TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, December 23, 2015

MILIONI 200 KUWAWEZESHA WAJASIRIAMALI KIUCHUMI, NI MKOPO NAFUU KUTOKA TPB

Bw. Moshingi akisalimiana na wana VICOBA


NA K-VIS MEDIA/Khalfan Said


BENKI ya Posta Tanzania, TPB, imekabidhimkopo wa jumla ya shilingi milioni 244,500,000/- kwa vikundi vinane vya wajasiriamali.

Makabidhiano hayo yamefanyika leo Desemba 23, 2015 kwenye hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Fedha na Mipango jijini Dar es Salaam, ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, (NEEC).

Akizungumza kwenye makabidhiano hayo, Afisa Mtendaji Mkuu wa TPB, Bw. Sabasaba Moshingi alisema, fedha hizo ni awamu ya kwanza ya benki kutoa mikopo hiyo yenye masharti nafuu, baada ya kutiliana saini na NEEC Julai mwaka huu wa 2015, ambapo baraza hilo litadhamini vikundi hivyo ambavyo vitapaswa kwanza kufungua akaunti TPB kabla ya kupatiwa mikopo hiyo ambayo jumla ya shilingi bilioni 2 zimetengwa kwa dhumuni hilo.
“Ninayo furaha kubwa kuwakabidhi nyinyi wajasiriamali ili muweze kutimiza ndoto zenu za kujikwamua kiuchumi.” Alisema Bw. Moshingi na kuhimiza vikundi zaidi vya wajasiriamali kujiunga na benki hiyo ili navyo vifaidi kwa wanachama wake kujiongezea mitaji kwa ajili ya shughuli zao za kiuchumi.Akizungumza kwenye hafla hiyo, mgeni rasmi ambaye ni Kaimu Katibu Mtendaji wa NEEC, Bi. Anna Dominic, alisema, baada ya NEEC kuona takwimu zinaonyesha kuwa hapa nchini ukosefu wa ajira ni moja ya changamoto kubwa kabisa na hivyo inahimiza wananchi kujiunga kwenye vikundi ili NEEC kwa kushirikiana na taasisi nyingine kama TPB, kuweza kuwapatia mikopo kwa ajili ya kufanya shughuli za kiuchumi.“Ningependa kuwaasa wajasiriamali mliopokea mikopo hiyo, kufanya kazi kwa bidii kama ulivyo msimamo wa serikali ya awamu ya tano chini ya Mh. Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya “Hapa Kazi Tu”.” Alisema na kuwahimiza kutumia vizuri mikopo hiyo kwa shughuli zilizokusudiwa ili waweze kurejesha tena kwa wakati.Akitoa shukrani zake baada ya kupokea mkopo huo kwa niaba ya wenzake, Mkurugenzi wa Shirika la Vijana Wajasiriamali na Uwezeshaji Tanzania, (TYEEO), Bw. Ayub Gerald Luhuga, aliishukuru TPB kwa kuwaunga mkono katika kuhakikisha wajasiriamali wanakuza mitaji yao ili kujikwamua kiuchumi, na kuahidi kuwa mikopo hiyo itatumika kama ilivyokusudiwa na kurejeshwa kwa wakati. Bi. Anna akitoa hotuba yake Mkurugenzi wa Idara ya Mikopo ya TPB, Bw.Henry Bwogi, (kulia), Mkurugenzi wa Masoko wa TPB, Bw.Deogratius Kwiyukwa, (katikati), na Meneja Mikopo ya Vikundi ya TPB, Bw.Ramadhan Liganga, wakibadilishana mawazo Bw.Moshingi, (kushoto), akimsikiliza Bw. Kwiyukwa, huku Afisa Habari Mwandamizi wa TPB, Bw.Theo Mwakifulefula akisikilzia Mmoja wa wajasiriamali akipiga makofi kufurahia jambo. Mkurugenzi wa Idara ya Mikopo ya TPB, Bw.Henry Bwogi,(kushoto) na Mkurugenzi wa Masoko wa TPB, Bw.Deogratius Kwiyukwa, (katikati), wakimsikiliza mkurugenzi wa TYEEO, Bw. Ayubu Bw. Ayubu akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wajasiriamali wenzake Picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment