleo ya jamii jinsia na Watoto Mhe.Sophia Simba kufuatia kifo cha mwanaye Marehemu Leeford Simba huko Mikocheni jijini Dar es Salaam leo.Marehemu Leeford Simba anatarajiwa kuzikwa leo katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.D92A3503 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji Neema Mathew(kulia) na waombolezaji wengine kufuatia kifo cha Mumewe Leeford Simba kilichotokea juzi. Marehemu Leeford Simba ni mtoto wa Waziri wa Maendeleo ya Jamii jinsia na Watoto Mhe.Sophia SimbaD92A3511Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpa mkono wa pole na kumfariji Waziri Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto Mhe.Sophia Simba kufuatia kifo cha Mwanaye Leeford Simba wakati wa ibada ya kumuombea marehemu iliyofanyika nyumbani kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam leo.Marehemu Leedford anatarajiwa kuzikwa leo katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam(picha na Freddy Maro)

MAMA PINDA ATAKA WAZAZI WAJALI ELIMU YA WATOTO WAO BILA KUWABAGUA


IMG_0136MKE WA WAZIRI MKUU, Mama Tunu Pinda amewataka wazazi hapa nchini watoe kipaumbele kwenye suala la elimu kwa vijana bila ubaguzi wa kijinsia.
Ametoa wito huo leo mchana (Jumamosi, Machi 8, 2014) wakati akifungua Kongamano la Wanawake wa Afrika ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani lililofanyika kwenye ukumbi wa Karimjee, jijini Dar es Salaam.
Kongamano hilo liliandaliwa na Chama cha Walimu Wanawake Tanzania (Tanzania Women Teachers’ Association – TAWOTEA) kwa kushirikiana na taasisi ya African Women Charity Organisation ya Oakland, California, Marekani.
Akizungumza na washiriki wa kongamano hilo, Mama Tunu Pinda alisema: ”Ninawaomba wazazi wenzangu, wake kwa waume tuungane kwa pamoja kwa kutoa kipaumbele kwenye suala zima la elimu kwa vijana wetu bila ubaguzi wa kijinsia. Kwa kufanya hivyo tutawajenga wavulana na wasichana ili wawe na uwezo wa kiuchumi na uthubutu katika masuala ya uongozi na maisha yao ya baadaye.”

Akizindua mfuko wa elimu ulioanzishwa na chama hicho, Mama Pinda  alisema ana imani utakuwa endelevu na utakidhi malengo ya kuazishwa kwake ambayo ni kuwasaidia watoto wenye uhitaji na waishio kwenye mazingira ili wapate elimu ya msingi na ya sekondari.
”Mkiwa ni waalimu wanawake na tena ni walezi wa watoto wetu, mmefanya jambo kubwa na la kihistoria kwa kuanzisha mfuko wa elimu mlioamua kuuita Tanzania Education Fund (TEF). Nimedokezwa kwamba malengo ya mfuko huu ni kusaidia gharama za elimu ya msingi na sekondari kwa watoto wa kike na wa kiume na hasa kwa watoto walio kwenye mazingira magumu na wenye uhitaji. Ni matumaini yangu kwamba utakuwa endelevu.”
”Ni imani yangu kwamba kupitia mfuko huu unaozinduliwa rasmi leo hii, utaowaongezea vijana wetu wa kike na wa kiume wigo wa kupata elimu ambapo kama mfuko huu usingekuwepo, isingekuwa rahisi kwao kumudu gharama za masomo,” aliongeza.
Aliwaomba wadau wote wa elimu na wananchi kwa ujumla, waunge mkono juhudi za walimu hao katika kuikomboa nchi hii, hasa katika sekta ya elimu huku wakiamini elimu ni ufunguo wa maisha.
Mapema, akisoma risala yao, Mkurugenzi Mtendaji wa TAWOTEA, Mwl. Neema Kabale alisema asasi hiyo ambayo imesajiliwa tangu mwaka 2008, inajihusisha na utetezi wa haki za msingi za wanawake, wasichana, vijana na watoto katika masuala ya elimu, afya, na upatikanaji wa chakula.
Katika kongamano hilo la siku moja, asasi hiyo iliandaa mada sita zikiwemo za “Ushiriki wa wanaume katika ukombozi wa mwanamke” na “Majukumu ya Vijana katika Muungano wa Afrika”.
Akitoa hitoria fupi ya Kongamano la Wanawake Afrika, Rais wa taasisi ya African Women Charity Organisation ya Oakland, Marekani, Bi. Rwanda Saleem, alisema Tanzania ni nchi ya nane kupata fursa ya kuratibu wa kongamano kama hili.
”Barani Afrika tayari nchi saba zimekuwa  waratibu wa kongamano hili ambazo ni Ghana, Guinea, Gambia, Senegal, Kenya, Rwanda, na Msumbiji ambayo ilikuwa mwenyeji mwaka jana. Tanzania imepewa fursa ya kuandaa kongamano hili mwaka huu,” aliongeza.
Kaulimbiu ya kongamano hilo ni “Kujenga Muungano wa Afrika kwa Kushirikisha Wanawake kwenye Uongozi” (The Unification of Africa Through the Emancipation of Leadership of Women). 
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 3021,
DAR ES SALAAM.
JUMAMOSI, MACHI 8, 2014

