TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, December 2, 2014

Msimu wa pili wa tamthilia Siri ya Mtungi Wazinduliwa

unnamed2Muongozaji wa tamthilia hiyo, Karabani akisisitiza jambo katika mkutano huo.
………………………………………………………………………..
Na Mwandishi Wetu
Msimu wa pili wa tamthilia ya Siri ya Mtungi itazinduliwa rasmi Desemba 7 kupitia televisheni ya Taifa (TBC).
Akizungumza jijini jana, Mtayarishaji wa tamthilia hiyo, Louise Kamin kutoka  Shirika Lisilo la Kiserikali la  Media for Development International Tanzania (MFDI-TZ) alisema kuwa sehemu ya pili ya tamthilia hii inakamilisha Siri ya Mtungi kufuatia msisimko mkubwa wa msimu wa kwanza.
Kamin alisema kuwa kukamilika kwa hatua ya pili kunatokana na udhamini mnono wa the John Hopkins University Centre for Communication Programs (JHU CCP) ambao walitoa uongozi wa elimu na mkakati katika tamthilia, taasisi ya Misaada ya Wamarekani kupitia (Usaid), Wizara ya Afya Ustawi wa Jamii na MFDI.
Alisema kuwa sehemu hii ndiyo inatoa majibu ya msimu wa kwanza na kuwataka mashabiki watamthilia hii kuangalia TBC kuanza saa 12.30 jioni kupitia TBC.
“Msimu wa kwanza wa tamthilia ya Siri ya Mtungi uliwavutia watu wengi wa ukanda wa Afrika Mashariki na kuwaachia maswali kibao na hii imetokana na tamthilia kubeba vionjo halisi vya maisha katika jamii na hasa kwa wakazi wa mikoa ya Pwani ya Tanzania,” alisema Kamin.
Alisema kuwa mapokeo mazuri kutoka kwa watazamaji kuliwapa nafasi ya kuingia katika vipengele saba vya tuzo za M-Net Africa Magic Viewers Choice Awards mwaka 2014 ambavyo ni TV Series, Make Up, Wardrobe, Art Direction, Sound Editor, Acting, and Indigenous Language Series.
“Msimu wa kwanza ulikuwa hewani katika vipindi vya miaka miwili tangu mwezi Desemba mwaka jana kupitia vituo vya televisheni vya ITV/EATV na baadaye kurushwa hewani kupitia DTV, TV1, MNet Africa Magic, Maisha Magic kabla ya msimu huu kupitia televisheni ya TBC,” alisema.
Kwa mujibu wa Kamin, mpaka sasa wanajivunia kupata mapokeo mazuri kwenye mitandao ya kijamii na hasa facebook kwa kupata mashabiki 200,000 na kwenye YouTube ambapo tumepata watazamaji zaidi ya 500,000 kwani tamthilia hii imepata umaarufu mkubwa kwa kutazamwa na mashabiki wengi kuliko vipindi mbali mbali vya televisheni hapa nchini na ukanda wa Afrika Mashariki.
Alisema kuwa Siri ya Mtungi ni hadithi ya Kitanzania ambapo wametumia siku 86 kukamilisha kurekodi. Alisema mbali ya kuwashirikisha waigizaji maarufu kama yvonne Cherie maarufu kwa jina la Monalisa, pia imewashirikisha warembo maarufu kutoka Miss Tanzania kama Richa Adhia na Jokate Mwegelo.
“Tumetoa ajira kwa waigizaji 60 ambao walipatikana baada ya mchujo wa watu 2,500,” alisema.

No comments:

Post a Comment