TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, June 14, 2016

Askari 1,657 Wapandishwa Vyeo kwa Mwaka wa Fedha 2014/15

 
Ole Nasha amekiri kuwepo kwa ucheleweshwaji wa ulipaji wa mishahara inayolingana na vyeo katika jeshi la polisi na kufafanua kuwa yapo matatizo ya kiufundi yanayojitokeza wakati wa zoezi la kurekebisha mishahara ambayo husababisha baadhi ya askari kutorekebishiwa mishahara yao.
 
 Aliongeza kuwa juhudi hufanyika ili kutatua tatizo hilo mara mhusika anapowasilisha malalamiko yake Makao Makuu ya Jeshi hilo.Naibu Waziri huyo alisema Kitengo cha Maslahi Polisi Makao Makuu hupokea malalamiko yao na kuwasiliana na Mamlaka za ulipaji ili kutatua tatizo husika.
 
Ole Nasha ametoa wito kwa skari yeyote ambaye amepatwa na tatizo kama hilo awasiliane na viongozi katika Kamandi yake au Makao Makuu ya Polisi Idara ya Maslahi ili kupata ufumbuzi wa tatizo hili haraka iwezekavyo.
 
Kuhusu suala la ucheleweshwaji mishahara kuchangia katika vitendo vya polisi kujihusisha na rushwa, Ole Nasha alisema hilo suala halipo kwani polisi wanafanya kazi kwa kuzingatia maadili ya kazi na kwamba malalamiko ya ucheleweshwaji yanapotokea hushughulikiwa.

No comments:

Post a Comment