Kaimu
 mwenyekiti wa Uukwaa la Katiba Tanzania Hebron Mwakagenda akizungumza 
na wanandishi wa habari leo Agosti 27, 2014 juu ya mwenendo wa bunge la 
katiba.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.
Wakati
 mchakato wa katiba Tanzania ukiwa ni kama kitendawili kisicho na majibu
 sahihi kutokana na mchakato huo kuvurugika na kukosa mwelekeo, nao 
Jukwaa la Katiba Tanzania (JUKATA) wazidi kumtupia lawama zote za 
kuvurugika bunge hilo mwenyekiti wa bunge hilo mheshimiwa Samweli Sitta 
na kudai kuwa ndiye aneyeuvuruga mchakato huo baada ya kugeuza Bunge 
hilo kama kikao cha Chama cha Mapinduzi (CCM).
Akizungumza
 na wanahabari muda huu jijini Dar es salaam kaimu mwenyekiti wa Jukwaa 
la Katiba Tanzania Hebron Mwakagenda amesema kuwa JUKATA wamekuwa 
wakifuatilia mchakato huu wa bunge ka katiba kwa wiki mbili hizi na 
kubaini mapungufu makubwa sana ambayo yanatokea jambo ambalo linaonyesha
 wazi kuwa mwenyeikiti wa bunge hilo hana nia wala dhamira ya kulipatia 
taifa katiba mpya ya watanzania.
Wanahabari
 mbalimbali wakiwa wanamsikiliza kiongozi huyo wakati wa mkutano Bw 
Mwakadenga amesema kuwa swala la mahudhurio ya wabunge wanaoshiriki 
katika kamati mbalimbali za bunge hilo yamekuwa madogo sana na yasiyo ya
 kuridhisha ikiwa ni pamoja na wabunge wengi kutokuhudhuria katika 
kamati hizo pamoja na kusaini kulipwa posho za siku jambo ambalo amesema
 kuwa ni wizi mpya kwa
watanzania,
 “Kwanza
 bunge la katiba linaonyesha kuwa wajumbe 441 wamehidhuria lakini 
uchunguzi wetu unaonyesha kuwa hawa ni wale wote ambao wamewahi kufika 
na kusaini kwenye kitabu cha mahudhurio wengine wao takribani 100 
tuligundua kuwa hawapo bungeni wakiwemo mawaziri wa Jamhuri ya Muungano 
wa Tanzania na serikali ya mapinduzi Zanzibar pamoja na baadhi ya 
viongozi wa kamati”amesema Mwakagenda.
Ameongeza
 kuwa mambo mengine ambayo yanalifanya bunge hilo kuvurugika ni pamoja 
na kukosekana kwa muafaka na maridhiano ya kitaifa, matumizi mabaya 
fedha ikiwa ni pamoja na Wajumbe kulipwa bila kuhudhuria bungeni, 
kukosekana kwa theluthi mbili toka Zanzibar ili kupitisha katiba,pamoja 
na uondoaji wa vifungu muhimu kwenye rasimu mambo ambayo amesema kuwa 
mwenyekiti Samweli Sitta ameyafumbia macho na kijifanya kama hayaoni 
huku akiwa anajua wazi kuwa anauzika mchakato huo.
“Huyu
 mzee hatujamwelewa kabisa, sisi tumekaa tumezungumza naye tukamuuliza 
atueleze swala la theluthi mbili hawa wajumbe watapatikana wapi hajatupa
 jibu la kuridhisha na ukimwona ni kama mtu ambayeameshachanganyikiwa, 
anapambana na kila anayekuja mbele yake, iwe mwandishi, mwanaharakati, 
mbunge, yeye amekaa kujihami tu, sasa hali hii sio nzuri kwa mchakato 
muhimu kama huu”alisema kiongozi huyo wa JUKATA.
Katika
 hatua nyingine JUKATA wamemwomba raisi Kikwete kiusimamisha mchakato 
huu wa katiba hadi kipindi kingine kutokana na kuonekana wazi kuwa 
hauwezekani na kusema Tanzania imekuwa na michakato mingi ambayo sisi 
kama taifa hatuwezi kuiendesha kwa wakati mmoja na kupata katiba bora, 
“Kusema ukweli taifa sasa lina michakati mingi sana mfano mchakato wa vitambulisho vya taifa, uchaguzi wa serikali za mitaa, daftari la kudumu la kupiga kura na michakato mingine mikubwa, hii haitaki usome sana ndo uelewe ni kutumia busara tu kwamba huu mchakato wa katiba hautawezekana tena, sisi tunamwomba mheshimiwa Rais Kikwete awasikilize watanzania na kuusimamisha mchakato huu wa katiba ili tujipange upya kuanza
“Kusema ukweli taifa sasa lina michakati mingi sana mfano mchakato wa vitambulisho vya taifa, uchaguzi wa serikali za mitaa, daftari la kudumu la kupiga kura na michakato mingine mikubwa, hii haitaki usome sana ndo uelewe ni kutumia busara tu kwamba huu mchakato wa katiba hautawezekana tena, sisi tunamwomba mheshimiwa Rais Kikwete awasikilize watanzania na kuusimamisha mchakato huu wa katiba ili tujipange upya kuanza
tena.
Mchakato
 wa katiba umekuwa ukiendelea jijini Dodoma bila ya mariano na wajumbe 
waliotoka wa UKAWA huku kukiwa na taarifa kuwa rais amekubali kukutana 
nao wiki hii kwa ajili ya mazungumzo ya kuunasua mchakato huu.



No comments:
Post a Comment