TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, October 26, 2014

HABARI ZILIZOTAWALA SIKU YA JANA KWENYE VYOMBO MBALI MBALI VYA HABARI NI PAMOJA NA

Mke wa Rais wa China aipa msaada Shule ya Sekondari ya WAMA-Nakayama

IMG_4094
Na Anna Nkinda – Beijing, China Mke wa Rais wa China Mama Peng Liyuan ameahidi kutoa vifaa vya shule vikiwemo vya maabara pamoja na vitabu kwa ajili ya shule ya Sekondari ya WAMA-Nakayama ili  wanafunzi hao waweze kusoma vizuri masomo ya sayansi. Mama Liyuan aliitoa ahadi hiyo  jana wakati akiongea na  mke wa Rais Mama Salma Kikwete katika ukumbi maarufu wa watu (Great hall of the People) uliopo mjini Beijing.
“Nina mapenzi na Taasisi ya  WAMA, nakupongeza kwa kazi unayoifanya ukiwa Mke wa Rais ya kuwainua wanawake kiuchumi na kuwasaidia  watoto wa kike ambao ni yatima na wanaotoka katika mazingira hatarishi ambao nao wanapata elimu sawa na watoto wengine”.
Najua kitaaluma wewe ni mwalimu na unapenda shule mwaka huu nitakuunga  mkono zaidi katika masuala ya shule,  hii itawasaidia wanafunzi kusoma vizuri. Pia nitakuwa na ushirikiano  endelevu na Taasisi ya WAMA”, alisema Mama Liyuan.
Kwa upande wake Mama Kikwete alishukuru kwa msaada huo na kusema kila kwenye maendeleo changamoto hazikosekani alizitaja changamoto zinazoikabili sekta ya elimu ambazo ni  upungufu wa maabara, kutokuwepo kwa wataalamu wa maabara na walimu wa masomo ya sayansi wa kutosha.
Mama Kikwete  ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) alisema  katika upande wa elimu Serikali kwa kushirikiana na wananchi wamejitahidi kujenga shule nyingi za  Sekondari lakini  bado kuna  upungufu wa walimu wa masomo ya  sayansi , kutokuwa na maabara za kutosha, kutokuwa na vifaa vya maabara na  upungufu wa wataalamu wa maabara .
“Ninaomba  kuwe na ubadilishanaji wa ujuzi wa kazi (Exchange Program) kwa walimu wetu wa nchi hizi mbili hii itawasaidia kupata  utaalamu zaidi katika fani zao na kutoa mfano wa wataalamu wa maabara ambao wakija nchini watasaidia kwa kiasi kikubwa kuwafundisha wanafunzi masomo ya sayansi kwa njia ya vitendo”, alisema Mama Kikwete.
Shule hiyo ambayo inamilikiwa na Taasisi ya WAMA wanafunzi  wake ni watoto wa kike  ambao ni yatima na wanaotoka  katika mazingira hatarishi  kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani iko  kijiji cha Nyamisati wilaya ya Rufiji mkoani Pwani.
Hii ni mara ya pili kwa Mama Liyuan kuiunga mkono Taasisi ya WAMA ambapo mwaka 2013 alipotembelea nchini  alitoa Yuan milioni moja  sawasawa na shilingi milioni  250 za kitanzania na mabegi ya shule 100 kwa ajili ya wanafunzi wa shule ya Sekondari ya WAMA-Nakayama na vyerehani 20 kwa ajili ya Umoja wa Vikundi vya WAMA  (UVIMA).
Mama Kikwete  ameambatana na mumewe Rais Prof. Jakaya Mrisho Kikwete nchini China kwa ziara ya kikazi ya siku sita.
===============================================================

Dk. Shein Azungumza na Wakuu wa Mikoa na Wilaya Zanzibar Ikulu.

IMG_2736WAKUU wa Mikoa na Wilaya Zanzibar wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein,wakati alipokutana nao Ikulu Zanzibar.(Picha na Othman Maulid) 
IMG_2747KATIBU Mkuu  Kiongozi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, akizungumza wakati wa Mkutano huo na Wakuu wa Mikoa na Wilaya walipokutana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein Ikulu Zanzibar.(Picha na Othman Maulid
IMG_2756RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Wakuu wa Mikoa na Wilaya wa Zanzibar, wakati alipokutana nao Ikulu Zanzibar leo 25/102014.(Picha na Othman Maulid)
 =============================================================

