TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, December 5, 2014

Kampuni za simu Tanzania zashirikiana na AU ‘kutokomeza Ebola barani Afrika’

ttttttttttt
Meneja wa Uwajibikaji kwa Jamii kutoka Tigo Bi. Woinde Shisael (katikati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na kampeni maalum ya kampuni za simu tatu nchini zilizoungana kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia kutokomeza ugonjwa wa Ebola Afrika. Kushoto ni Mkuu wa Mawasliano na Mahusiano ya Umma kutoka Vodacom Bi. Rosalynn Mworia, na Meneja wa Huduma za Kijamii kutoka Airtel Bi. Hawa Bayumi (kulia). Kuchangia mteja yeyote wa kampuni hizo tatu tajwa anaweza akatuma neno ‘Tokomeza Ebola’ kwenda 7979
Kampuni za simu nchini Tanzania zimeingia katika ushirikiano na Tume ya Umoja wa Afrika (AU Commission) ili kuendeleza vita dhidi ya ugonjwa wa Ebola unaoendelea kutishia amani nchi za Afrika Magharibi. Ushirikiano huo unaojulikana kama ‘AfricaAgainstEbola’ (AfrikaDhidiYaEbola) itatumia mtindo wa ujumbe wa kiganjani (SMS) kuweza kuchangisha fedha kwa ajili ya kuwawezesha watalaam wa afya kutoka Afrika kuweza kwenda na kuhudumia nchi zilizo athirika.
Watu zaidi ya 5,000 wameshapoteza maisha kutokana na ugonjwa wa Ebola kutoka sehemu mbali mbali Afrika Magharibi tangu ugonjwa huo kulipuka kwa mara ya kwanza nchini Guinea mwezi Machi 2014. Kutokana na taarifa za Shirika la Afya Duniani (WHO) huu ni mlipuko mkubwa zaidi kuwahi kutokea katika bara hili ambayo kwa sasa ugonjwa huo umeshatapakaa katika nchi nne zikiwemo – Guniea, Liberia, Sierra Leone na Mali.
Katika mkutano wa kibiashara uliofanyika hivi karibuni chini ya AU, kampuni za simu zilijitolea kuanzisha kampeni maalum ya bara nzima ijulikanayo kama “United Against Ebola” (Pamoja Dhidi ya Ebola). Kampeni hii itakusanya michango kutoka kwa wateja wa kampuni mbali mbali za simu, na fedha hizo zitakazo kusanywa katika muda wa miezi mitatu, zitatumika katika mapambano dhidi ya kirusi hiki cha Ebola.
Akizungumzia kuhusu mpango huu hivi karibuni, Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, Mheshimiwa Yayi Boni, Rais wa Jamhuri ya Benin, alisema: Tunayofuraha kuungana na kampuni za mawasiliano ya simu katika jitihada hizi. Mlipuko huu wa ugonjwa wa Ebola ni hali ya hatari kwa wanadamu, ni janga kwa familia zilizo athirika na tishio kwa ustawi wa uchumi ulioweza kufikiwa na nchi husika.
Aliendelea, “Hatuwezi tukakaa bila kufanya lolote. Tunaamini kwamba kwa ushirikiano wa sekta binfasi tunaweza kwa pamoja kutokomeza ugonjwa huu wenye malengo wa kuangamiza bara la Afrika

No comments:

Post a Comment