TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, December 4, 2014

MAADHIMISHO YA SIKU YA KIMATAIFA YA KUJITOLEA DUNIANI

Siku ya Kimataifa ya Kujitolea Duniani huadhimishwa tarehe 5 Desemba kila mwaka kwa lengo la kutambua mchango wa kujitolea unaotolewa kwa ajili ya maendeleo katika jamii tunamoishi, kitaifa na kimataifa. Kujitolea hujumuisha hiari, umoja, utu na kuaminiana na kunatoa fursa muhimu katika kupambana na maradhi, ujinga, umasikini, hifadhi ya mazingira na maeneo mengi ya kimaendeleo ambayo yanahitaji msukumo.
Aidha, kujitolea kunatoa mchango muhimu katika kushughulikia majanga pale yanapotokea, kuimarisha umoja katika jamii na kuboresha maisha ya watu.
Tanzania kama sehemu ya jamii ya Kimataifa itaadhimisha siku hiyo katika katika ukumbi wa Chuo cha Utalii kilichopo karibu na Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM),saa mbili na nusu asubuhi. Kaulimbiu ya Maadhimisho hayo mwaka huu ni ‘Ushiriki na Ushirikishwaji katika kuleta maendeleo katika ngazi zote za mitaa, taifa na kimataifa.’
Katika maadhimisho hayo, wananchi hasa vijana watashiriki katika mdahalo kuhusu umuhimu wa kujitolea kwa ajili ya kuleta maendeleo. Aidha, kutakuwa na shuhuda na maonyesho ya taasisi zinazoshiriki katika shughuli za kujitolea ili kuhamasisha na kufufua moyo wa kujitolea miongoni mwa jamii.
Watanzania hususan Vijana wanahamasishwa kuibua shughuli za kujitolea na kushiriki katika zile zilizokwisha anzishwa ikizingatiwa kuwa wao ndiyo nguvu kazi kubwa ya jamii.
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo inawakaribisha wananchi wote kushiriki katika maadhimisho hayo muhimu ili kushiriki katika mdahalo huo na kujionea jinsi watu mbalimbali wanavyotoa mchango mkubwa katik jamii kupitia shughuli za kujitolea.

No comments:

Post a Comment