TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, June 23, 2016

Rais Dkt. Magufuli alipokabidhiwa Taarifa ya Uchaguzi Mkuu wa 2015 leo Ikulu jijini Dar.


Baadhi ya viongozi wa dini waliohudhuria hafla ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kumkabidhi Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Taarifa ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani uliofanyika Novemba 25, 2015 , Ikulu jijini Dar es Salaam leo.
Mwanasheria Mkuu Mstaafu Jaji Mstaafu Mark Boman akiteta jambo na Mkurugenzi wa Uchaguzi Mstaafu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Rajab Kiravu kwenye hafla ya tume hiyo kumkabidhi Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Taarifa ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani uliofanyika Novemba 25, 2015 na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya Mabalozi waliohudhuria hafla ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kumkabidhi Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Taarifa ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani uliofanyika Novemba 25, 2015, Ikulu jijini Dar es Salaam leo.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (CDF) Jenerali Davis Mwamunyange (kulia) akiwa na Wakuu wa Vikosi vya Majeshi, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Ernest Mangu, na Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Rashid Othman, Kamishna Jenerali wa Magereza John Minja, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Kamishna Mstaafu Valentino Mlowola na Kamishna wa Uhamiaji (Sheria) Said Kamugisha wakiwa kwenye hafla ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli kukabidhiwa Taarifa ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani uliofanyika Novemba 25, 2015 na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam leo.

MIAKA 10 YA UMOJA SWITCH WAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM

Afisa Mtendaji Mkuu wa Umoja Switch Bw Danford Mbilinyi Akizungumza na Vyombo vya Habari leo wakati wa Uzinduzi wa Maadhimisho ya Miaka 10 ya UMOJASWITCH.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Umoja Switch Bw Danford Mbilinyi Amezindua Amezindua Rasmi Maadhimisho ya Miaka 10 ya Umojaswitch..Katika Hotuba yake aliyoitoa kwa Vyombo vya Habari Amesema Miaka 10 iliyopita Benki ndogo zilikuwana Changamoto Kubwa ya kuweza Kupatia Huduma za ATM wateja wao kwani Mitaji na Gharama za uwekezaji,Uendeshaji wa ATM na Wigo wao wa utoaji wa Huduma hii Uliwapa Changamoto kubwa.Kutokana na ChangamotoHizo Mabenki Sita Yaliamua Kuanzisha Umoja wao ili Yaweze Kuweka ATM na Kuwezesha Benkihizo Kushirikiana katika Utoaji wa Huduma a ATMKWA Wateja wao,Umoja huo Ndio uliozaa UMOJASWITCH.

Akielezea Zaidi Bw Danford Mbilinyi Amesema kwa Sasa Umoja Switch Ina Jumla ya Mabenki 27 Yanayoshirikana katika Utoaji wa Huduma za Kibenki Kupitia ATMzaidi ya 250 Nchi nzima.Kupitia Umojaswitch Mteja wa Benki Yenye Tawi Moja Inamwezesha Mteja wake Kupata Huduma Sehemu Yoyote Tanzania.
Mafanikio ya Umojaswitch ni Mafanikio ya Ushirikiano na Mabenki Pamoja na Mzingira Wezeshi yaliowekwa na Serikali Kuptia Benki Kuu.Wakti Umoja Huo Ulioanzishwa na Kuanza kutoa Huduma zake Jumla ya Benki sita tu ndio walikuwa wanachama wa Umoja Swich Pamoja na ATM 27 tu.
Tofauti na Ssas umoja huo una Wanachama 27 unaotoa Huduma kwa zaidi ya wateja Milionoi 2 kupitia Zaidi ya ATM 250.Mafanikio ya Umoja Huo yanachangiwa na Ubunifu na Huduma zitolewazo na Umojaswitch kama Kuhamisha Fedha Kutoka Benki moja kwenda Nyingine zilizopo ndani ya Umoja huo Kupitia ATM Pamoja na Huduma za Kununua Luku Mpesa pamoja na Kulipia Huduma Mbalimbali Kupitia Hudama za Mobile Banking na zile za Uwakala.

Katika Uzinduzi wa Maadhimisho ya Miaka 10 ya Umojaswitch ni Kutoa Elimu kwa Wananchi Kuhusu Umuhimu wa Mtandao huu na Technolojia kwa Ujumla Katika Kukuza na Kuendeleza Sekta ya Kibenki na Mchango wake katika maendeleoa ya Maisha ya Kila siku, Pia katika Maadhimisho haya Wanategemea Kufanya Shuguli Mbalimbali ikiwemo kuchagiza Matumizi ya Technolojia na Ubunifu Kwenye Vyuo vikuu hapa Nchini kwajili ya kuwa Kichocheo muhimu Katika Maendeleo ya Sekta ya Kibenki h 
= ============================================

