TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, December 26, 2015

Youla ateuliwa waziri mkuu mpya wa Guinea

Rais Alpha Conde wa Guinea amemteua waziri mkuu mpya, baada ya kuapishwa mapema wiki hii kwa muhula mpya wa miaka mitano wenye utata. Mamady Youla, mchumi ambaye amefanya kazi serikalini na kwenye sekta binafsi, anachukuwa nafasi ya Mohamed Said Fofana, aliyejiuzulu Jumatano iliyopita. Youla, mwenye umri wa miaka 54, amepewa jukumu la kuunda serikali itakayojikita kwenye uundaji wa nafasi mpya za ajira, kuinua maisha ya vijana na kuuimarisha uchumi wa taifa hilo la kipato cha chini. Conde, mwenye umri wa miaka 77, alichaguliwa kwenye uchaguzi wenye utata hapo mwezi Oktoba na akaapishwa Jumatatu iliyopita. Mwezi uliopita, mahakama ya katiba ilitupilia mbali madai ya wapinzani kwamba ushindi wa asilimia 57.8 wa kiongozi huyo ulikuwa wa wizi.

No comments:

Post a Comment