TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, December 26, 2015

Mafuriko makubwa Amerika ya Kusini, Uingereza

Watu wapatao 140,000 wameokolewa kufuatia mafuriko makubwa katika mataifa manne ya Amerika ya Kusini. Paraguay ndiyo nchi iliyoathirika vibaya na mafuriko hayo, ambapo hali ya hatari imetangazwa. Maafisa wanasema wengi wa watu waliopoteza makaazi yao ni familia masikini zinazoishi kandoni mwa Mto Paraguay, karibu na mji mkuu, Asuncion. Maelfu ya watu nchini Uruguay, Brazil na Argentina pia wamekimbia makaazi yao. Watabiri wa hali ya hewa wanasema kumekuwa na mvua kali za El Nino na zisizo za kawaida katika msimu huu wa kaskazi. Kwengineko, barani Ulaya mvua kubwa imesababisha mafuriko kaskazini mwa kisiwa cha England. Mito mikubwa katika miji ya Manchester na Leeds imefurika na wakaazi kwenye kaunti za Lancashire na West Yorkshire wamehamishwa. Jeshi la Uingereza limeitwa kusaidia uokozi.

Youla ateuliwa waziri mkuu mpya wa Guinea

Rais Alpha Conde wa Guinea amemteua waziri mkuu mpya, baada ya kuapishwa mapema wiki hii kwa muhula mpya wa miaka mitano wenye utata. Mamady Youla, mchumi ambaye amefanya kazi serikalini na kwenye sekta binafsi, anachukuwa nafasi ya Mohamed Said Fofana, aliyejiuzulu Jumatano iliyopita. Youla, mwenye umri wa miaka 54, amepewa jukumu la kuunda serikali itakayojikita kwenye uundaji wa nafasi mpya za ajira, kuinua maisha ya vijana na kuuimarisha uchumi wa taifa hilo la kipato cha chini. Conde, mwenye umri wa miaka 77, alichaguliwa kwenye uchaguzi wenye utata hapo mwezi Oktoba na akaapishwa Jumatatu iliyopita. Mwezi uliopita, mahakama ya katiba ilitupilia mbali madai ya wapinzani kwamba ushindi wa asilimia 57.8 wa kiongozi huyo ulikuwa wa wizi.

Al-Shabaab yapoteza mshambuliaji 1, yaua polisi 1 Kenya

Mshambuliaji mmoja wa kujitoa muhanga ameuawa kaskazini mwa Kenya, baada ya kuripukiwa na bomu alilokuwa akilitega hapo jana. Afisa mmoja wa polisi wa mji wa Mandera, Suleiman Rashid, ameliambia shirika la habari la AP kwamba maafisa waliokuwa kwenye doria waliwakamata washukiwa watano wa kundi la al-Shabaab wakitega bomu barabarani, lakini  mmoja wao akaliripua na kusababisha kifo chake. Juzi Ijumaa, anamgambo wa kundi hilo waliushambulia msafara wa polisi na kumuua afisa mmoja. Msemaji wa al-Shabaab, Sheikh Abdiasis Abu Musab, alisema awali waliliacha gari lililobeba abiria lililokuwa likisindikizwa na polisi hao. Polisi ya Kenya imethibitisha kupoteza askari wake mmoja kwenye mashambulizi hayo.

Israel yauwa Wapalestina wawili

Vikosi vya Israel vimewauwa Wapalestina wawili kwenye mashambulizi mawili tafauti hapo jana. Mtu mmoja mwenye umri wa miaka 56 alipigwa risasi na kuuawa wakati akijaribu kumponda mwanajeshi kwa gari katika kituo cha ukaguzi cha Huwara, Ukingo wa Magharibi. Masaa kadhaa kabla ya hapo, polisi mjini Jerusalem walimpiga risasi na kumuua kijana mmoja wa Kipalestina katika eneo la Mji Mkongwe, wanayesema alitoa kisu wakati  wa kukaguliwa. Kwa mujibu wa vyanzo vya upande wa Wapalestina, maafisa wa polisi wa Israel walirusha mabomu ya machozi na risasi za mpira dhidi ya waandamanaji wapatao 150, ambapo watu 20 walijeruhiwa. Tangu kuanza kwa vuguvugu jipya la maandamano ya mitaani hapo mwezi Oktoba, vikosi vya Israel vimeshawauwa zaidi ya Wapalestina 130, huku Waisraili 18 wakipoteza maisha kwa kushambuliwa kwa visu.