KAMPUNI YA TOMONI FARMS LIMITED YAFUNGUA DUKA NA MGAHAWA WA KISASA WA MAZAO YA KILIMO DAR

Kampuni ya Tomoni Farms Limited, inayomilikiwa na wazawa, wakijishughulisha na Kilimo cha umwagiliaji cha mazao ya Matunda na Mbogamboga, wamefungua duka na Mgahawa wa Kisasa kwa ajili ya uuzaji wa mazao yao katika hali ya usafi na usalama wa hali ya juu uliopo eneo la jirani na Victoria, Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa Habari mapema leo Jijini Dar Es Salaam, wakati wa utambulisho wa duka hilo na shughuli zinazofanywa na kampuni hiyo ya Tomoni Farms Limited, Mkurugenzi wa uendeshaji wa Kampuni hiyo Bwana Franklin Bagalla ameeleza kuwa, wameamua kuwasogezea watanzania bidhaa bora za kilimo ambazo watazipata moja kwa moja kupitia duka lao hilo na watajiona kama wapo shambani ama bustanini kwa namna ya uwekezaji wao walivyoweza kuuandaa ikiwemo mazingira safi na utunzaji wa kisasa kutoka shambani hadi kumfikia mlaji.

“Baada ya kuwekeza kwa miaka mine katika kilimo cha Matunda na Mboga mboga kwa kutumia teknolojia ya umwagiliaji, huku tukiwa na uhakika wa kutoa mazao Mwaka mzima, sasa tumewekeza katika miundo mbinu ya kuhakikisha mazao yetu yanawafikia walaji yakiwa katika hali ya usafi na usalama. Hivyo kupitia katika duka letu hili la kisasa hapa Dar es Salaam linatoa fursa kwa wananchi kujipatia bidhaa za kila aina na watazipata kwa hali ile ile kama zipo shambani na tunawakaribisha sana” alieleza Bwana Bagalla.

DK. MENGI ACHANGIA MADAWATI 1,000, ATOA SOMO KWA WATU MATAJIRI


Hata hivyo Dk. Mengi alisema kuwa anaamini kama watu matajiri nchini wakiungana kwa pamoja na kujadili jinsi ya kumaliza tatizo la madawati nchini basi jambo hilo litaweza kupatiwa ufumbuzi wa haraka tofauti na sasa ambapo linakwenda kwa mwendo wa kusuasua.

"Ukisaidia mtu mmoja katika elimu ni sawa umesaidia jamii na taifa kwa ujumla kama watu matajiri wakisema wakae kwa pamoja na kuangalia jinsi ya kumaliza tatizo hili linaweza kutatuliwa na shida ya madawati kumalizika.


Mkurugenzi Mtendaji wa makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi akimkabidhi mfano wa hundi ya milioni 35, Mkuu wa wilaya ya Haneni, Husna Rajab. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Mji wa Handeni, Kenneeth Haule, Mwenyekiti wa Mji wa Handeni, Twaha Mgaya na Mwenyekiti wa Halmshauri ya Handeni, Ramadhani Diliwa.

Mkurugenzi Mtendaji wa makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi akimkabidhi mfano wa hundi ya milioni 35 kwa ajili ya ununuzi wa madawati 500, Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Alhaj Majid Mwanga. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi Chalinze, Edes Lukoa, Mkurugenzi wa Bagamoyo, Natujwa Melau, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Ally Issa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze, Said Zikatimu.

Mkurugenzi Mtendaji wa makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi akizungumza katika halfa ya kukabidhi milioni 70 kwa wilaya ya Handeni na Bagamoyo ambazo zitawezesha wilaya hizo kununua madawati 1,000 na kila wilaya kupata madawti 500.

"Matajiri wanatakiwa kutambua kuwa wanatakiwa kurudisha shukrani zao kwa Mungu, taifa na wananchi na hasa kwa walio na hali ya chini kwani hao ndiyo wanaowasaidia kufanya biashara zao kwa amani," alisema Dk. Mengi.

Aidha amewataka wakuu wa wilaya hizo kuondoa hofu ya kufukuzwa kazi kama watakuwa hawajakamilisha na wanachotakiwa kufanya kwa sasa ni kuongeza juhudi huku akiwashauri kuandaa mikutano katika wilaya zao na kushirikisha wananchi wao ili waweze kuchangia na hatimaye tatizo hilo kumalizika.

Kwa upande wa mkuu w wilaya ya Bagamoyo, Alhaj Majid Mwanga na mkuu wa wilaya ya Handeni, Husna Rajab wamemshukuru Dk. Mengi kwa msaada ambao amewapatia na kuwataka watanzania wengine kuwa na moyo wa kujitolea kama jinsi amevyofanya Dk. Mengi kwa kuchangia upatikanaji wa elimu bora.

Awali kabla ya msaada ambao umetolewa na Dk. Mengi, wilaya ya Bagamoyo ilikuwa ikikabiliwa na upungufu wa madawati 2,463 na Handeni ikikabiliwa na tatizo la upungufu wa madawati 4,000.