MEGATRADE YAVIPIGA JEKI VILABU VYA POLISI KILIMANJARO NA MACHAVA FC VYA MJINI MOSHI

 Meneja masoko wa kampuni ya Megatrade (T) Ltd,Goodluck Kway akimkabidhi mkuu wa mkoa
wa Kilimanjaro Leonidas Gama jezi zenye thamani ya kiasi cha sh Milioni 3 ikiwa ni sehemu ya msaada kwa timu ya soka ya
Machava fc inayoshiriki ligi daraja la tatu ngazi ya mkoa wa Kilimanjaro.shoto
kwake ni Meneja mauzo wa Kampuni ya Megatrade(T)Ltd kanda ya kaskazini Edimund
Lutaraka.
 Meneja masoko wa kampuni ya Megatrade (T) Ltd,Goodluck Kway akimkabidhi mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama Mpira ikiwa ni sehemu ya msaada kwa timu ya soka ya Machava fc inayoshiriki ligi 
daraja la tatu ngazi ya mkoa wa Kilimanjaro.shoto kwake ni Meneja mauzo wa Kampuni ya Megatrade(T)Ltd kanda ya kaskazini Edimund Lutaraka.
 Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama akimkabidhi jezi nahodha wa timu ya
Machava ,Dickson Muganda.Jezi hizo zenye thamani ya kiasi cha sh Milioni 3 zimetolewa
na kampuni ya Megatrade ikiwa ni sehemu ya msaada kwa timu hiyo inayoshiriki ligi daraja la tatu ngazi ya mkoa wa Kilimanjaro.
 
 Meneja masoko wa kampuni ya Megatrade (T) Ltd,Goodluck Kway  akikabidhi hundi ya sh Milioni 3 kwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama ikiwa ni sehemu ya msaada kwa timu ya soka ya Machava fc inayoshiriki ligi daraja la tatu ngazi ya
mkoa wa Kilimanjaro.shoto kwake ni Meneja mauzo wa Kampuni ya Megatrade(T)Ltd kanda ya kaskazini Edimund Lutaraka.
Meneja masoko wa kampuni ya Megatrade (T) Ltd,Goodluck Kway akimkabidhi kamanda wa Polisi, Robert Boaz jezi zenye thamani ya kiasi cha sh Milioni 3 ikiwa ni sehemu ya msaada kwa timu ya soka ya Machava fc inayoshiriki ligi daraja la tatu ngazi ya mkoa wa Kilimanjaro.shoto kwake ni Meneja mauzo wa Kampuni ya Megatrade(T)Ltd kanda ya kaskazini Edimund
Lutaraka.
 Viongozi wa klabu ya Polisi Kilimanjaro.
Viongozi wa timu ya Polisi Kilimanjaro wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa kampuni ya Megatrade(T)Ltd muda mfupi baada ya kukabidhiwa zawadi.