Rais wa Czech asema wahamiaji ni uvamizi uliopangwa

Rais Milos Zeman wa Jamhuri ya Czech amesema wimbi la wakimbizi barani Ulaya ni "uvamizi uliopangwa", na sio suala la bahati mbaya. Kiongozi huyo anayefahamika kwa misimamo yake mikali dhidi ya wahamiaji, amewataka vijana wa kiume nchini Syria na Iraq kukamata silaha kupambana na kundi lijiitalo Dola la Kiislamu, IS, badala ya kukimbilia Ulaya. Katika ujumbe wake wa Krismasi uliotolewa jana, Rais Zeman alisema "inawezekana" kuwahurumia wakimbizi wazee, wagonjwa, na watoto, lakini sio vijana wa kiume, kwani kukimbia kwao kunalipa nguvu kundi la IS. Hata hivyo, ujumbe huo wa Rais Zeman ulikanushwa na Waziri Mkuu
Bohuslav Sobotka akisema umejikita kwenye dharau na tabia ya kuyachukulia mambo kijuujuu. Utafiti wa hivi karibuni unaonesha kuwa asilimia 70 ya raia wa Czech, ambayo ni mwanachama wa Umoja wa Ulaya,  wanapinga uingiaji wahamiaji na wakimbizi kwenye nchi yao.

IS yatishia kuishambulia Israel kwa mara ya kwanza

Umoja wa Mataifa waitisha mazungumzo ya amani ya Syria

Liverpool wazima Leicester, Man Utd walala

Liverpool

Image copyrightPA
Image captionLiverpool walifungiwa na nguvu mpya Christian Benteke
Liverpool wamepunguza kasi ya Leicester kileleni mwa Ligi ya Uingereza baada ya kuwalaza 1-0 uwanjani Anfield.
Leicester walikuwa wameenda mechi tisa bila kushindwa ligini na leo imekuwa mara yao ya kwanza kumaliza bila kufunga bao ligini msimu huu.
Uwanjani Britannia, masaibu ya meneja Louis Van Gaal yamezidi baada ya Red Devils kucharazwa 2-0 na Stoke City. Meneja huyo amekabiliwa na shinikizo baada ya klabu hiyo kuandikisha msururu wa matokeo mabaya.

Janet Jackson aahirisha ziara ya kimuziki

Janet
Image copyrightAP
Image captionUnbreakable ni albamu ya 11 ya Janet Jackson
Mwanamuziki nyota kutoka Marekani Janet Jackson ameahirisha ziara yake ya kimuziki ya Unbreakable ili kufanyiwa upasuaji.

Wakuu wakamatwa kwa sababu ya rushwa Serbia

Serbia

Image copyrightReuters
Image captionWaziri Mkuu wa Serbia Aleksandar Vucic (kulia) ameanzisha mazungumzo kuhusu kujiunga na EU
Polisi nchini Serbia wamewakamata watu 79, akiwemo waziri wa zamani kwa tuhuma za ufisadi.

Mwanahabari wa Ufaransa ‘afukuzwa’ Uchina

Gauthier

Image copyrightAP
Image captionGauthier atatakiwa kuondoka Uchina ifikapo 31 Desemba asipopata kibali kipya
Mwanahabari wa Ufaransa amezuiwa kuendelea kufanya kazi nchini Uchina wiki chache baada yake kuandika makala akikosoa sera za taifa hilo kuhusu watu wa jamii ya Uighers eneo la Xinjiang.

Wanajeshi wa Iraq wapiga hatua dhidi ya IS

Ramadi

Image copyrightAP
Image captionOperesheni ya kuukomboa mji wa Ramadi ilianza Jumanne
Wanajeshi wa Iraq wamepiga hatua kwenye operesheni yao dhidi ya wapiganaji wa Islamic State mjini Ramadi.

Waasi wachelewa kuondoka kambi Syria

Yarmouk
Image copyrightGetty
Image captionEneo la Yarmouk limeshuhudia mapigano makali
Maelfu ya waasi ambao walitarajiwa kusaidiwa kuondoka kutoka kambi ya wakimbizi ya Yarmouk na maeneo ya karibu hawakuondoka kama ilivyotarajiwa, ripoti zinasema.
Mpango huo umekawishwa kutokana na hofu za kiusalama na mauaji ya kiongozi wa kundi moja la waasi jana.
Wapiganaji hao na familia zao walikuwa wamepangiwa kusafirishwa kutoka kambi hiyo kusini mwa Damascus hadi maeneo yanayodhibitiwa na makundi yao, chini ya mkataba kati ya serikali na waasi.

