TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, November 1, 2014

Nchi inaposhindwa kufuata misingi ya Haki na DEMOKRASIA: Burkina Faso wananchi wamepindua serikali ya miaka 27 katika maandamano makubwa ya siku moja tu.

 Wananchi wakiwa kwenye Maandamano hayo
 Mkuu wa Majeshi wa Nchi hiyo
 Vikosi vya Majeshi ya Ulinzi na Usalama yakihakikisha hali inakuwa Tulivu.

CCM YAVUNA MAVUNO YAKE KUTOKA CHADEMA NGORONGORO

imagesNa Gladness Mushi, Ngorongoro

CHAMA cha Mapinduzi, CCM, kimezidi kujiimarisha baada ya kukisambaratisha Chama cha Chadema wilayani Ngorongoro, kufuatia hatua ya mwenyekiti wake ,Revocatus Parapara,na viongozi wa kata na matawi kubwaga manyanga na kujiunga CCM.
Tukio hilo limetokea jana kwenye mkutano wa hadhara wa Chama cha Mapinduzi, uliokuwa ukihutubiwa na Katibu wa CCM, mkoa, Alphonce Kinamhala,aliyekuwa kwenye ziara ya kujitambulisha kwa wananchi uliofanyika  kijiji cha Waso wilayani Ngorongoro, na viongozi hao kujiunga rasmi na Chama cha mapinduzi.

Akihutubia mkutano huo , Katibu wa CCM, Kinamhala, amewataka madiwani wasijiingize kwenye uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa na badala yake wawaache wananchi wachague viongozi wawatakao .
Amewataka madiwani  kutokujiingiza kwenye Zabuni mbalimbali za serikali kazi zao ni kusimamia wakandarasi  ili kuhakikisha miradi yote inayotekelezwa kwenye vijiji na kata inatekelezwa kwa kiwango kinachotakiwa. Amesema  hasara ni kubwa iwapo wao watajiingiza kwenye Zabuni watashindwa kusimamia utekelezaji wa miradi hiyo na mradi usipotekelezwa kwa kiwango na muda wake serikali na Chamna cha mapinduzi ndio watakaonyoshewa vidole na kulaumiwa na wao watashindwa kutetea na huko ni kukiuka majukumu yao.

 .Kuhusu mchakato wa KATIBA, Katibu Kinamhala, amewaambia wananchi wasikubali kudanganywa kwamba mchakato huo uliporwa na CCM, Katiba hiyo sio ya Chama cha Mapinduzi, bali ni ya wananchi na ndio maana imepitishwa kwenye bunge la katiba maalum, Na CCM, haijawa
Awali katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi, CCM, mkoa wa Arusha, Joseph Izack  ,amewataka wanaotaka kuvuruga  amani ya nchi hii kwa kisingizio cha siasa kuacha mara moja  vinginevyo watashughulikiwa kokote pale walipo.

Ameongeza kuwa  katiba inatoa fursa kwa wanawake kugombea uongozi ngazi mbalimbali ambapo sasa wanayo nafasi ya 50 kwa 50 kila nafasi ya uongozi na haya ni mafanikio makubwa .

