TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, March 5, 2014

MADIWANI 23 MERU WATAKA KUJIUZULU

picture2bno-2b2Na Gladness Mushi, Meru
BARAZA la madiwani Meru lenye jumla ya madiwani 23 limeathimia kujiuzulu nyadhifa hiyo ya udiwani endapo kama Serikali haitaweza kuingia kati masakata mbalimbali ya migogoro ya radhi iliyodumu kwenye halmashauri hiyo kwa muda mrefu
Uamuzi huo uliwekwa hadharani juzi mara baada ya kumalizika kwa baraza la madiwani lililofanyika katika halmashauri ambapo lilitoa siku chache kwa serikali kuweza kuingilia kati.
Akiongelea sakata hilo mmoja wa madiwani wa Halmashauri hiyo loti Nnko alisema kuwa sakata la migogoro ya ardhi kwenye halmashauri hiyo limedumu kwa muda mrefu sasa ndio maana wwamefikia uamuzi wa kutaka kujiengua katika nyadhifa hiyo ya udiwani.
Nnko alisema wanachokisubira kwa sasa ni majibu kutoka kwa kamati ambayo wameiunda ambapo kamati hiyo itaenda Jijini Dar es saalam wiki ijayo na watakaporudi basi watarudi na majibu ambayo yataweza kuwafanya kuondoka kwenye viti hivyo vya udiwani.
Akitolea mfano moja yashamba lenye migogoro katika Halmashauri hiyo,shamba la  Madira lililopo katika maeneo ya Seela Singisi ambalo  ni mali halisi ya Halmasahuri hiyo lakini kwa sasa kuna migogoro ambayo inasababishwa na baadhi ya viongozi jambo ambalo wamedai kuwa hawataweza kuvumilia bali wataingia katika vita kwa mara nyingine
“kwa mfano hili shamba la Seela Singisi ni mali ya wananchi wote wa Meru na hadi Raisi ameshaweka saini yake jamani litumike kwa ajili ya matumizi ya kata zote za Meru lakini vigogo wanasema ni mali yao alafu bado tumenyamaza tu haitawezekana tunaachia udiwani alafu htunaingia katika Vita kwa mara nyingine”aliongeza Kimu.
“hili ni tamko rasmi tunatoa tunataka majibu ya migogoro hii rasmi kama hatupewi itakuwa ni vita baina ya Wameru na hawa wanaojichukulia ardhi kinyemelea, pia itakuwa ni huzuni kubwa kwa CCM  manake kwanza sisi wote hapa tunatokea CCM uzalendo umetushinda kabisa”aliongeza Nyiti
Naye Mwenyekiti wa Halmasahuri hiyo ya Meru, Goodson Majola alisema kuwa tamko hilo la kutaka kujiuzulu kwa madiwani 23 wote wa halmashauri hiyo lipo sawa kabisa kwa kuwa migogoro yote ya ardhi inasababishwa na Viongozi wasio waadilifu kuanzia ngazi ya Halmashauri hadi Wizara
“mimi nasema kuwa tutajiuzulu wiki chache zinazokuja baada ya kujiridhisha juu ya maangaiko haya ya ardhi ambayo yamedumu toka karne hadi karne na ninasiistiza kuwa itakuwa ni kilio kwa CCM kwa kuwa wanchama wetu nao tutaweka chini ya ulinzi hadi tutakapowaambia hawatajishugulisha na shuguli yoyote ya chama”alisema Majola.
Majola alisema kuwa kujiuzulu kwao lakini pia kuondoka na wanachama wote wa CCM katika Wilaya hiyo ni uzalendo wao kwa wananchi na hivyo Hata CCM nao hawapaswi kuumia kwa hilo.

No comments:

Post a Comment