TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, December 3, 2014

Kamati ya Kusimamia Tuzo za Wanamichezo Bora Tanzania yatangaza majina ya wanaowania tuzo hizo.

asa
Katibu Mkuu wa TASWA Bw. Amir Mhando akizungumza na waandishi wa habari kwenye mgahawa wa City Sports Lounge wakati kamati hiyo ilipotangaza wanamichezo watakaowania tuzo ya mwanamichezo bora wa mwaka inayoandaliwa na Chama cha waandishi wa habari za michezo TASWA, kutoka kulia ni Mahmoud Zuberi Makamu Mwenyekiti wa kamati na katikati ni Rehure Nyaulawa Mwynekiti wa kamati hiyo.
…………………………………………………………………………………………….
KAMATI ya Kusimamia Tuzo za Wanamichezo Bora Tanzania zinazotolewa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) ilikutana Dar es Salaam jana na kupitia majina ya wanamichezo waliopendekezwa kuwania tuzo hizo.
 
Tuzo itafanyika Desemba 12 mwaka huu ukumbi wa Diamond, Jubilee (VIP), Dar es Salaam, ambapo wanamichezo mbalimbali waliofanya vizuri kati ya Juni 2013 hadi Juni 2014 watakabidhiwa tuzo zao.
 
Ni imani yetu kwamba zaidi ya wanamichezo 40 watakabidhiwa tuzo zao siku hiyo, ambapo kamati imejiridhisha kwamba wanaowania tuzo hiyo wanastahili kulingana na mapendekezo ya vyama vya michezo kupitia Kamati zao za Ufundi.
 
Mshindi wa kila tuzo ataingia katika mchakato wa kumpata Mwanamichezo Bora wa Tanzania wa mwaka 2013/2014, ambapo pia siku hiyo ya sherehe za tuzo itatangazwa zawadi ya Tuzo ya Heshima kwa yule ambaye itaonekana alikuwa na mchango mkubwa katika masuala mbalimbali ya kimichezo hapa nchini. Tuzo hizo ni kuanzia Juni 2013 hadi Juni 2014.
 
ORODHA KAMILI YA WANAOWANIA TUZO ZA TASWA 2013/2014
 
OLIMPIKI MAALUM:
Wanaume: Raphael Kalukula, Pazi Mwinyimkuu na Hatibu Matali
wanawake: Blandina Blasi, Shida Jaha na Mwanaharusi Risasi.
MPIRA WA KIKAPU;
Wanaume:Lusajo Samwel (Oilers), Erick Mchemba (ABC)
wanawake:Sajda Ahmed Lyamaiga(Don Bosco Lioness), Rehema Silomba (Don Bosco Lioness) na Orlyn Titus (Don Bosco Lioness).
 
MPIRA WA MAGONGO;
Wanaume:Yohana Wilson, Focus Paul, Deep Vaja
Wanawake: Valentina Quarantta, Kidawa Seremala na Mary Mhina
MPIRA WA WAVU: Wanawake: Yasinta Remmy (Jeshi Stars), Hellena Richard (Magereza) na Teddy  Abwao (Jeshi Stars).
WanaumE: Kelvin Peter Severino (Magereza), Nassoro Sharifu (Jeshi Stars) na Athuman Rupia (Jeshi Stars).
 
RIADHA:
Wanawake: Zakia Mrisho, Jaqueline Sakilu na Catherine Lange
Wanaume:Alphonce Felix, Dickson Marwa na Fabian Nelson.
Continue reading →

No comments:

Post a Comment