Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mh, 
Mwantumu Mahiza siku ya jumamosi wiki hii anatarajia kuongoza Bonanza la
 Wanavyuo linaloendea sehemu mbali mbali na ikiwa ni sehemu ya tatu kwa 
kanda ya kaskazini inayoendelea lwemye viwanja mbali mbali chini ya 
Kampuni ya Miss Demokrasia Tanzania & Entertainment C.o Ltd kwa 
kushirikiana na kituo bora cha Matangazo TIMES FM 100.5.
Bonanza hilo ambalo ni kwa ajili ya kupata timu zitakazoshiriki 
michuano ya NACTE linatarajiwa kuwa gumzo kwa mkoa wa Pwani kutokana na 
mfumo wake uliobuniwa kiufundi na waandaaji ambapo timu mbali mbali za 
Viongozi wa Serikali na zile za mkoa upata fulsa ya kushiriki pamoja kwa
 kufanya michezo ya soka, kikapu,netball pamoja na Voleyball.
Akizungumzia bonanza la jumamosi Mratibu wa Michezo Vyuoni, 
Mpalule Shaaban alisema kuwa Mh, Mwantumu anatarajia kufanya Uzinduzi wa
 Michezo hiyo kwa Mkoa wa Pwani kutokana na kwamba sasa Michezo hiyo 
itafanyika kila mwaka Sehemu mbali mbali za Tanzania.
“Ni heshima ya pekee ambayo Serikali imetoa kwa Vijana wetu wa 
vyuo vya elimu ya kati kushiriki michezo, kumbuka kwamba michezo hii 
aijawahi kuwepo tangu NACTE imeanzishwa hivyo hii ni fulsa ya pekee 
tuliyonayo katika kuhakikisha kwamba tunahamasisha michezo hii wakati 
wote ili vijana wanaojiunga na Vyuo vya Elimu ya Ufundi, Veta, na wale 
wa ngazi ya Diploma kushiriki michezo vyuoni”alisema Mpalule.
Sehemu ya pili imefanyika mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya 
ustawi wa jamii kijitonyama tarehe 29/11/2014, ambako Vyuo mbalimbali 
vya NACTE mkoa wa dar es salaam, vilicheza katika michezo ya soka, 
Basketball, Voleyball na netball,katika kutafuta timu zitakazoshiriki 
ligi ya NACTE Tanzania katika msimu wa 2014/2015.
sehemu ya kwanza Ilizinduliwa kwenye chuo cha DIT tarehe 
22/11/2014 mwezi huu na kusisimua wengi katika Michuano lutokana na kuwa
 na mfumo wa mtoano kuwa kivutio kwa Wachezaji na Mashabiki ambao wengi 
wao ni wanafunzi kutoka vyuo mbali mbali wanaofika kushuhudia michuano 
hiyo inayoendeshwa kwa ubunifu wa hali ya juu.
 Vyuo vilivyokwisha cheza ni Institute of Adult Education, 
Institute of Social Work (ISW) – DSM, Lugalo Military Medical School – 
Dsm, St. Joseph College (University), Dar es salaam City College 
(DACICO, Dar-es-Salaam School of Journalism (DSJ) – DSM, National 
Institute of Transport (NIT) – DSM, Bandari College – DSM,huku timu 
mwalikwa ikiwa ni Timu ya wafanyakazi wa PPF Dsm.
Vyuo vingine ambavyo tayari 
vimemaliza michezo yao ya awali ni pamoja na IFM ,DIT, CBE, 
Muhimbili,TRA, Mlimani Profesianal,na Royal College, waliokuwa kundi la 
kwanza lililofanyika viwanja vya chuo cha DIT akiba Posta.
Aidha vyuo vyote vinavyohusika na michezo ya wiki hii zimetakiwa
 kuwahi Viwanjani ili kukamilisha taratibu za ukaguzi kabla ya michuano 
hiyo ya mtoano kuanza na ikumbukwe kwamba michuano hiyo inaendeshwa kwa 
mfumo wa Bonanza na inafanyika kila siku za jumamosi kutokana na 
wanafunzi kuwa masomoni katika siku za kawaida.
kila mwaka michuano hii itakuwa ikifanyika kwa kushirikisha vyuo
 mbali mbali vya elimu ya kati hapa nchini Tanzania na vilivyopata 
usajili wa kudumu wa NACTE ambapo Kanda mbali mbali za Tanzania kupitia 
vyuo vyao vitashindana katika michezo mbali mbali kwa wavulana na 
wasichana ni vyuo 32 tu vitakavyokuwa vikishiriki baada ya kufanya 
mchujo wa awali kwa njia ya Bonanza na Timu mbili za juu kila BONANZA 
ndizo zitakazokuwa zikiingia katika idadi ya vyuo 32 vya NACTE ITER 
COLLEGE DAR ES SALAAM.
Ukiachilia mbali michezo hiyo, michezo mingine itakayokuwa 
ikifanyika kati ya wanafunzi na wanafunzi ni DEBATE, Marathon, Modoling,
 Mashindano ya Vipaji kwa viongozi wanaosimamia serikali za wanafunzi 
kwa nafasi za Rais na Makamu, Waziri Mkuu, Mawaziri wa Michezo,Fedha, na
 Spika , watakaokuwa wakichuana katika kujielezea, kujibu maswali, na 
kuelezea Mada katika nafasi zao na changamoto wanazokabiliana nazo na 
washindi watakuwa wakipata tuzo mbali mbali kulingana na ushindi wa kila
 mmoja.
Wadhamini aliojitokeza mpaka sasa na kuonyesha nia ya kusaidia 
mashindano hayo ni pamoja na Coca Cola, Vodacom, MLONGE BY MAKAI, CXC 
–Tours,Bonga Resort & Hoteli, Ikondolelo Hoteli, na 100.5 Times 
Fm. 
 lakini hata hivyo dirisha la wadhamini bado liko wazi kwa maana
 bado gharama ni kubwa za uendeshaji ambapo wajitokeze waweze kusaidia 
michezo hii iliyoanza kwa shamrashamra nyingi na kuwa na mvuto kwa 
watazamaji ususani wanafunzi wa vyuo mbalimbali waliojitokeza.

No comments:
Post a Comment