KAMPUNI YA KARIATI YAKABIDHI WAKULIMA MATREKTA MANNE LEO, JIJINI DAR ES SALAAM

 
Kampuni ya Kariati Matracktor Diwani wa Kata ya Kwadelo, Kondoa mkoani Dodoma, Omary Kariati, leo imekabidhi matrekta manne kwa wakulima wa wilaya ya Kondoa (matrekta matatu) na Mbarali (trekta moja), katika hafla iliyofanyika leo asubuhi, kwenye Ofisi za Kariati Matrektor, Kinondoni, Dar es Salaam. Zinazofuatia ni picha za hafla hiyo. Picha/Maelezo na Bashir Nkoromo
Mkurugenzi Mtendaji wa Kariati Matractor, Omary Kariati akimkabidhi fungua za trekta Mwakilishi wa wkulima wa Kondoa, Karoli Lubuva, katika hafla ya makabidhiano hayo, iliyofanyika leo.
Kariati akikata uatepe kuzindua makabidhiano ya trekta hizo
Kariati akiwapa maelezo kuhusu trekta husika kabla ya kuzikabidhi kwa wawakilishi wa wakulima hao leo
Kariati akilijaribu moja ya matrekta hayo akiwa na mwakilishi wa wakulima kutoka Kondoa Karoli Lubuva.
=============================================================

Kamati ya Bunge ya Kudumu Ardhi, Maliasili na Mazingira yatembelea kiwanda cha Mifuko ya Plastiki (East African Industy)

unnamedWaziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira Mhe. Dkt injinia Binilith Satano Mahenge (kulia) akiwa na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu Ardhi, Maliasili na Mazingira  Mhe. Abdulkarim Hassan Shaha (wapili kulia),Pamoja na  Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu Ardhi, Maliasili na Mazingira wakikaguwa Mazingira katika moja ya kiwanda cha Mifuko ya Plastiki (East African Industy)kilichopo Mbagara jijini Dar es Salaam. unnamed1Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira, Mhe. Dkt injinia Binilith Satano Mahenge (kushoto),akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu Ardhi, Maliasili na Mazingira  Mhe. James Lembeli (Mb),baada ya kuwasili kiwanda  kinachozalisha mifuko ya plastiki cha Binfijaa kilichopo barabara ya Pugu jijini Dar es Salaam. unnamed2Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira, Mhe. Dkt injinia Binilith Satano Mahenge (wa nne kulia),Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu Ardhi, Maliasili na Mazingira  Mhe. James Lembeli Mb (wa tano ulia), pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu Ardhi, Maliasili na Mazingira wakikaguwa mifuko Inayozalishwa na kiwanda cha BinFijaa kilichopo barabara ya Pugu jijini Dar es Salaam.
================================================================

Dr Slaa akiwasilisha mada katika mkutano ulioandaliwa na TCD.

 
====================================================================

Mwandosya amuwakilisha JK Sherehe za miaka 50 ya uhuru wa Zambia

unnamed 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu asiye na Wizara Mhe. Mark Mwandosya  akisalimiana na Makamu wa Rais wa Kenya Mhe William Ruto wakati wa sherehe za kuadhimisha Miaka 50 ya Uhuru wa Zambia Mjini Lusaka jana. Mhe. Mwandosya alimuwakilisha  Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika sherehe hizo. unnamed3Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu asiye na Wizara Mhe. Mark Mwandosya (wa tatu kulia ) pamoja na Mkewe Lucy Mwandosya wakishiriki kuimba Wimbo wa Taifa wa Zambia wakati wa sherehe za kuadhimisha Miaka 50 ya Uhuru wa Zambia Mjini Lusaka jana. Wengine kutoka kulia ni Kaimu Rais wa Zambia Mhe Edgar Lungu ambaye pia ni Waziri wa Ulinzi, na wa  pili kulia ni Makamu wa Rais wa Nigeria Monance Namadi Sambo. unnamed5Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu asiye na Wizara Mhe. Mark Mwandosya  na mkewe Lucy Mwandosya wakisalimiana na Rais wa kwanza wa Zambia Mzee Kenneth  Kaunda wakati wa sherehe za kuadhimisha Miaka 50 ya Uhuru wa Zambia Mjini Lusaka jana. Mhe. Mwandosya alimuwakilisha  Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika sherehe hizo ambazo zimefanyika Mjini Lusaka jana.
Picha na Mpiga Picha wetu
================================================================

