Mahafali ya nane ya Chuo cha 
Teknolojia Dar es Salaam (DIT), yanatarajiwa kufanyika Januari 31 mwaka 
huu katika viwanja vya chuo hicho na yatatanguliwa na utoaji wa tuzo na 
zawadi mbalimbali kwa wahitimu ambao wamefanya vizuri katika masomo yao.
 Taarifa ya DIT kwa vyombo vya habari imesema kuwa tuzo kwa 
wanafunzi zitatolewa Januari 23 mwaka huu ikiwa ni wiki moja kabla ya 
mahafali hayo ambayo wahitimu katika ngazi na masomo tofauti 
watatunukiwa.
 Wahitimu watakaotunukiwa ni siku hiyo ni pamoja na wa 
Stashahada ya Uhandisi (Ordinary Diploma), cheti cha awali cha TEHAMA 
(IT) mwaka wa masomo 2013/2014.
 Wahitimu wametakiwa kusoma utaratibu wa kuthibitisha kushiriki 
mahafali hayo katika tovuti ya Taasisi www.dit.ac.tz na “Rehearsal” 
itafanyika Ijumaa tarehe 30 Januari 2015.
 “Malipo ya Tshs 30,000/= kwa ajili usajili yatafanyika kwenye 
tawi lolote la NBC kwenye akaunti namba 018101003145 na kujisajili 
kupitia tovuti ya Taasisi www.ac.dit.tz” Inasema taarifa hiyo.
 Malipo yanatakiwa klufanyika kwa kutumia jina kamili kama 
linavyoonekana kwenye orodha ya wahitimu iliyotolewa kwenye tovuti ya 
Taasisi, namba ya usajili na dhumuni la malipo mf. Ada, transcript na 
graduation.
 Kulingana na taarifa hiyo, mwisho wa kujisajili ni tarehe 31 
Desemba, 2014 na wahitimu wametakiwa kufahamisha kuhusiana na mahafali 
hayo.
No comments:
Post a Comment