MFUKO WA WANAFUNZI WALIOHITIMU SHULE KONGWE ILBORU WATARAJIA KUTUMIA ZAIDI YA MILIONI 20 KUKARABATI MAJENGO

New Picture
 Na Gladness Mushi,Arusha

MFUKO wa wanafunzi waliohitimu zamani katika shule kongwe ya vipaji maalum ya  Ilboru(Ilboru Alumni Foundation)wanatarajia kutumia kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 20 hadi ifikapo  desemba mwaka huu kwa ajili ya kukarabati majengo  ya shule hiyo ili kuweza kuirejesha katika mazingira mazuri .
Aidha kwa sasa shule hiyo pamoja na kuwa ni ya vipaji maaluma lakini mazingira yake hayako katika hali nzuri hali ambayo iliwafanya wanafunzi hao waliomaliza miaka ya nyuma kuungana ili kuikarabati na kuirejeshea mzingira yake ya miaka ya nyuma kwa lkuwa mazingira mabaya yanachangia kufelisha wanafunzi.
Hayo yalisemwa na mtendaji mkuu katika mfuko huo ambaye ni dr Daniel Maro alipokuwa akikabidhi rasmi funguo za darasa moja lililomalizika kukarabatiwa katika mahafali ya 25 ya kidato cha nne ya shule hiyo ambapo darasa hilo limegharimu kiasi cha  zaidi ya milioni 4 .
Dr Maro alisema kuwa shule hiyo imekuwa ikizalisha wataalamu mbali mbali sana lakini bado ina changamoto nyingi ambazo zinawahitaji wadau wa elimu kuziunga mkono ili kuhakikisha kuwa watoto wanasomea katika mazingira mazuri.
“sisi tumeungana kwa pamoja tuliosoma kwa kipindi cha kuanzia 1999 katika kuhakikisha kuwa tunarejesha mzingira ya nyuma kwani mazingira ya sasa nay a kipindi tulichokuwa tunasoma yalikuwa ni tofauti sana na mzingira mabaya yanasababisha hata watoto kutosoma vizuri”aliongeza dr Maro.
Alifafanua kuwa hadi sasa wameshafanikiwa kukarabati darasa moja na wana mpango wa kuendelea na madarasa mengine manne ambayo kila moja litagharimu zaidi ya milioni nne ambapo wanatarajia hadi ifikapo desemba wawe wameshakamilisha mchakato wa kukarabato majengo hayo ambayo yamekuwa chakavu mno.
Aidha dr Maro alisema kuwa mara baada ya kumaliza kukarabati majengo hayo bado wataendelea kutatua changamoto nyinginzo zinazoikabili shule hiyo huku akiwataka wale wote waliomaliza katika shule

KULUVYA UNITED YAIFUNGA SINZA STAR 3-0 NA KUTINGA ROBO FAINALI YA MICHUANO YA DK. MWAKA SPORTS EXTRA NDONDO CUP 2014

 Kikosi cha Kiluvya United kikiwa katika picha ya pamoja.
Kikosi kamili cha timu ya Snza Star kikiwa katika picha ya pamoja.
Beki wa tmu ya Kiluvya United, Mwita Enoshi (kushoto) akiwania mpira na mshambuliaji wa Sinza Stars katika mchezo wa Ligi ya Dk. Mwaka Sports Extra Ndondo Cup 2014 uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Makurumla Dar es Salaam. Kiluvya ilishinda 3-0 na kutinga hatua ya robo fainali ya mchuano hiyo.
Mshambuliaji wa timu ya Kiluvya United, Haji Zege (kushoto) akichuana na beki wa Sinza Stars Charles Kaembe katika mchezo wa Ligi ya Dk. Mwaka Sports Extra Ndondo Cup 2014 uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Makurumla Dar es Salaam. Kiluvya ilishinda 3-0 na kutinga hatua ya robo fainali ya mchuano hiyo.
 Kikosi cha Kiluvya United kikifanya mazoezi mepesi kabla ya mechi yao ya Ligi ya Dk. Mwaka Sports Extra Ndondo Cup 2014 katika Uwanja wa Makurumla dhidi ya Sinza Star. Kiluvya United ilishinda 3-0.
  Kikosi cha Kiluvya United kikifanya mazoezi mepesi kabla ya mechi yao na Sinza Star. Kiluvya United ilishinda 3-0.
 Wachezaji wa Sinza Star wakifanya mazoezi mepesi kabla ya kuanza kwa mchezo wao na Kiluvya United.
 Wachezaji wa Kiluvya United wakisalimiana na wachezaji wa Sinza Stara kabla ya mchezo wao wa hatua ya 16 bora ya michuano ya Dk. Mwaka Sports Extra Ndondo Cup 2014 uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Makurumla jijini Dar es Salaam. Kiluvya United ilishinda 3-0 na kuingia hatua ya robo fainali ya michuano hiyo. 
 