ZIARA YA WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA NCHINI POLLAND

 PG4A6758Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akizungumza na Wajumbe wa Chama cha Wafanyabiashara cha Polland jijini Warsaw akiwa katika ziara ya kikazi nchini humo Oktoba 24, 2014. Wengine Pichani kutoka kushoto ni Makamu wa Rais na Mkurugenzi Mkuu wa Chama cha Wafanyabiashara cha Polland, Bw. Marek Kloczko,Naibu Katibu  Mkuu wa  Wizara ya Mambo ya Nje ya Polland, (Under Secretary Of State Ministry of Foreign Affairs),  Bibi Katarzyna Kacperczyk na Bwana  Jerzy Pietrewiez ambaye ni  Katibu Mkuu Wizara ya Uchumi ya Polland  (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)PG4A6721Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Watanzania waishio Polland baada ya kuwasili jijini  Warsaw kwa ziara ya kikazi  Oktoba 24, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) PG4A6747Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na wajumbe wa Chama cha Wafanyabiashara cha Polland  jijini Warsaw akiwa katika ziara ya kikazi nchini humo Oktoba 24, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) PG4A6770 Baadhi ya wajumbe wa Chama cha Wafanyabiashara cha Polland wakimsikiliza Waziri Mkuu, Mizengo  Pinda wakati alipowahutubia jijini Warsaw Oktoba 24, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) PG4A6813Waziri Mkuu Mizengo Pinda akikagua matrekta yanayotengenezwa katika kiwanda cha  ROL- BRAT  kilichopo Warsaw, Polland akiwa katika ziara ya kikazi nchini humo Oktoba 24, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) PG4A6832Waziri Mkuu Mizengo Pinda akikagua matrekta yanayotengenezwa katika kiwanda cha  ROL- BRAT  kilichopo Warsaw, Polland akiwa katika ziara ya kikazi nchini humo Oktoba 24, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) PG4A6897Waziri Muu, Mizengo  Pindaakipata maelezo kutoka kwa mshauri wa uchumi nchini Polland Bw, Aleksandr Zincman(kushoto)  kuhusu usindikaji ngano wakati alipokagua kiwanda cha kusindika unga   cha  Chojnow nchini Polland akiwa kayika ziara ya kikazi nchini huo Oktoba 24, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)   PG4A6900Waziri Muu, Mizengo  Pindaakipata maelezo kutoka kwa mshauri wa uchumi nchini Polland Bw, Aleksandr Zincman(kushoto)  kuhusu usindikaji ngano wakati alipokagua kiwanda cha kusindika unga   cha  Chojnow nchini Polland akiwa kayika ziara ya kikazi nchini huo Oktoba 24, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)    PG4A7041Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akipata maelezo kutoka  kwa mshauri wa uchumi nchini Polland Bw, Aleksandr Zincman (kulia) wakati alipotembelea  kiwanda cha kutengeneza  maghala ya kuhifadhia nafaka (silos), mashine za kukausha nafaka na mashine za kusafisha nafaka cha Chojnow nchini Polland akiwa katika ziara ya kikazi nchini humo Oktoba 24, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
==================================================================

MKUTANO WA KUANDAA RAMANI YA MJI WA ZANZIBAR WAFANYIKA

04Mkuu wa Mkoa Mjini Mgharibi Maalim Abdalla Mwinyi Khamis ambae alikuwa Mwenyekiti wa mkutano wa Mpango  wa kuandaa ramani ya mji wa Zanzibar akizungumza na washiriki wa mkutano huo.Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.06   Baadhi ya washiriki wa mkutano uliojadili mpango wa kuandaa ramani ya Mji wa Zanzibar wakifuatilia maelezo yaliyotolewa kwenye mkutano huo katika Hoteli ya Marumaru.
03Mshauri mwelekezi kutoka kampuni ya Shapira Hellerman ya Israel,   Jos Hellerman akitoa taarifa  ya ramani ya Mji wa Zanzibar katika mkutano uliozungumzia mpango wa kuandaa matumizi bora ya ardhi katika Hoteli ya Marumaru, Shangani Mjini Zanzibar. 01Mkurugenzi  Mipango Miji na vijiji Muhammad Juma akitoa maelezo kwa washiriki wa mkutano wa kuandaa ramani ya Mji wa Zanzibar uliofanyika Hoteli ya Marumaru, Shangani.
==============================================================

