TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, November 1, 2014

HOTUBA YA WAZIRI WA UCHUKUZI Mhe. Dkt. Harrsion Mwakyembe KATIKA MKUTANO WA SITA WA MAMENEJA WA MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE TANZANIA ULIOFANYIKA HOTEL YA DOUBLE TREE DAR ES SALAAM

DSC_5248
Awali ya yote napenda nichukue fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kujumuika pamoja leo hii katika tukio hili muhimu linalohusu mkutano mkuu wa sita wa mameneja wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA). Aidha nichukue nafasi hii pia kuipongeza Menejimeti ya TAA pamoja na wafanyakazi wote kwa kufanikisha maandalizi ya mkutano huu na kunipa heshima hii kubwa ya kuwa mgeni rasmi katika ufungaji wa mkutano huu. Kwa hili nawashukuru na kuwapongeza sana.
Ndugu Wajumbe, Pamoja na shukrani zangu za awali, nimefarijika sana kuona Mkutano huu unawajumuisha Viongozi wa Menejimenti na Mameneja wote wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini kote wapatao sitini (60) kama Mkurugenzi Mkuu alivyoeleza katika hotuba yake. Katika mkusanyiko huu, ni matarajio yangu kwamba Mkutano huu ulikuwa ni fursa nzuri ya kubadilishana mawazo kwa ukaribu zaidi na kutafuta ufumbuzi wa matatizo na changamoto zinazohusiana na shughuli za utoaji huduma katika Mamlaka yenu. Aidha, hii ni njia mojawapo ya ushirikishwaji na uwajibikaji katika uendeshaji wa Taasisi hii. Sambamba na pongezi zangu za awali, nichukue fursa hii pia kwa kuwapongeza tena juu ya kauli mbiu ya mkutano mliyoichagua ambayo inaendana na mabadiliko ya huduma za makampuni yaliyoanza kutoa huduma za usafiri wa anga kwa gharama nafuu ambayo yatakuwa chachu ya ukuaji wa sekta ya Anga Tanzania. Ukuaji wa “low cost carriers” kwa sasa na kwa siku zijazo ni wa uhakika, hivyo nawaasa kuwa TAA kama mdau mkuu katika ukuaji huo, ihakikishe kwamba inajipanga vizuri kwa kuweka mazingira yanayowezesha kukabiliana na changamoto zitakazotokana na ukuaji huo.
Bila shaka na kama nilivyoarifiwa, mada mbalimbali zilizoandaliwa zilijadiliwa kwa kina na ufasaha kutokana na kwamba zote zilijikitika katika kufanikisha lengo la mkutano huu, ambazo zimeainishwa vizuri katika kauli mbiu yake.
Ndugu Wajumbe, Wizara tunajivumia sana mafanikio ambayo TAA imeyapata tangu kuanzishwa kwake, ni dhahiri kwamba mafanikio hayo si tu kwamba yatatokana na mipango mizuri mliyojiwekea bali pia yanatokana na usimamizi wenu wa karibu juu ya malengo hayo kwa kuwashirikisha kwa karibu wafanyakazi walioko chini yenu. Dunia ya sasa ya karne ya 21 katika viwanja vya ndege, inatawaliwa zaidi na utoaji huduma ulio bora ukilenga kuwavutia wateja na hili linaweza tu kufikiwa iwapo wafanyazi watahamasishwa na kupewa mafunzo ambayo yatawaongezea ujuzi ukiwemo wa kiteknolojia, weledi na hamasa ya kufanya kazi kwa bidii zaidi. Na ili ushirikishwaji huo utoe matunda yanayostahili, mnaaswa mhakikishe kwamba wafanyakazi hao wanahamasishwa na kupewa mafunzo stahiki na hasa katika kusimamia miradi ya maendeleo ambayo inatekelezwa sasa katika viwanja vyenu, inayokuja na inayotarajiwa.
Sanjari na hili mnaaswa pia mhakikishe kuwa ili kujua na kupima utendaji wao wa kazi, watumishi hao wapimwe juu ya utendaji wao wa kazi wa kila siku kwa kutumia mfumo ulio wazi wa kupima utendaji wa kazi wa watumishi wa serikali yaani OPRAS. Nimefahamishwa kuwa upimaji wa utendaji kazi chini ya OPRS umekuwa na changamoto nyingi. Hata hivyo, siamini kama changamoto hizo hazitatuliki, hivyo kwa weledi mlio nao, naomba muendelee kuboresha mfumo huo kwa lengo la upimaji bora wa watumishi hatimaye ulete matunda ya pamoja kwa utendaji ulio bora kwa Mamlaka.

No comments:

Post a Comment