Tetemeko la ardhi lakumba Afghanistan

Peshawar
Image copyrightEPA
Image captionWatu 17 wamejeruhiwa mjini Peshawar, Pakistan
Tetemeko la ardhi lenye nguvu ya 6.3 limekumba maeneo ya kaskazini mwa Afghanistan, na kuathiri maeneo ya mbali hadi India.
Kwa mujibu wa Idara ya Utafiti wa Jiolojia ya Marekani kitovu cha tetemeko hilo kilikuwa mkoa wa Badakhshan, karibu na mpaka wa Pakistan na Tajik.
Haijabainika iwapo kulikuwa na majeruhi eneo hilo, lakini watu 17 walijeruhiwa katika mji wa Peshawar, nchini Pakistan.
Mamia ya watu waliuawa eneo lilo hilo 26 Oktoba baada ya tetemeko jingine la ardhi kutokea.

mkazi wa mtaa wa Bugweto kata ya Ibadakuli katika manispaa ya Shinyanga akiwa eneo la tukio baada ya pikipiki aliyokuwa anaendesha kugongana uso kwa uso na gari

 Jafari Ramadhani(20) mkazi wa mtaa wa Bugweto kata ya Ibadakuli katika manispaa ya Shinyanga akiwa eneo la tukio baada ya pikipiki aliyokuwa anaendesha kugongana uso kwa uso na gari ndogo katika barabara ya Mohammed Trans karibu na shule ya msingi Bugoyi B.Licha ya kugongana na pikipiki hiyo,pia mwendesha baiskeli aliyejulikana kwa jina la Peter Machanga amenusurika kufa baada ya kuruka na kuacha baiskeli ikagongwa na gari hilo.Tukio hilo limetokea leo majira ya saa nne asubuhi.Kwa mujibu wa mashuhuda wanasema chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi wa dereva wa gari pamoja ubovu wa barabara hiyo ambayo ina mashimo mengi-Picha zote na Marco Maduhu-Malunde1 blog

FAMILIA MBALI MBALI ZIMESHEREHEKEA SIKU KUU YA CHRISTMAS ILIVYOKUWA KWA WAKAZI WA JIJI LA DAR ES SALAAM,



KAMPUNI YA AGECO ENERGY & CONSTRUCTION LTD YAFUNGA MWAKA KWA KUFUNGA MTAMBO MKUBWA WA SOLA HOSPITALI YA MKOA SINGIDA.

FUNGA MWAKA CONCERT NA DIAMOND NDANI YA DAR LIVE... ACHA KABISA!FUNGA MWAKA CONCERT NA DIAMOND NDANI YA DAR LIVE... ACHA KABISA!

BONDIA THOMASI MASHALI AMKALISHA FRANSIC CHEKA MOROGORO

WAZIRI NAPE NNAUYE AWATAKA WATANZANIA KUENDELEA KUMUOMBEA RAIS DK JOHN POMBE MAGUFULI, KAZI YA KUTUMBUA MAJIPU NI NGUMU NA INA VIKWAZO VINGI

WAZIRI MKUU KESHO KUANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI KIGOMA

WANAKIJIJI WA KIJIJI CHA ENGUSEROSAMBU WAFURAHIA MSITU KUREJESHWA MIKONONI MWAO.


Ilikuwa ni siku ya shangwe na furaha kwa wananchi wa kata ya Enguserosambu wilayani Ngorongoro. Hii ni baada ya serikali kukubali ombi lao la kusimamia rasilimali ya msitu wa Loliondo namba 2 unaopakana na vijiji vinne vinavyokadiriwa kuwa na idadi ya wakazi wapatao 20,000 wanaotegemea mahitaji yao toka katika huo msitu.

Huu ni msitu pekee ambao wananchi kwa kushirikiana na Mkuu wao wa wilaya, na mashirika rafiki, wamefanikiwa kuishawishi serikali kuukabidhi msitu huo kwao. Katika mchakato huo uliochukua miaka kadhaa wanawake toka katika vijiji vya Enguserosambu, Ng’arua, Orkiu na Naan wamekuwa mstari wa mbele katika kufanikisha azma hiyo ya kubakiza msitu wao wa enzi mikononi mwao. Akielezea furaha yake aliposikia msitu wa Loliondo namba 2 umekabidhiwa kwa wananchi, mraghbishi mwanamke Noorkiyengop Mbaima alisema 

MKESHA WA KRISMAS HOSPITALI YA MUHIMBILI WATOTO 12 WAZALIWA

MHE. RIDHIWAN KIKWETE AVUNJA UKIMYA, AZUNGUMZIA KUHUSU MAKONTENA NA MALI ANAZODAIWA KUMILIKI...