BENKI YA DUNIA YAIPATIA TANZANIA SHILINGI BILIONI 440 KWAAJILI YA KUSAIDIA KAYA MASIKINI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dkt. Servacius Likwelile akibadilishana mawazo na Mratibu Maendeleo ya Sekta Binafsi na SAGCOT kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu mara baada ya kumaliza kusaini Hati ya Makubaliano itakayoiwezesha Tanzania kupata nyongeza ya Sh. Bilioni 440 kwa ajili ya mradi wa Tasaf II. Tukio hilo limefanyika katika Ukumbi wa Wizara Jijini Dar es salaam

Na Benny Mwaipaja, WFM

Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango imesaini hati ya makubaliano na Benki ya Dunia itayoiwezesha Tanzania kupata nyongeza ya fedha katika mradi wa Tasaf kiasi cha Shilingi Bilioni 440.

Hati hiyo ilisainiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia Bella Bird, Makao Makuu ya Wizara ya Fedha, Dar es Salaam, leo, Juni 23, 2016.

Akiongea wakati wa kusaini hati hiyo Dkt. Likwelile alisema kuwa fedha hizo zitaelekezwa katika mradi wa Tasaf II kwa ajili ya kuziwezesha kaya maskini kukuza kipato chao kupitia ajira za muda zitakazowawezesha kupeleka watoto shule na kuwapatia huduma za afya.

Aliongeza kuwa katika mwaka wa fedha 2015/2016 Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia imefanya kazi kubwa iliyowezesha miradi kumi kupitishwa ambayo ina thamani ya Shilingi Trilioni 1.9.

"Miongoni mwa miradi iliyopata ufadhili ni pamoja na mradi wa kuboresha mazingira ya biashara uliopata shilingi Bilioni 168, mradi wa kusambaza umeme vijijini (REA), uliopata Shilingi Bilioni 440" Aliongeza Dkt. Likwelile.

Aidha, alisema kuwa Serikali inaendelea na majadiliano na Benki hiyo kwa ajili ya kuboresha Bandari ya Dar es Salaam, ambapo kiasi cha dola Milioni 600 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

Dkt. Likwelile ameishukuru Benki ya Dunia kwa mchango wake mkubwa na kusema kuwa Serikali itahakikisha kuwa inazisimamia taasisi zinazotekeleza miradi hiyo ili ziweze kutumia fedha hizo vizuri na kwa malengo yaliyokusudiwa.

Kwa upande wake Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia, Bella Bird, amepongeza juhudi za Serikali ya awamu ya tano katika kupambana na rushwa na kuweka mazingira rafiki kwa sekta binafsi.

Aliongeza kuwa sekta binafsi ndizo zinatoa ajira kwa wingi na kusaidia kuchangia katika kuongeza mapato ya Serikali. Ameahidi kuwa Benki yake itaendelea kushirikiana na Tanzania ili kuiwezesha kufikia malengo yake ya kiuchumi na kijamii kwa faida ya wananchi wake.

====================================================
 

Msama amwangukia Dkt Mwakyembe,amwomba radhi.

 






==========================================

KATIBU MKUU OFISI YA WAZIRI MKUU AKUTANA NA BODI YA MRADI WA MENEJIMENTI YA MAAFA DAR ES SALAAM.

T4 
T5 
T6 
===================================================

Ubia wa TTCL na Bharti Airtel Wafikia Kikomo


Msajili wa Hazina, Laurence Mafuru (wa kwanza kulia) akimkabidhi Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL, Profesa Tolly Mbwete (katikati) hati ya mauzo ya hisa asilimia 35 za Kampuni ya Bharti Airtel Afrika. Serikali imezinunua rasmi hisa za kampuni hiyo ndani ya TTCL ambapo leo wamesaini mkataba wa mauziano wa hisa hizo. Kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Bharti Airtel Afrika, Christian De Faria akishuhudia.
Msajili wa Hazina, Laurence Mafuru (kushoto waliokaa) akitiliana saini na Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Bharti Airtel Afrika, Christian De Faria (mwenye tai nyekundu) kwenye hafla ya kusaini mkataba wa mauziano. Serikali leo imezinunua rasmi hisa asilimia 35 za kampuni ya Bharti Airtel Afrika ndani ya Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL). Nyuma waliosimama ni viongozi mbalimbali walioshuhudia tukio hilo.

Msajili wa Hazina, Laurence Mafuru (mwenye tai ya bluu) akionesha hati ya mauziano ya hisa. Serikali leo imezinunua rasmi hisa asilimia 35 za kampuni ya Bharti Airtel Afrika ndani ya Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), ambapo sasa inakuwa ikiimiliki TTCL kwa asilimia 100. Kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Bharti Airtel Afrika, Christian De Faria (mwenye tai nyekundu) akiwa kwenye hafla ya kusaini mkataba wa mauziano hayo. Nyuma waliosimama ni viongozi mbalimbali wa TTCL na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano walioshuhudia tukio hilo.

Msajili wa Hazina, Laurence Mafuru (kushoto) akibadilisha hati ya mkataba wa mauziano ya hisa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Bharti Airtel Afrika, Christian De Faria. Wanaoshuhudia ni viongozi mbalimbali walioshuhudia tukio hilo.

ASILIMIA 89 YA WATANZANIA WAMKUBALI RAIS MAGUFULI, AWAPIKU JK NA LOWASSA; UTAFITI WA CZI WABAINISHA

No comments:

Post a Comment