Baraza l;a madiwani laitaka REA kukamilisha umeme kwa wakati

indexNa Gladnesss Mushi,Arusha

BARAZA la madiwani wa halmashauri ya Arusha limemtaka wakala wa usambazaji wa umeme vijijini (REA)kuhakikisha kuwa vijiji vyote vilivyoko kwenye mpango wa kupatiwa umeme vinapata kwa wakati kwani kwa sasa mashimo yalichimbwa yanahatarisha maisha ya wananchi.
Mbali na baraza hilo kuwataka REA kufikisha umeme kwa wakati vijijini lakini pia wanatakiwa kuifanya jamii iweze kuwakubali tofauti na sasa ambapo wamechimba mashimo ya kusimamamishia nguzo na wameyaaacha.
Akiongea na katika baraza hilo la madiwani lililofanyika jana mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Saimon Saningo alisema  kuwa ni muda mrefu sasa umepita toka wakala hao wachimbe mashimo na kuyaacha kama yalivyo jambo ambalo limewafanya wananchi kubaki na malalamiko.
Amedai kuwa,mashimo hayo yanahatarisha sana maisha ya wananchi lakini pia hata mifugo ambayo ipo vijijini humo na kwa hali hiyo wananchi wamebaki wakiwa na manunguniko makubwa. Ameongeza kuwa endapo kama muda wa kufikisha umeme vijijini haujafika basi REA wanatakiwa kwenda kufukia mashimo hayo na pindi watakapokuwa tayari basi watayafukua na kisha kusimamisha nguzo kwa ajili ya umeme.
Hataivyo ameitaka  REA kuhakikisha kuwa wanashirikiana na madiwani waliopo kwenye kata husika kwani takwimu za halmashauri hiyo zinaonesha kuwa bado asilimia kubwa ya madiwani hawajui mradi huo
Amesema  kuwa wakati mwingine wananchi wanashindwa kupenda na kuthamini mradi huo kwa kuwa hawana hamasa kutoka kwa madiwani hao hali ambayo wakati mwingine inasababisha fujo zisizo za lazima hasa maeneo ambayo mradi huo umepita.

NHC watathmini utekelezaji wa ujenzi wa miradi

Meneja wa NHC Mkoa wa Tabora, Erasto Chilambo akiwasilisha ripoti ya utekelezaji wa mradi wa nyumba za gharama nafuu za NHC Isikizya zilizopo wilayani Uyui mkoani Tabora kwenye semina ya mameneja na wakurugenzi wa NHC inayoendelea katika Hoteli ya Tanga Beach Resort.
Meneja wa NHC Mkoa wa Dodoma, Itandula Gambalagi akiwasilisha ripoti ya utekelezaji wa mradi wa nyumba za gharama nafuu za NHC Mnyakongo, Kongwa Dodoma kwenye semina ya mameneja na wakurugenzi wa NHC inayoendelea katika Hoteli ya Tanga Beach Resort.
 Washiriki wa Semina hiyo Wenceslaus Tillya, Meneja wa NHC mkoa wa Temeke, Nehemia Msigwa, Meneja wa NHC Katavi na Daniel Nkya wakifuatilia kwa kina somo lililokuwa likitolewa na Wataalamu Washauri wa Delloite Touche juu ya mapitio ya Mpango Mkakati wa Shirika unaomalizika mwakani, ili kuuboresha kwa kipindi kijacho. Somo hilo lilitolewa kabla ya mawasilisho ya mameneja wa mikoa.
Meneja Mshauri Taasisi inayojishughulisha na mambo ya uchumi ya Deloitte Bw.Frederick Nsemwa, Mkurugenzi wa Watushi Housing Limited, Dk Fred Nsemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu wakifuatilia somo hilo
Wataalamu washauri wa semina hiyo  wakiwa pamoja na Mkurugenzi wa Rasilimaliwatu, James Rhombo na Mkurugenzi wa Uendelezaji Miliki Benedict Kilimba wakifuatilia semina hiyo.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Jamii Susan Omari akifuatilia kwa kina soma hilo la Delloite Touche.
Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani, Fatuma Chillo akisisitiza jambo katika semina hiyo huku Mkurugenzi wa Fedha, Felix Maagi na Mkurugenzi wa Uendelezaji Biashara, David Shambwe wakifuatilia.
Julius Ntoga wa Shirika la Nyumba la Taifa, William Genya, Joseph Mwanasenga, Ramadhani Macha, Elias Msese, Pauline Mrango , Hamad Abdallah na Ladislaus Bamanyisa wakifuatilia kwa kina somo lililokuwa likitolewa na Wataalamu Washauri wa Delloite Touche.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akisisitiza jambo katika semina hiyo.
Humphrey Kishimbo, Meneja wa NHC, Iringa, George Magembe, Meneja Miradi wa NHC na Mektilda Mihayo, Meneja wa Mahusiano kwa Wateja wakifuatilia somo katika semina hiyo.
 Washiriki wakifuatilia mada iliyotolewa na Wataalamu wa Afrika Kusini kutoka kampuni ya Hydraform.
 Wataalamu wa Afrika Kusini kutoka kampuni ya Hydraform.wakiwa na mdau kutoka Hydraform Tanzania wakifuatilia semina hiyo

