Kiongozi
 wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya
 Mipango, Bibi Florence Mwanri (Kushoto) akizungumza na Meneja wa Uwanja
 wa ndege wa Mpanda, Mkoani Katavi Bw. Seneti Lyatuu (Kulia). 
Anayefuatilia mazungumzo ni Bw. Omary Abdallah ambaye Kaimu Mkurugenzi 
wa Mipango na Ufuatiliaji (Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango).  
Timu
 ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango
 ikiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Mpanda kujionea shughuli mbalimbali
 za maendeleo uwanjani hapo. 
Kiongozi
 wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya
 Mipango, Bibi Florence Mwanri (Kushoto) akizungumza na Meneja wa Uwanja
 wa ndege wa Mpanda, Mkoani Katavi Bw. Seneti Lyatuu (Kulia). 
Anayefuatilia mazungumzo ni Bw. Omary Abdallah ambaye Kaimu Mkurugenzi 
wa Mipango na Ufuatiliaji (Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango).  
Meneja
 wa Uwanja wa ndege wa Mpanda, Mkoani Katavi Bw. Seneti Lyatuu (Kulia) 
akifafanua jambo kwa Kiongozi wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo 
kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Kushoto). 
Anayewasikiliza ni Kaimu Mkurugenzi wa Mipango na Ufuatiliaji (Ofisi ya 
Rais, Tume ya Mipango), Bw. Omary Abdallah (Katikati).  
Timu
 ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango
 wakipata maelekezo ya uendelezaji wa Uwanja wa Ndege wa Mpanda kutoka 
kwa Meneja wa uwanja huo, Bw. Seneti Lyatuu (Kushoto). 
…………………………………………………………………………….
Na Saidi Mkabakuli, Mpanda
Kufuatia kukamilika kwa ukarabati 
na upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Mpanda, mkoani Katavi, Serikali 
imewaasa watumiaji wa uwanja huo kutunza miundombino ya uwanja huo ili 
kuweza kuhudumia wakazi na wageni wapitao uwanjani hapo kwa muda mrefu.
Wito huo umetolewa na Kiongozi wa 
Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya 
Mipango, Bibi Florence Mwanri wakati walipofanya ziara ya kukagua 
maendeleo ya miundombinu katika Uwanja wa Ndege wa Mpanda, mkoani 
Katavi.
Bibi Mwanri alisema kuwa serikali 
kupitia Mamlaka ya Viwanja vya Ndege imekamilisha kazi ya kuufanya 
uwanja huo uwe wa kiwango kizuri tayari kwa kutumika kwa ndege za 
binafsi na biashara, hivyo uongozi wa uwanja huo hawana budi ya 
kuhakikisha miundombinu ya uwanja huo inatunzwa ipasavyo.
“Kama munavyofahamu Serikali 
imekuwa ikiwekeza sana katika uendelezaji wa miundombinu ya usafiri 
nchini hasa kuendelea kuboresha miundombinu ya usafiri wa anga ili 
kuongeza ufanisi na kuendelea na kazi ya ujenzi na ukarabati wa viwanja 
vya ndege katika maeneo ya kimkakati, hivyo kuna haja ya kuunga mkono 
jitihada hizi za Serikali,” aliasa Bibi Mwanri.
Akitoa taarifa ya uendelezaji 
uwanja huo kwa msafara wa timu ya ukaguzi, Meneja wa Uwanja wa Ndege wa 
Mpanda, Bw Seneti Lyatuu alisema uwanja huo umeboreshwa na hivyo, 
unaweza kutumika kutua na kuruka ndege za kiwango cha kati na hata zile 
ndege kubwa zinaweza kutua kwa dharura.
“Uwanja huu umekarabatiwa na 
barabara ya kuruka na kutua ndege imerefushwa kwa kiwango cha lami 
kutoka urefu wa mita 1,500 na upana wa mita 30 hadi kufikia urefu wa 
mita 1,820 na upana wa mita 30,” alisema Bw. Lyatuu.
Kwa mujibu wa Meneja huyo, 
kukamilika kwa uwanja huo kumevutia idadi ya abiria wanaoutumia uwanja 
huo kutoka abiria 285 mwaka 2009 hadi 2,390 mwaka 2013/14.
Kwa mujibu wa Mpango wa Maendeleo 
wa Taifa wa Miaka Mitano (2011/12 – 2015/16),  Miundombinu ni kipaumbele
 cha kwanza, hasa uwekezaji mkubwa katika miundombinu ya nishati, 
usafirishaji (bandari, reli, barabara na usafiri wa anga), maji (safi, 
taka na ya uzalishaji) na TEHAMA.
Serikali imeandaa Mpango wa 
Maendeleo wa Miaka Mitano (2011/12 -2015/16) wa kutekeleza Dira ya Taifa
 ya Maendeleo 2025. Lengo kuu la Mpango huu ni kufungulia fursa za 
ukuaji uchumi wa nchi ili kuweka misingi ya ukuaji mpana wa uchumi na 
unaolenga watu walio masikini zaidi. Mpango wa Kwanza wa Maendeleo wa 
Miaka Mitano unawianisha katika mfumo mmoja wa mipango mbalimbali ya 
maendeleo ya kitaifa ili kutoa mwongozo wa utekelezaji na kuipa Serikali
 fursa na mfumo rasmi wa ufuatiliaji na tathmini wa miradi ya maendeleo 
kitaifa.
Lengo la Dira ni  kuibadili Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.
No comments:
Post a Comment