KAMISHNA JENERALI WA JESHI LA MAGEREZA NCHINI, JOHN MINJA AHUDHURIA SHEREHE ZA KUFUNGA RASMI MAFUNZO KOZI NAMBA 08 YA MWAKA 2014 KWA MAAFISA MAGEREZA NCHINI MSUMBIJI

1 Rais wa Msumbiji, Mhe. Armando Emilio Guebuza(kulia vazi jeupe) akikagua Gwaride Maalum lililoandaliwa na Maafisa Magereza Wahitimu wa taaluma ya Uaskari Magereza Nchini Msumbiji katika Sherehe za kufunga Mafunzo hayo zilizofanyika Machi 07, 2014 katika Chuo cha Maafisa Magereza kilichopo Maputo, Msumbiji ambapo Nchi mbalimbali za Afrika zilialikwa zikiwemo Afrika Kusini, Zambia, Namibia, Zimbabwe, Swaziland pamoja na Tanzania. Jumla ya Wahitimu Maafisa 430 wamehitimu vyema mafunzo hayo ya Uaskari wa Magereza.2 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Tanzania, John Casmir Minja(wa nne toka kulia) akiwa meza Kuu pamoja na Wakuu wa Magereza toka nchi mbalimbali za Afrika katika Sherehe za kufunga rasmi Mafunzo ya taaluma ya Uaskari Magereza kwa Maafisa Magereza wa Msumbiji. Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa ni Rais wa Msumbiji, Mhe. Armando Emilio Guebuza(wa tatu toka kulia) ni Kamishna wa Magereza nchini Zambia, Percy Chato.3 Gadi ya Maafisa Magereza wa Msumbiji Wanaume wakipita kwa mwendo wa haraka wakitoa heshima mbele ya Mgeni rasmi, Rais wa Msumbiji, Mhe. Armando Emilio Guebuza katika hafla fupi ya ufungaji Mafunzo ya taaluma ya Uaskari Magereza kwa Maafisa 430 wa Magereza yaliyofanyika Machi 07, 2014 Maputo, Msumbiji.4Kamishna Jenerali wa Magereza Tanzania, John Casmir Minja akisalimiana kwa kushikana mikono na Rais wa Msumbiji, Mhe. Armando Emilio Guebuza(kama wanavyoonekana katika picha) baada ya hafla fupi iliyotanguliwa na Gwaride Maalum katika Sherehe za kufunga rasmi Mafunzo ya taaluma ya Uaskari Magereza ambapo jumla ya Maafisa Magereza 430 wamehitimu taaluma hiyo Machi 07, 2014 Maputo, Msumbiji (kulia pembeni kwa Jenerali Minja) ni Waziri wa Sheria Nchini Msumbiji, Mhe. Bervinda Levi.5Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Tanzania, John Casmir Minja(wa nne toka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wakuu wa Vyombo vya Urekebishaji/Magereza Afrika, Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza Nchini Msumbiji pamoja Maafisa Magereza Wahitimu wa Kozi namba 08 ya Mwaka 2014 ya taaluma ya Magereza (upande wa kulia). Wa tano toka kulia ni Kamishna wa Magereza Nchini Zambia, Percy Chato(wa tano toka kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini Namibia, Raphael Hamunyela(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

