TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, August 27, 2014

MAMEYA NA WAKURUGENZI WA TANZANIA WATEMBELEA NYUMBA ZILIZOJENGWA KWA MBAO FINLAND

 Baadhi ya viongozi kutoka majiji sita ya Tanzania wakipata maelezo kuhusu mfumo wa ukusanyaji wa taka na uchujaji wa maji machafu katika jiji la LAHTI, kutoka kushoto ni mratibu wa mtandao wa majiji Tanzania, ( Tanzania Cities Network) Philoteus Mbogoro, Meya wa jiji la Tanga Omary Guledi, Lissa Tervo wa taasisi ya Uongozi ya Tanzania, Johanna Palamoki ambae ni mtaalam wa mipangomiji katika jiji la LAHTI, Mkurugenzi wajiji la Lahti Kari Porra na Meya wa jiji la Mbeya Athanas Kapunga ( picha zote na Vedasto Msungu wa ITV)
 Mkurugenzi wa jiji la LAHTI, Kari Porra akitoa maelezo kuhusu ujenzi wa nyumba hizo za mbao kwa mratibu wa ziara hiyo Godfrey Nyamrunda kutoka taasisi ya Uongozi ya Tanzania, nyuma yao ni Meya wa jiji la Dar Esa Salaam Dk Didas Masaburi
Badhi ya nyumba za ghorofa zilizojengwa kutumia mbao katika jiji la LAHTI nchini Finland ambazo zilitembelewa na madiwani wa majiji sita ya Tanzania waliokuwa katika ziara ya mafunzo nchini humo iliyoratibiwa na taasisi ya Uongozi ya Tanzania. Finland ni miongoni mwa nchi zenye maeneo makubwa ya misitu ya kupandwa dunaini, zaidi ya asilimia 80 ya eneo la nchi hiyo ni misitu na wenyewe wanasema nyumba zinazojengwa kwa kutumia mbao zina gharama nafuu kuliko kujenga kwa matofali au mawe.
 Viongozi kutoka majiji sita ya Tanzania wakiwa kando kando ya ziwa Maji ambako mkondo wa maji machafu kutoka majumbani huingia ziwani baada ya kuchujwa, viongozi hawa kutoka kushoto ni Stanslaus Mabula ambaye ni Meya wa jiji la Mwanza, Athanas Kapunga ambae ni meya wa jiji la Mbeya, Mussa Zungiza,mkurugenzi mtendaji wa jiji la Mbeya na Philoteus Mbogoro ambae ni mratibu wa mtandao wa majiji Tanzania TACIN
Badhi ya nyumba za ghorofa zilizojengwa kutumia mbao katika jiji la LAHTI nchini Finland ambazo zilitembelewa na madiwani wa majiji sita ya Tanzania waliokuwa katika ziara ya mafunzo nchini humo iliyoratibiwa na taasisi ya Uongozi ya Tanzania. Finland ni miongoni mwa nchi zenye maeneo makubwa ya misitu ya kupandwa dunaini, zaidi ya asilimia 80 ya eneo la nchi hiyo ni misitu na wenyewe wanasema nyumba zinazojengwa kwa kutumia mbao zina gharama nafuu kuliko kujenga kwa matofali au mawe.

No comments:

Post a Comment