Tanzania and China Marks 50 Years of Diplomatic Relations

D92A7592President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete delivers his speech during the celebrations to mark 50 years anniversary of the establishment of the diplomatic relations with China held at Diaoyutai State Guest House in Beijing yesterday evening. D92A7608President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete delivers his speech during the celebrations to mark 50 years anniversary of the establishment of the diplomatic relations with China held at Diaoyutai State Guest House in Beijing yesterday evening. D92A7667President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete and China’s Vice President Li Yuanchao cuts a special cake during the celebrations to mark 50 years of establishment of Diplomatic relations between Tanzania and People’s Republic of China yesterday in Beijing.  D92A7680President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete together with China’s Vice president Li Yuanchao unveils special coins during the celebrations to mark 50 years anniversary of the establishment of the diplomatic relations with China held at Diaoyutai State Guest House in Beijing yesterday evening.(picha na Freddy Maro)D92A7687President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete together with China’s Vice president Li Yuanchao unveils special coins during the celebrations to mark 50 years anniversary of the establishment of the diplomatic relations with China held at Diaoyutai State Guest House in Beijing yesterday evening.(picha na Freddy Maro)
===========================================================

Benki ya Exim yasaini mkataba wa mwaka mmoja na Stand United FC

unnamed
Mkuu wa matawi wa Benki ya Exim Kanda ya Ziwa, Bw. Justus Mukurasi (wapili kushoto) akibadilishana mkataba na Mwenyekiti wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Stand United, Bw. Amani Vicent (wapili kulia) wakati wa hafla fupi iliyofanyika mkoani Shinyanga jana. Mkataba huo utaiwezesha benki kuidhamini timu hiyo katika ligi kuu ya mpira wa miguu ya Vodacom (VPL) katika msimu wa 2014/2015. Wakishuhudia wa kwanza kushoto ni Meneja Msaidizi Tawi la Shinyanga, Bw. Hatunga Nicodemus na Katibu wa kamati ya Fedha, Bw. Bakari Salum (Wa kwanza kulia). Picha na mpiga picha wetu.  
unnamed3  Na Mwandishi Wetu, Shinyanga
 
Benki ya Exim imesaini makubaliano ya kuifadhili timu ya mpira wa miguu ya Stand United FC ya mkoani Shinyanga. Hii ni timu ya kwanza kupata ufadhili toka Benki ya Exim. Ufadhili huo wa mwaka mmoja utaisaidia timu hiyo kushiriki katika ligi kuu soka Tanzania bara kwa msimu wa 2014/2015.
 
“Makubaliano haya yanaikutanisha Benki ya Exim na mchezo mkubwa kuliko yote Tanzania,” alisema mkuu wa matawi ya Benki ya Exim kanda ya ziwa, Bw. Justus Mukurasi jana katika hafla fupi iliyofanyika mkoani Shinyanga. Aliongeza kuwa hakuna mchezo wenye watazamaji, wafuatiliaji na mashabiki wengi zaidi nchini kama mpira wa miguu.
 
“Timu ya Stand United inanguvu kubwa ya kuunganisha mashabiki  wa kanda ya ziwa. Hivyo ni jambo stahiki kwa Benki ya Exim kuisaidia timu hii ambayo mashabiki wake ni miongoni mwa wateja wa Benki ya Exim,” alisema Bw. Mukurasi.
 
Mukurasi aliongeza kuwa pande hizo mbili zilifanikiwa kuingia katika makubaliano ambayo yataiwezesha benki hiyo kuifadhili timu ya Stand United toka Ligi Kuu Tanzania bara ilipoanza.
 
“Kwetu sisi udhamini tuliofanya sio tu wa nembo, nbali ni ufadhili wa muda mrefu utakaozinufaisha pande zote mbili,” alisema Mukurasi.
 
”Tunatumai kuwa kila mmoja wetu ataweza kujifunza kutoka kwa mwenzake ili kupata matokeo mazuri kwa pamoja. Exim itasaidia kukuza na kuundeleza mchezo wa soka na hivyo kuiwezesha benki yetu karibu zaidi na wateja wake,” alisema Bw. Mukurasi.
 
Naye, Mwenyekiti wa Stand United FC, Bw. Aman Vicent alisema kuwa timu yake inayofuraha kubwa kuingia katika makubaliano na Benki ya Exim. “Tunadhamiria kuimarisha uhusiano huu ili kuhakikisha timu yetu inafanya vizuri katika Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu,” alisema Bw. Vicent.
 
“Kwa niaba ya Stand United FC, ningependa kuishukuru Benki ya Exim kwa jitiada zao za kusaidia wachezaji wetu na timu kwa ujumla. Tunafanya kazi kubwa kuhakikisha tunainua vipaji vya wachezaji wetu ili na wao waweze kufika mbali zaidi,” aliongeza Bw. Vicent.

No comments:

Post a Comment