Matukio katika picha Siku ya Wanawake Duniani jijini Dar

DSC_0363 Wanawake wanaowakilisha Wizara ya Maliasili na Utalii wakipita mbele ya mgeni rasmi katika uwanja wa Mwembe-yanga.DSC_0321 Bibi aliyefurahia maandamano ya wanawake wenzake na kujiunga nao kusheherekea siku ya wanawake duniani.DSC_0336 Wanawake wa Wizara ya Maliasili na Utalii wakiserebuka wakati wa maandamano kuelekea uwanja wa Mwembe-yangaDSC_0350Baadhi wa wanawake wa wizara ya maliasili na utalii wakijiandaa kujiunga kwenye maandamano nje ya uwanja wa Mwembe – yanga

KAMPUNI YA TANZANIA DISTILLERIES LTD. KONYAGI WASHEREKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

Baadhi ya wanawake wafanyakazi wa kampuni ya Tanzania Distilleries Ltd. | Konyagi wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani inayoadhimishwa march 8 kila mwaka


Baadhi ya wanawake wafanyakazi wa kampuni ya Tanzania Distilleries Ltd.  Konyagi wakiwa katika maandamano yaliyoanzia ofisini kwa wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani iliyoadhimishwa march 8 kila mwaka


Baadhi ya wanawake wafanyakazi wa kampuni ya Tanzania Distilleries Ltd. |Konyagi wakiwa katika maandamano wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani iliyoadhimishwa march 8 kila mwaka na kuishia katika viwanja vya mwembeyanga Dar es salaam


Baadhi ya wanawake wafanyakazi wa kampuni ya Tanzania Distilleries Ltd.  Konyagi wakiungana na wanawake wenzao kutokasehemu mbalimbali kuadhimisha maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani katika viwanja vya mwembeyanga Dar es salaam


Baadhi ya wanawake wafanyakazi wa kampuni ya Tanzania Distilleries Ltd. | Konyagi wakiangalia bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na wanawake wenzao katika viwanja vya mwembe yanga Dar es salaam  wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani inayoadhimishwa March 8 kila mwaka


Baadhi ya wanawake wafanyakazi wa kampuni ya Tanzania Distilleries Ltd.  Konyagi wakiangalia bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na wanawake wenzao katika viwanja vya mwembe yanga Dar es salaam  wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani inayoadhimishwa March 8 kila mwaka

