Siku ya Kimataifa ya Kujitolea 
Duniani huadhimishwa tarehe 5 Desemba kila mwaka kwa lengo la kutambua 
mchango wa kujitolea unaotolewa kwa ajili ya maendeleo katika jamii 
tunamoishi, kitaifa na kimataifa.
Kujitolea hujumuisha hiari, 
umoja, utu na kuaminiana na kunatoa fursa muhimu katika kupambana na 
maradhi, ujinga, umasikini, hifadhi ya mazingira na maeneo mengi ya 
kimaendeleo ambayo yanahitaji msukumo.
Aidha, kujitolea kunatoa mchango
 muhimu katika kushughulikia majanga pale yanapotokea, kuimarisha umoja 
katika jamii na kuboresha maisha ya watu.
Tanzania kama sehemu ya jamii ya
 Kimataifa itaadhimisha siku hiyo katika katika ukumbi wa Chuo cha 
Utalii kilichopo karibu na Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM),saa mbili 
na nusu asubuhi.
Kaulimbiu ya Maadhimisho hayo mwaka huu ni ‘Ushiriki na Ushirikishwaji katika kuleta maendeleo  katika ngazi zote za mitaa, taifa na kimataifa.’
Katika maadhimisho hayo, 
wananchi hasa vijana watashiriki katika mdahalo kuhusu umuhimu wa 
kujitolea kwa ajili ya kuleta maendeleo. Aidha, kutakuwa na shuhuda na 
maonyesho ya taasisi zinazoshiriki katika shughuli za kujitolea ili 
kuhamasisha na kufufua moyo wa kujitolea miongoni mwa jamii.
Watanzania hususan Vijana 
wanahamasishwa kuibua shughuli za kujitolea na kushiriki katika zile 
zilizokwisha anzishwa  ikizingatiwa kuwa wao ndiyo nguvu kazi kubwa ya 
jamii.
Wizara ya Habari, Vijana, 
Utamaduni na Michezo inawakaribisha wananchi wote kushiriki katika 
maadhimisho hayo muhimu ili kushiriki katika mdahalo huo na kujionea 
jinsi watu mbalimbali wanavyotoa mchango mkubwa katik jamii kupitia 
shughuli za kujitolea.

No comments:
Post a Comment