VODACOM TANZANIA YAENDELEZA UTOAJI WA ELIMU KWA MADEREVA NA ABIRIA HAPA NCHINI

Friday, December 25, 2015

RAIS MAGUFULI AUNGANA NA WAKRISTO KUADHIMISHA SIKUKUU YA KRISMASI

Faksi: 255-22-2113425



 







ASKOFU DR MDEGELLA ATAKA WATANZANIA KUMWOMBEA RAIS DR MAGUFULI KWA KAZI NZURI

RAIS MAGUFULI ASHIRIKI MISA YA KRISMASI KANISA LA MTAKATIFU PETER JIJINI DAR ES SALAAM LEO

RAIS DKT. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI KIMBILIO LA WATANZANIA - WAZEE WANENA ZANZIBAR

GO FOR ZANZIBAR (GOZA) A GERMAN NGO SUPPORTS THE WELEZO OLD AGE HOME

WANAKIJIJI WACHARUKA WAMTAKA MKURUGENZI MBOGWE AKAZOE TAKA ZILIZOTUPWA KIJIJINI KWAO SIKU YA USAFI DECEMBER 9

UCHAFU ULIOZOLEWA KATIKA KATA YA MASUMBWE NA KUTUPWA KATIKA MAKAZI YA WATU KATIKA KIJIJI CHA SHENDA.Wanachi wa kijiji cha Shenda katika kata ya Masumbwe wilayani Mbogwe mkoani Geita Wameitaka ofisi ya mkurugenzi wa halmashauri ya Mbogwe kuziondoa takataka zilizowekwa kijijini kwao kufuatia zoezi la usafi la December 9 Lililofanyika nchi nzima.Wakiongea na waandishi wa habari za mtandaoni wananchi hao wanakijiji hao wamesema kuwa wanashangazwa na kitendo cha halmashauri ya wilaya kutuma takataka katika kijiji chao licha ya kwamba hakuna dampo la uchafu eneo hilo.Wameongeza kuwa taka hizo ni hatari kwa afya zao kwani zimetupwa karibu na eneo la shule ya msingi,Makazi ya watu na vibanda vya mama ntilie hali inayozua hofu ya kuzuka kwa magonjwa ya mripuko kwani taka hizo zimeanza kuoza na kusambaa katika makazi ya watu kipindi hiki cha masika.Sambamba na hayo wameshangazwa na maamuzi ya ofisi ya mkurugenzi kutupa taka hizo katika kijiji chao licha ya kuwa yapo maeneo mengi ya wazi ambayo yangeweza kutumika kutupa taka hizo ambazo kwa sasa zimekuwa kero katika kijiji chao hasa kutoa harufu mbaya na funza.Kwa mujibu wa kaimu mtendaji wa kijiji cha Shenda Joseph Jaseda amesema sehemu zilizotupwa taka hizo ni makazi ya watu na kwamba walipouliza kuhusu hatua hiyo waliambiwa kuwa gari la kuzoa taka liliharibika sehemu hiyo na ndipo walipoamua kutupa taka hizo.Kwa upande wake diwani wa kata ya Masumbwe Shimo Kiyuyu amesema kuwa alifikisha malalamiko ya wananchi kwa mkurugenzi na Mkurugenzi akatoa gari ili uchafu uzolewe lakini juhudi hizo ziligonga mwamba kutokana na gari hiyo kwenda eneo la uchafu bila wazoaji wa taka hizo.Kwa upande wake afisa afya wa halmashauri ya wilaya ya MbogweEdward Razalo amekiri uchafu huo kutupwa katika maeneo hayo na kuongeza kuwa baada ya wananchi kulalamika walienda kuweka dawa ya kuwa wadudu katika taka hizo na kwamba hawajaziamisha kutokana na taka hizo kutokuwa na madhara kwa wananchi.

MKUU WA WILAYA YA IRINGA RICHARD KASESELA AFUNGUA MAFUNZO YA ULENGAJI SHABAHA

WATANZANIA WAASWA KUENDELEZA AMANI ILIYOPO

MUUAJI WA AFISA WA INTELIJENSIA WA TANAPA AKAMATWA

REBECCA MALOPE KUWASHA MOTO TAMASHA LA XMASS DIAMOND JUBILEE LEO

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AHUDHURIA SHREHE ZA MAULID ZANZIBAR