ATCL yapata ndege mpya, Yaanza utekelezaji wa mkakati wa kuimarisha huduma zake

ATCL 2Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Ndege la ATCL, Kapteni Milton Lazaro (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa shirika hilo mara baada ya kuwasili kwa ndege mpya ya shirika hilo aina ya CRJ-200, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam Alhamis usiku.ATCL 3 Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Ndege la ATCL, Kapteni Milton Lazaro (Kulia) akiwatambulisha baadhi ya watendaji wa shirika hilo mara baada ya kuwasili kwa ndege mpya ya shirika hilo aina ya CRJ-200, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam Alhamis usiku.ATCL 4 Wafanyakazi wa Shirika la Ndege la Taifa Air Tanzania (ATCL) wakisheherekea mara baada ya kuwasili kwa ndege mpya ya shirika hilo aina ya CRJ-200, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam Alhamis usiku.ATCL 5 ATCL 6Picha ya ndege mpya ya Shirika la Ndege la Taifa (ATCL), aina ya CRJ-200 ya nchini Canada, mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam Alhamis usiku.
……………………………………………………………………………………………………………..
  •  Yaanza utekelezaji wa mkakati wa kuimarisha huduma zake
  • Kupata ndege mbili mpya zenye uwezo wa kubeba abiria 78 ifikapo mwezi Mei
  • Yaondoa adhabu na masharti magumu kwa abiria wanaobadilisha tarehe za safari na wanaochelewa kufika uwanjani siku ya safari 
Na Mwandishi Wetu.
SHIRIKA la Ndege la Taifa (Air Tanzania) limepata ndege nyingine aina ya CRJ-200 ya nchini Canada yenye uwezo wa kubeba abiria 50, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati wake madhubuti wa kuimarisha huduma zake.
Shirika hilo la Air Tanzania (ATCL) linaona ujio wa ndege hii kama chachu ya kutimiza azma yake ya kuimarisha huduma zake ikiwa ni pamoja na kuongeza safari zake katika njia wanazoruka kwa sasa, kuanzisha njia nyingine mpya, na kuwahakikishia wateja wake uhakika wa huduma zake.  
Mara tu baada ya ndege hiyo kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Alhamis usiku, Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa ATCL, Captain Milton Lazaro alisema kuwa kuna matumaini makubwa ya Shirika la Ndege la Taifa kufanya vizuri zaidi katika utoaji wa huduma za usafiri wa anga, ikizingatiwa kuwa shirika lina mkakati madhubuti wa upanuzi wa huduma zake ambao utekelezaji wake umeanza.
“Ndege tuliyoipokea leo hii, ni sehemu ya ndege tatu tulizopanga kuleta mwaka huu. Ndege nyingine mbili zinatarajiwa kufika kati ya mwezi Aprili na Mei mwaka huu. Kuongezeka kwa idadi ya ndege zetu kutatuwezesha sisi kufungua mipaka kwa kuanzisha njia mpya na kuongeza safari nyingi zaidi katika maeneo tunayoenda kwa sasa,” alisema Kapteni Lazaro.  
Alisema kuwa ndege mbili zitakazoletwa nchini ifikapo Mei, zinauwezo wa kubeba abiria 78 na ni toleo jipya katika sekta ya usafiri wa anga, na zitatumika katika kusafirisha abiria ndani na nje ya nchi.
Kapteni Lazaro alisema kuwa shirika lake linampango wa kuanzisha safari mpya ikiwa ni pamoja na ya Tabora – Mpanda, Mbeya- Dar es Salaam na kuongeza idadi ya safari za Mwanza- Dar es Salaam, Dar es Salaam-Comoros na Mtwara pamoja na Kigoma.
“Kwa ongezeko hili la safari zetu, abiria wetu watafurahia safari za kila siku za kutoka Dar es Salaam kwenda Mwanza, ikiwa muda wa kuondoka Dar kuwa 1600hrs na kutoka Mwanza kuwa 1800hrs. Tutakuwa tukienda mkoani Mbeya mara nne kwa wiki; kwa siku za Jumatatu, Jumatano, Ijumaa na Jumapili. Wakati Moroni katika visiwa vya Comoro tutakwenda katika siku za Jumatatu, Jumatano, Ijumaa na Jumamosi. Na pia tunategemea kuzindua safari ya Tabora – Mpanda hivi karibuni,” alisema.  
Aliongeza kuwa shirika hilo pia limeondoa baadhi ya adhabu watozwazo abiria endapo wanashindwa kusafiri siku na muda waliyoomba, na kusema kuwa hii itawasaidia abiria wao kutoingia gharama za ziada endapo watakumbana na dharura mbali mbali kabla ya safari.
“Katika jitihada za kuwasaidia abiria wetu na kuwaonyesha kuwa tunayatambua mazingira tunayoishi na yakibiashara vizuri, shirika limeamua kuondoa adhabu kwa abiria ambao watashindwa kufika uwanja wa ndege kabla ya muda wa ndege kuondoka na adhabu ya kubadilisha safari,” alisema Kapteni Lazaro.
Kwa mujibu wa Ofisa Mtendaji huyo, upatikanaji wa ndege hiyo utaongeza idadi ya abiria kwa kati ya asilimia 30 mpaka 40, kutokana na kuwa huduma za shirika hilo bado ni nzuri na viwango vya nauli ni vya kiushindani zaidi na vyenye unafuu ukilinganisha na mashirika mengine.
Kwa kutumia ndege yake aina ya Bombardier Dash-8, ATCL kwa sasa inasafiri katika zaidi ya maeneo nane (8) nchini Tanzania ikiwa ni pamoja na Mtwara, Mwanza, Tabora, Kigoma, Dar es Salaam, Mbeya, Bujumbura na Moroni nchini Comoro.