TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, March 30, 2016

UGONJWA WA ENDOMETROSIS WAWATESA WANAWAKE.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dk. Hamis Kigwangalla akizungumza na wanafunzi wa sekondari (hawapo pichani) juu ya ugonjwa wa Endometrosis katika semina hiyo kutoa elimu ya ugonjwa iliyoratibiwa na Miss Tanzania 2001, Millen Magese ambaye ni Mhanga wa Ugonjwa huo leo jijini Dar es Salaam.


Mkuruenzi Millen Magese Foundation na Miss Tanzania 2001, Millen Magese akizungumza wakati wa semina ya wanafunzi wa sekondari juu ya ugonjwa wa Endometrosis ambapo yeye ni mhanga wa ugonjwa huo iliyofanyika leo katika shule sekondari Tulian Jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, watoto na Wazee, Dk. Hamis Kigwangalla akiwa katika picha ya pamoja na Miss Tanzania 2001, Millen Magese na wageni walikwa katika semina ya utoaji wa elimu ya ugonjwa wa endometrosis leo jijini Dar es Salaam.


Na:Mwandishi Wetu,
 
IMEELEZWA kuwa kutibu ugonjwa wa Endometrosis ni gharama kubwa na serikali pekee yake haiwezi kushughulikia tatizo hilo.

Ugonjwa huo huwapata wanawake wakati wa hedhi na kufanya mwanake kukosa furaha na kutibu kwake ni gharama kubwa.

Akizungumza na leo katika semina kutoa uelewa kwa wasichana 400 iliyoandaliwa na Taasisi ya Miss Tanzania 2001 Millen Magese, Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamis Kigwangalla amesema kuwa ugonjwa wa Endometrosis unasababisha ugumba kwa wanawake.

Amesema kugundua ugonjwa huo unachukua kati ya miaka sita hadi 10 na kati ya wanawake 100 wenye ugonjwa huo nusu hawawezi kupata watoto.

Dk.Kigwangalla amesema kutambua ugonjwa huo kwa wataalam inachukua miaka saba hadi 10 hivyo kunahitajika elimu hata maeneo vijijini wanawake wanaweza wanaugua lakini hawajui.

“Wahenga wanasema raha ya mwanamke na kuzaa mtoto wake mwenye hivyo kuwa na ugonjwa unafanya mwanamke akose furaha katika maisha yake”amesema Kigwangalla.

Mkurugenzi wa Millen Magese Foundation,Miss Tanzania 20O1, Millen Magese amesema kuwa amefanyiwa operesheni mara 13 na kuamua kutoa elimu juu ya ugonjwa huo.

Amesema kuwa wanawake wengi wanasumbuliwa na ugonjwa huo lakini wanasema ni siri wakati ni ugonjwa wenye maumivu makali..

No comments:

Post a Comment