TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, September 26, 2013

NCHIMBI: MSIWAHIFADHI WAHAMIAJI HARAMU

Na Penina Malundo


  Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt. Emmanuel Nchimbi,amesema Serikali itahakikisha wahamiaji haramu hawarudi nchini bila kufuata taratibu za kisheria zinazostahili kufuatwa. Dkt. Nchimbi aliyasema hayo Dar es Salam jana wakatiakizungumza na waandishi wahabari na kutoa matokeo ya awali juu ya utekelezaji Operesheni Kimbunga iliyolenga kuwaondoa wahamiaji haramu nchini

  Alisema kupitia operesheni hiyo awamu ya kwanza, wahamiaji haramu 12,604 wamerejeshwa katika nchi zao kutokana na agizo la kiongozi wa nchi, Rais Jakaya Kikwete. "Kati ya wahamiaji hawa,Wanyarwanda ni 3,448, Warundi 6,125, Waganda 2,496, Wakongo 589, Wasomalia 44, raia wa Yemeni mmoja na India mmoja," alisema Dkt. Nchimbi na kuongeza;"Ni vyema wahamiaji haramu wakafuata utaratibu wa kisheria,hata Watanzania wanaokwenda nchi nyingine nao wanapaswa kufuata utaratibu na si vinginevyo,"alisema.

   Alitoa wito kwa Watanzania,kuacha utamaduni wa kuwapokea na kuwahifadhi wahamiaji haramu jambo ambalo linaweza kuhatarisha maisha yao na nchi kwa ujumla. Alisema Watanzania wanapaswa kuwa macho na wageni wanaoingia nchini kutoka nchi nyingine bila kufuata taratibu za kuishi nchini kwani wengi wao wanauwezo wakufanya uhalifu hasa katika kipindi hiki cha usalama wa dunia kuwa hatarini.   

   Aliongeza kuwa, katika operesheni hiyo watuhumiwa 212 wa unyang'anyi wa kutumia silaha walikamatwa pamoja na mabomu 10 ya kutupwa kwa mkono, silaha 61, risasi 662 na mitambo miwili ya kutengeza silaha aina ya magobori

No comments:

Post a Comment