MABONDIA WAZIPIGA MAZOEZINI

Bondia Shabani Kaoneka kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Obago Kamata wakati wa mazoezi .
Bondia Shabani Kaoneka kulia 
akimtupia konde  Obago Kamata wakati wa mazoezi .
Bondia Shabani Kaoneka kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Obago Kamata wakati wa mazoezi.
Bondia Jumaa Rashid akioneshana ubavu na Juma Biglee wakati wa mazoezi yaliyofanyika katika uwanja wa Shule ya Uhuru uwanja wa basket  Dar es salaam jana.
Bondia Omari Bai kushoto akipambana ya Kelvin Majiba wakati wa mazoezi yaliyofanyika katika uwanja wa basket Shule ya Uhuru  Dar es salaam jana.
Bondia Shabani Kaoneka akipambana na Omari Bai wakati wa mazoezi .
Bodia Obaga Kamata kushoto akipambana na Idrisa Mweta wakati wa mazoezi .

President Kikwete meets Cyril Ramaphosa at State House

D92A2326President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete in conversation with South Africa’s Deputy President Cyril Ramaphosa at State House Dar es Salaam when the later paid him a courtesy call yesterday evening(photos by Freddy Maro) D92A2352 D92A2382

HOTUBA YA WAZIRI WA UCHUKUZI Mhe. Dkt. Harrsion Mwakyembe KATIKA MKUTANO WA SITA WA MAMENEJA WA MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE TANZANIA ULIOFANYIKA HOTEL YA DOUBLE TREE DAR ES SALAAM

