TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, December 26, 2015

Wanajeshi wa Iraq wapiga hatua dhidi ya IS

Ramadi

Image copyrightAP
Image captionOperesheni ya kuukomboa mji wa Ramadi ilianza Jumanne
Wanajeshi wa Iraq wamepiga hatua kwenye operesheni yao dhidi ya wapiganaji wa Islamic State mjini Ramadi.

Kasi yao imepunguzwa na mabomu yaliyotegwa katika mji huo, maafisa wa jeshi wanasema.
Wanajeshi hao ambao wanasaidiana na wapiganaji wa Kisuni wamo mita 500 kutoka afisi kuu ya baraza la mji.
Wamefanikiwa kukomboa mitaa kadha ya mji tangu kuanza kwa operesheni hiyo siku tano zilizopita.
Mji huo wenye Wasuni wengi umo kilomita 90 magharibi mwa Baghdad na ulitekwa na wapiganaji wa IS mwezi Mei.
Kutekwa kwa mji huo kuliaibisha sana jeshi la Iraq.
Wakati wa kuzinduliwa kwa operesheni Jumanne, jeshi la Iraq lilisema lilitarajia wapiganaji takriban 300 walio mjini humo wafurushwe katika kipindi cha siku kadha.
Lakini sasa kuna wasiwasi kwamba huenda wapiganaji hao wanashikilia mateka raia.
Wapiganaji wa IS wamepokonywa miji mingi waliyokuwa wameiteka nchini Iraq, huku wakiendelea kukabiliwa vikali na wanajeshi wa Iraq na wapiganaji wa Kikurdi.

No comments:

Post a Comment