Siku ya Kimataifa ya 
Kujitolea Duniani huadhimishwa tarehe 5 Desemba kila mwaka kwa lengo la 
kutambua mchango wa kujitolea unaotolewa kwa ajili ya maendeleo katika 
jamii tunamoishi, kitaifa na kimataifa.
 Kujitolea hujumuisha hiari, umoja, utu na kuaminiana na kunatoa
 fursa muhimu katika kupambana na maradhi, ujinga, umasikini, hifadhi ya
 mazingira na maeneo mengi ya kimaendeleo ambayo yanahitaji msukumo.
Aidha, kujitolea kunatoa mchango 
muhimu katika kushughulikia majanga pale yanapotokea, kuimarisha umoja 
katika jamii na kuboresha maisha ya watu.
Tanzania kama sehemu ya jamii ya 
Kimataifa itaadhimisha siku hiyo katika katika ukumbi wa Chuo cha Utalii
 kilichopo karibu na Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM),saa mbili na nusu
 asubuhi.
 Kaulimbiu ya Maadhimisho hayo mwaka huu ni ‘Ushiriki na 
Ushirikishwaji katika kuleta maendeleo katika ngazi zote za mitaa, taifa
 na kimataifa.’
Katika maadhimisho hayo, wananchi 
hasa vijana watashiriki katika mdahalo kuhusu umuhimu wa kujitolea kwa 
ajili ya kuleta maendeleo. Aidha, kutakuwa na shuhuda na maonyesho ya 
taasisi zinazoshiriki katika shughuli za kujitolea ili kuhamasisha na 
kufufua moyo wa kujitolea miongoni mwa jamii.
Watanzania hususan Vijana 
wanahamasishwa kuibua shughuli za kujitolea na kushiriki katika zile 
zilizokwisha anzishwa ikizingatiwa kuwa wao ndiyo nguvu kazi kubwa ya 
jamii.
Wizara ya Habari, Vijana, 
Utamaduni na Michezo inawakaribisha wananchi wote kushiriki katika 
maadhimisho hayo muhimu ili kushiriki katika mdahalo huo na kujionea 
jinsi watu mbalimbali wanavyotoa mchango mkubwa katik jamii kupitia 
shughuli za kujitolea.

No comments:
Post a Comment