DSC_5248
Awali ya yote napenda nichukue fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kujumuika pamoja leo hii katika tukio hili muhimu linalohusu mkutano mkuu wa sita wa mameneja wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA). Aidha nichukue nafasi hii pia kuipongeza Menejimeti ya TAA pamoja na wafanyakazi wote kwa kufanikisha maandalizi ya mkutano huu na kunipa heshima hii kubwa ya kuwa mgeni rasmi katika ufungaji wa mkutano huu. Kwa hili nawashukuru na kuwapongeza sana.
Ndugu Wajumbe, Pamoja na shukrani zangu za awali, nimefarijika sana kuona Mkutano huu unawajumuisha Viongozi wa Menejimenti na Mameneja wote wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini kote wapatao sitini (60) kama Mkurugenzi Mkuu alivyoeleza katika hotuba yake. Katika mkusanyiko huu, ni matarajio yangu kwamba Mkutano huu ulikuwa ni fursa nzuri ya kubadilishana mawazo kwa ukaribu zaidi na kutafuta ufumbuzi wa matatizo na changamoto zinazohusiana na shughuli za utoaji huduma katika Mamlaka yenu. Aidha, hii ni njia mojawapo ya ushirikishwaji na uwajibikaji katika uendeshaji wa Taasisi hii. Sambamba na pongezi zangu za awali, nichukue fursa hii pia kwa kuwapongeza tena juu ya kauli mbiu ya mkutano mliyoichagua ambayo inaendana na mabadiliko ya huduma za makampuni yaliyoanza kutoa huduma za usafiri wa anga kwa gharama nafuu ambayo yatakuwa chachu ya ukuaji wa sekta ya Anga Tanzania. Ukuaji wa “low cost carriers” kwa sasa na kwa siku zijazo ni wa uhakika, hivyo nawaasa kuwa TAA kama mdau mkuu katika ukuaji huo, ihakikishe kwamba inajipanga vizuri kwa kuweka mazingira yanayowezesha kukabiliana na changamoto zitakazotokana na ukuaji huo.
Bila shaka na kama nilivyoarifiwa, mada mbalimbali zilizoandaliwa zilijadiliwa kwa kina na ufasaha kutokana na kwamba zote zilijikitika katika kufanikisha lengo la mkutano huu, ambazo zimeainishwa vizuri katika kauli mbiu yake.
Ndugu Wajumbe, Wizara tunajivumia sana mafanikio ambayo TAA imeyapata tangu kuanzishwa kwake, ni dhahiri kwamba mafanikio hayo si tu kwamba yatatokana na mipango mizuri mliyojiwekea bali pia yanatokana na usimamizi wenu wa karibu juu ya malengo hayo kwa kuwashirikisha kwa karibu wafanyakazi walioko chini yenu. Dunia ya sasa ya karne ya 21 katika viwanja vya ndege, inatawaliwa zaidi na utoaji huduma ulio bora ukilenga kuwavutia wateja na hili linaweza tu kufikiwa iwapo wafanyazi watahamasishwa na kupewa mafunzo ambayo yatawaongezea ujuzi ukiwemo wa kiteknolojia, weledi na hamasa ya kufanya kazi kwa bidii zaidi. Na ili ushirikishwaji huo utoe matunda yanayostahili, mnaaswa mhakikishe kwamba wafanyakazi hao wanahamasishwa na kupewa mafunzo stahiki na hasa katika kusimamia miradi ya maendeleo ambayo inatekelezwa sasa katika viwanja vyenu, inayokuja na inayotarajiwa.
Sanjari na hili mnaaswa pia mhakikishe kuwa ili kujua na kupima utendaji wao wa kazi, watumishi hao wapimwe juu ya utendaji wao wa kazi wa kila siku kwa kutumia mfumo ulio wazi wa kupima utendaji wa kazi wa watumishi wa serikali yaani OPRAS. Nimefahamishwa kuwa upimaji wa utendaji kazi chini ya OPRS umekuwa na changamoto nyingi. Hata hivyo, siamini kama changamoto hizo hazitatuliki, hivyo kwa weledi mlio nao, naomba muendelee kuboresha mfumo huo kwa lengo la upimaji bora wa watumishi hatimaye ulete matunda ya pamoja kwa utendaji ulio bora kwa Mamlaka.

Friday, October 31, 2014

BEN KIKO AMEFARIKI DUNIA

Mtangazaji wa zamani wa Radio Tanzania Dar es salaam(RTD) ambayo sasa ni TBC Taifa, Ben Hamis Kikoromo au maarufu Ben Kiko (pichani) amefariki duania.

Mwandishi huyo mkongwe nchini Ben Kiko amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hosptali ya taifa ya rufaa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.
Ben Kiko alihamishiwa katika hosptali ya Muhimbili kutokea hosptali ya Jeshi ya Milambo ya mkoani Tabora ambako alilazwa kwa ajili ya matibabu ya figo kwa muda wa wiki mbili.
Atakumbukwa kama mmoja wa watangazaji mahiri ambao walijipatia umaarufu mkubwa ambapo katika enzi za uhai wake alifanya makubwa wakati wa Vita vya Kagera kwa kuleta matukio mbalimbali kutoka uwanja wa vita. Pia aliupaisha sana mkoa wa Tabora alikokuwa akifanyia kazi kwa habari na visa mbalimbali katika kipindi cha RTD cha Majira.

