Na Dotto Mwaibale
WAKALA
  wa Majengo Tanzania (TBA), umecharuka kwa kuingia mkataba na Kampuni 
ya Udalali ya Yono Auction Mart & Co. Ltd ili kusaidia kukusanya 
madeni ya wadaiwa sugu ambao walikopa nyumba.
Wakati
 huo huo mwakilishi wa kampuni hiyo ya udalali ya Yono Auction Mart 
& Co. Ltd, Scollastica Kevela ametoa siku tatu kwa wadaiwa wote wa 
TBA kuhakikisha wanalipa fedha hizo kabla ya kufikiwa na kampuni hiyo 
ambayo Jumatano ya Machi 16 mwaka huu itaanza rasmi kazi ya kuwaondoa 
katika nyumba za wakala huo watumishi wote wanaodaiwa kwa kufuata sheria
 kama inavyoelekeza.
Akizungumza
 katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo wakati wa 
kutiliana saini na kampuni hiyo ya udalali kwa ajili ya kukusanya fedha 
kutoka kwa wadeni wa wakala huo  Mtendaji Mkuu wa TBA ,  Elius 
Mwakalinga alisema wamefia hatua hiyo baada ya kuona wadaiwa wao ambao 
wengi wao ni kutoka sekta za serikali kushindwa kulipa fedha hizo.
"Tumeingia
 mkataba na Kampuni ya Yono Auction Mart baada ya kushinda zabuni ambayo
 tulitangaza Februari 23,2016 na sasa kazi yote ya ukusanyaji wa fedha 
hizo itafanywa na kampuni hiyo" alisema Mwakalinga.
Mwakalinga
 alisema fedha nyingi za wakala huo zipo mikononi mwa wadaiwa wao ambapo
 kwa mkoa wa Dar es Salaam na Dodoma ni shilingi.Bilioni 6 na kwa 
waliokopa ni sh.milioni 800 huku fedha zinazodaiwa kwa ajili ya kutoa 
ushauri mbalimbali wa ujenzi ni sh.bilioni 6.95.
Mwakilishi
 wa kampuni  ya Yono Auction Mart & Co. Ltd, Scollastica Kevela 
alisema wametoa siku tatu kwa wadaiwa wote kuhakikisha wanalipa fedha 
hizo vinginevyo watafikiwa na kampuni hiyo ambayo imepanga rasmi kupita 
kila nyumba inayodaiwa na kuwa kila muhusika atatakiwa kuilipa kampuni 
hiyo asilimia tano ya fedha anazodaiwa na TBA.
 Mtendaji
 Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ,  Arch. Elius Mwakalinga 
(kushoto), akikabidhiana hati ya mkataba na Mwakilishi wa Kampuni ya 
Udalali ya Yono Auction Mart & Co. Ltd, Scollastica Kevela Dar es 
Salaam leo asubuhi, baada ya kampuni hiyo kushinda zabuni ya kukusanya 
madeni ya TBA kuanzia leo.
 Taswira meza kuu katika mkutano huo.
 Mtendaji
 Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) , Arch Elius Mwakalinga 
(katikati), akizungumza katika mkutano huo kabla ya kutiliana saini na 
kampuni ya Yono. Kushoto Ofisa wa Idara ya Manunuzi, Mariam Kazoba.
No comments:
Post a Comment