ZIARA YA KINANA MIKOA YA LINDI NA MTWARA YAINGIZA  WANACHAMA ZAIDI YA 40,000 CCM 
Wakazi
 wa Mtwara mjini wakishangilia wakati wa mkutano wa hadhara wa CCM 
ukiongozwa na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa 
Mtwara mjini kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa 
Mashujaa ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa kazi ya CCM ni kuisimamia 
Serikali kutimiza wajibu wake kwa wananchi.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Mtwara mjini na kuwaa
 Mbunge
 wa Mtwara Mjini Ndugu Hasnain Murji akieleza utekelezaji wa ilani ya 
CCM ulivyotekelezwa vizuri kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye 
viwanja vya Mashujaa ambapo pia alieleza changamoto zinazowakabili 
wananchi wa Mtwara mjini hivyo kumtaka Katibu Mkuu wa CCM Ndugu 
Abdulrahman Kinana kusaidia katika kufanikisha baadhi ya mambo ambayo 
yameonekana kukwamishwa na viongozi wa juu serikalini.
 Wananchi
 wakilizunguka gari alilopanda Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman 
Kinana mara baada ya kumaliza kuhutubia kwenye viwanja vya Mashujaa 
Mtwara mjini.
MAPOKEZI YA KINANA MTWARA MJINI
 
 Vijana wa Bodaboda wakiongoza msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu 
Abdulrahman Kinana wakati akiwasili Mtwara mjini ambapo alishiriki 
shughuli mbali mbali za kujenga na kuimarisha chama pamoja na kukagua 
utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM 2010.
     Msafara wa Katibu Mkuu ukielekea Mtwara mjini.
 Katibu
 Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Mikindani 
mara baada ya kukabidhi leseni kwa madereva 70 wa boda boda waliohitimu 
mafunzo chini ya udhamini wa Mbunge wa Mtwara mjini Hasnain Murji.
                                                   MTWARA VIJIJINI 
 Wananchi
 wa kijiji cha Kitaya mkoani Mtwara wakishangilia ujio wa Katibu Mkuu wa
 CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye kijiji hicho kinachopakana na nchi 
ya Msumbiji.
 
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kijiji
 cha Kitaya kilichopo mpakani na nchi ya Msumbiji ikiwa sehemu ya ziara 
yake mkoani Mtwara ambapo anakagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi 
pamoja na kujenga na kuimarisha chama.
 Katibu
 Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasalimu wakazi wa kata ya 
Nanguruwe ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa kuna sheria 
zinazomkandamiza mkulima inabidi zitazamwe upya kwani zisipobadilishwa 
mkulima atakuwa anakandamizwa kila siku na kutoona faida ya kuwa mkulima
 wa korosho.
  
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Ndugu Nape Nnauye 
akiwasalimia wakazi wa kata ya Nanguruwe wakati wa ziara ya Katibu Mkuu 
wa CCM kwenye wilaya ya Mtwara Vijijini,tarehe 28 Novemba 2014.
Katibu
 Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa kwenye mnara wa shujaa 
Ahamad Mzee aliyepambana na Wareno waliokuwa wanataka kuivamia Tanzania 
mwaka 1972 mpakani mwa Tanzania na Msumbiji.
                                                          TANDAHIMBA 
 
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa 
Tandahimba ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa zao la korosho lina 
hadithi nyingi sana na njia pekee ya kuleta ukombozi kwa mkulima ni 
kujenga kwa viwanda vya kutosha vya kubangulia Korosho nchini pia 
aliwataka wazazi wa Tandahimba kusisitiza elimu kwa watoto wao kwani 
ndio mkombozi pekee atakayekuja kuwakomboa kwenye maisha yao.
 
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Nape Nnauye akihutubia wakazi wa 
Tandahimba ambapo aliwaambia wasihadaike na wapinzani ambao muda wao wa 
ujana wameutumia wakiwa CCM na uzeeni kuingia upinzani na kuanza kuhadaa
 watu walioishi kwa amani kwa muda mrefu.
 
 Wananchi wa Tandahimba mkoani Mtwara wakifuatilia kwa makini hotuba za 
viongozi wa CCM wakiongozwa na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman 
Kinana ambaye anazunguka nchi nzima kukagua na kuimarisha uhai wa Chama.
 Katibu
 Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi wa kata ya 
Mndimba wakati waujenzi wa ofisi ya CCM kata ya Mdimba wilayani 
Tandahimba.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akionyesha kadi zilizorudishwa na wapinzani kata ya Mdimba wilaya ya Tandahimba.
                                                   NEWALA 
 
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwaonyesha wananchi wa 
Mkwedu kadi ya CUF iliyorejeshwa kwake na Hakika Ibrahim ambaye 
alirudisha kadi hiyo baada ya kuona na kuelewa utekelezaji wa ahadi za 
CCM unavyokwenda vizuri.
 Katibu
 Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akionnyesha kadi juu zilizorudi 
kutoka upinzani ambapo wanachama hao kutoka upinzani wameahidi 
kushirikiana na CCM kwa ajili ya kuleta maendeleo yaTengulengu wilayani 
Newala.
 Aliyekuwa
 Makamu Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Newala Ndugu  Adam Lawi 
Nangwanda Sijaona akivua nguo za Chadema mbele ya Katibu wa NEC Itikadi 
na Uenezi CCM Ndugu Nape Nnauye.
 Wananchi
 wakishangilia kurejea kwa  Aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Chadema 
wilaya ya Newala Ndugu  Adam Lawi Nangwanda Sijaona kwenye mkutano wa 
hadhara uuliofanyika kwenye viwanja vya Mahakama ya mwanzo Newala
 Katibu
 Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Newala kwenye
 viwanja vya Mahakama ya Mwanzo ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa 
Serikali lazima itafute namna ya kuhakikisha uzalishaji wa korosho wote 
unafanyika nchini kwa kujenga viwanda vya kutosha vya korosho.
Aliyekuwa
 Makamu Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Newala Ndugu  Adam Lawi 
Nangwanda Sijaona akiwa amekabidhi kadi yake na ya mkewe kwa Katibu Mkuu
 wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana .
                                                       NANYUMBU 
 Katibu
 Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Mangaka  
wilaya ya Nanyumbu ambapo aliwaambia CCM ya sasa itakuwa kali kuliko 
wakati wowote na itaisimamia serikali na kuipongeza inapofanya vizuri na
 itakapofanya vibaya itasemwa.
No comments:
Post a Comment