MUNGU ILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALA PEMA, AMIN

Halmashauri zashauri kutenga maeneo ya uwekezaji.

unnamed
Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stela Manyanya akikagua bidhaa za wajasiliamali na waoneshashi kwenye viwanja vya maonesho ya SIDO yaliyojumuisha mikoa mitano ya Njombe,Mbeya,Rukwa ,Katavi na Kigoma sanjali na kongamano la uwekezaji kwa mikoa ya ukanda wa ziwa Tanganyika ambayo,Katavi Rukwa na Kigoma yanayoendelea kwenye uwanja wa Nelson Mandela Mjini Sumbawanga Mkoani Rukwa
……………………………………………………………..
Na Kibada Kibada –Rukwa. Halmashauri za Wilaya zimeshauriwa kutenga maeneo ya uzalishaji na kuendeleza maeneo maalum kwenye baadhi ya mipaka ili kuweza kupata sehemu bora za kuuzia bidhaa za wananchi zinazozalishwa katika maeneo hayo. Ushauri huo ulitolewa na waziri wa Viwanda na Biashara Dkt Abdalah Kigoda katika Hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stela Manyanya wakati wa ufunguzi wa maonesho ya kumi na mbili ya Kanda ya Nyanda za Juu kusini ya wajasiliamali wadogo na kati Mjini Sumbawanga. Dkt Kigoda ameeleza kuwa bidhaa kwenye maeneo maalum na ya pamoja hususani ya mipakani kunasaidia katika kuleta ushindani na uboreshaji wa bidhaa. Akasema serikali itaendelea kuweka mazingira mazuri ya kulitumia soko la AGOA na masoko mengine ambayo Serikali imeridhia ambayo ni Afrika Mashariki AECna lile la kusini mwa Afrika SADC. Akashauri kufanya biashara halali na nchi jirani na kutunza kumbukumbu sahihi ya biashara zinazofanyika nchi za jirani na nchi ya Tanzaznia ili kuweza kuandaa sera mahususi za kuwasaidia. Waziri Kigoda Katika Hotuba yake akasisitiza kwa Halmashauri zote nchini kushiriki moja kwa moja katika Program ya SIDO ya ’Wilaya moja Bidhaa moja’ ambayo inasisitiza kuwa kila wilaya iwe inatambulika kwa uzalishaji wa bidhaa moja itakayotiliwa mkazo zaidi kuliko nyingine zilizopo kwenye wilaya husika. Hii ikiwa na maana kutoa kipaumbele kwenye upande wa kuendeleza bidhaa kwa kuipa huduma zaidi kwenye upande wa kupata mafunzo teknolojia,masoko na mikopo,lengo ikiwa ni kuongeza mapato na ajira kwa vijana katika maeneo husika. Pia Wafanya biashara, wajasiliamali na wasindikaji wa bidhaa wa Mikoa ya Ukanda wa Nyanda za Juu Kusini na ule wa kanda ya ziwa Tanganyika wametakiwa kuwa wabunifu katika kubaini nini kinahitajika na mahali gani na lini wakati wa kuzalisha kadiri ya mahitaji ya soko. Mikoa mitano ya Kanda ya nyanda za juu na ukanda wa ziwa Tanganyika imejaliwa kuwa na rasilimali nyingi na hali ya hewa nzuri inayovutia na kufaa katika kuzalishaa bidhaa na kutoa huduma mbalimbali. Ambapo bidhaa zinazotokana na maliasili,mifugo,na mazao ya kilimo ambayo mikoa yote mitano ya kandahii imejaliwa ambayo ni Njombe Mbeya, Rukwa Katavi na Kigoma ambapo Serikali inajitahidi kuweka miundombinu ili kuwezesha huduma na bidhaa kusafiri kwa urahisi kutoka mikoa hiyo kwenda kwenye mikoa mingine na nchi jirani za Zambia,Jamhuri ya Kidemkrasi ya Kongo DRC,Burundi, Malawi na Rwanda, kwa kutumia barabara na majini Maziwa Tanganyika,Rukwa na Nyasa, Ambapo ili kutumia fursa hiyo wanatakiwa kuwa wabunifu katika kubaini mahitaji.

