Mratibu
 wa Uhurumarathon Tanzania Innocent Melleck akizungumza na waandishi wa 
habari jijini Dar Es Salaam juu ya kukamilika kwa maandalizi yam bio 
hizo zinazotarajiwa kufanyika jumapili hii jijini Dar Es Salaam katika 
viwanja vya Leders Club kushoto ni katibu mkuu wa shirikisho la Riadha 
la Taifa Selemani Nyambui.
………………………………………………..
Na Mwandishi Wetu
MAANDALIZI ya mbio za Uhuru, Uhuru
 Marathon, zinazotarajiwa kufanyika kesho jijini Dar es Salaam 
yamekamilika, huku wanaridha kadhaa kutoka ndani na nje ya nchi 
wakithibitisha kushiriki mbio hizo zenye lengo la kuulinda uhuru wetu, 
kudumisha umoja, amani, upendo na mshikamano miongoni mwa Watanzania.
Akizungumza na waandishi wa habari
 jana, Mratibu wa Uhuru Marathon, Innocent Melleck alisema, maandalizi 
yote yamekamilika, huku wanariadha wa hapa nchini kutoka nje ya Dar es 
Salaam wakiwa wamewasili tayari kwa ushiriki wao.
Melleck pia alisema, kwa 
kushirikiana na Jeshi la Polisi ulinzi umeimarishwa kwa kiwango kikubwa 
ili kuhakikisha usalama unakuwa mkubwa kwa washiriki wote na barabara 
zitakazotumika zitafungwa katika kipindi hicho.
“Kila kitu kimekamilika na 
washiriki kutoka nje ya Dar es Salaam wameanza kuwasili kwa ajili ya 
mbio hizo na tunawahakikishia usalama utakuwa mkubwa mno katika kipindi 
chote cha mbio hizo n mpaka kufikia jana (juzi) tayari washiriki 
waliojitokeza walikuwa 4000,” alisema.
Katibu Mkuu wa Chama cha Riadha 
Tanzania (RT), Selemani Nyambui alisema, wanariadha maarufu wa hapa 
nchini watakaoshiriki ni pamoja na Fabian Joseph na Dickson Marwa, huku 
Jacqueline Sekini aliyeshinda mbio hizo kwa upande wa wanawake mwaka 
jana, naye akiapa kutetea ubingwa wake.
“Wapo wanariadha wengi 
watakaoshiriki, lakini nataka kutoa angalizo kwa wanariadha kutoka 
Kenya, sisi tumetumwa mwaliko kwa wa chama husika na wao ndio watutumia 
majina ya wanariadha kumi, watano wa kiume na waliobaki wa kike, 
hatutapokea mwanariadha kutoka nchi hiyo ambaye hatujapewa jina lake,” 
alisema.
Nyambui alisema, tayari waamuzi 
watakaosimamia mbio hizo wapo tayari na akasisitiza ni lazima taratatibu
 zote zitafuatwa ili kupata mshindi halali.
Mbio hizo zinatarajiwa kuanzia 
viwanja vya Leaders Club na zitakuwa za kilomita 21, kilomita 5 na 
kilomita 3 ambazo ni maalumu kwa ajili ya viongozi wa kitaifa, dini na 
taasisi mbalimbali.
Aidha Melleck alisema, tayari namba kwa washiriki zimeanza kutolewa na wanaweza kuzipata katika viwanja vya Leaders Club.
Mgeni rasmi katika mbio hizo anatarajiwa kuwa Rais Jakaya Kikwete.
No comments:
Post a Comment