TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, March 19, 2014

SHIRIKA LA MAGEREZA LATILIANA SAINI MKATABA KATIKA SHUGHULI ZA KILIMO NA UFUGAJI NA MWEKEZAJI TOKA NCHINI UTURUKI, JIJINI DAR

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja( meza kuu mbele) akisaini Mkataba  wa Uwekezaji katika shughuli za Kilimo na Ufugaji na Mwekezaji toka nchini Uturuki, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya TARBIM LTD, Bw. Baddal Calikusu(wa kwanza toka kulia). Hafla fupi ya  utilianaji saini Mkataba huo umefanyika Machi 17, 2014 Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaam.2Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja(mbele meza kuu) akitoa utambulisho wa Makamishna wa Jeshi la Magereza(waliopo kushoto)kwa Mwekezaji wa shughuli za Kilimo na Ufugaji kabla ya kutiliana saini Mkataba wa Uwekezaji wa masuala ya Kilimo na Ufugaji katika Shamba la Magereza lililopo Bagamoyo, Mkoani Pwani.3Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akibadilishana Mkataba wa Uwekezaji katika shughuli za Kilimo na Ufugaji na Mwekezaji toka Nchini Uturuki ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya TARBIM LTD. Jeshi la Magereza kupitia Shirika lake la Magereza limetiliana saini Mkataba huo ambao utatekelezwa katika Shamba la Magereza lililopo Bagamoyo, Mkoani Pwani.4Mkurugenzi wa Kampuni ya TARBIM LTD(kulia mbele meza kuu) akiagana rasmi na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(kushoto mbele meza kuu) mara baada ya hafla fupi ya utilianaji saini wa Mkataba wa Uwekezaji katika shughuli za Kilimo na Mifugo ambapo Jeshi la Magereza kupitia Shirika lake la Magereza litatekeleza miradi ya Uzalishaji ya Kilimo na Ufugaji katika Shamba la Magereza lililopo Bagamoyo, Mkoani Pwani kwa kushirikiana na Kampuni ya Mwekezaji ya TARBIM LTD(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

No comments:

Post a Comment