SERIKALI ITAENDELEA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA KWA WANANCHI-DKT.BILALI

unnamedMakamu wa Rais Dk. Mohamed  Gharib Bilali (watatu kutoka kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau wa Sekta ya afya nchini mara baada ya kufungua Kongamano la wadau  hao leo jijini Dar es salaam.Wengine   kushoto ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Seif Rashid.Picha zote na Frank Mvungi-MAELEZO_Dar es salaam.
unnamed1Makamu wa Rais Dk. Mohemed  Gharib Bilali akiwa kwenye picha ya pamoja  na Waziri wa Afya na ustawi wa Jamii  Dk Seif Rashid leo Jijini Dar es salaam wakati wa Kongamano la wadau  wa  Sekta ya Afya lililofanyika leo Jijini Dar es  salaam.
unnamed2Baadhi ya Wadau wa Kongamano la wadau wa Sekta ya Afya wakiwa wanamsikiliza mgeni  rasmi ambaye ni makamu wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilali (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo leo jijini Dar es salaam.
……………………………………………………….
Na Frank Mvungi-MAELEZO Serikali imesema itaendelea kuboresha huduma za afya hapa nchini kuanzia ngazi ya Zahanati hadi Hosipitali za Rufaa zote nchini ili kuhakikisha wananchi wanapata matatibu bora na yanayoridhisha. Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Makamu wa Rais Dkt. Mohamed Gharib Bilali wakati akifungua Kongamano la wadau wa Afya nchini. Amesema kuwa Serikali inayo dhamira ya dhati katika kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anapata huduma bora za afya ili apate muda mzuri wa kuchangia shughuli nyingine za maendeleo akiwa mzima. Dkt. Bilali ameongeza kuwa Serikali itaendelea kutoa motisha kwa watumishi wa Sekta ya afya ili waendelee kutoa huduma bora za afya kwa wananchi. Kwa upande wake Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid amesema Tanzania ni moja kati ya nchi nne barani Afrika zilizoweza kufikia lengo namba 4 la malengo ya millennia katika utoaji wa huduma bora za afya. Amesema kuwa hatua imefikiwa baada ya Wizara hiyo kuamua kuanzisha idara maalum itakayohusika kuangalia ubora wa huduma zinazotolewa hapa nchini ili kuongeza tija katika Sekta ya Afya kwa kuwapa Wananchi huduma bora zinazokidhi vigezo. Ameongeza kuwa kwa wale wanaofanya vizuri katika kutoa huduma za Afya watatambuliwa kwa mchango wao katika kutoa huduma bora. Dkt. Rashid ametaja vigezo vinavyotumika katika kuwapata watoa huduma za afya kuwa ni kutoa huduma inavyotakiwa,kutumia utaalamu sahihi katika kutoa huduma hiyo na kuzingatia viwango vilivyowekwa katika kutoa huduma za afya. Aidha Dkt. Rashid ametoa wito kwa wananchi kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) ili waweze kunufaika na huduma zinazotolewa kupitia mfuko huo kwa lengo la kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma bora za afya. Kongamano la wadau wa Sekta ya Afya limehusisha wadau zaidi ya 300 kutoka katika Taasisi mbalimbali za Serikali na zisizo za Kiserikali na linafanyika kwa muda wa siku mbili ambapo baadhi ya wadau walitambuliwa kwa kutoa huduma bora za Afya ni kama vile Hosipitali ya Rufaa Mbeya,KCMC, na Bugando.