WAZIRI DR. FENELLA MUKANGARA AKUTANA NA JUKWAA LA WAHARIRI
 
           
       
       
       
         
       
       
        
Waziri
 wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara 
akiwaeleza wahariri wa vyombo vya habari nchini wajibu na umuhimu wa 
vyombo vya habari katika mchakato huu wa upatikani wa katiba mpya 
ikiwemo kutoa elimu kuhusu umuhimu wa mchakato huu kwa mustakabali wa 
Taifa pia alivipongeza vyombo vya habari katika elimishaji wa wananchi 
katika mchakato wa Bunge Maalum la Katiba, Wakati wa Mkutano na Wahariri
 wa Vyombo vya Habari jana Jijini Dar es Salaam. 
Mwenyekiti
 wa Jukwaa la wahariri Absalom Kibanda akiongea wakati wa mkutano 
uliowakutanisha wahariri wa vyombo na Waziri wa Habari, Vijana, Utamduni
 na Michezo ambapo Dkt. Fenela Mukangara ambapo waliwataka wahariri kuwa
 wamoja katika masuala ya kitaifa hasa yatakayopelekea kuibomoa nchi 
yetu pia aliwaasa wahariri kutumia kalamu zao vizuri kuwaelimisha 
wananchi katika mchakato huu wa kuelekea upatikaji wa Katiba Mpya 
kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari Bw. Assah Mwambene, Naibu
 Waziri Wizara ya Katiba na Sheria Mh.Angela Kairuki na Mwisho ni Waziri
 wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara jana 
Jijini Dar es Salaam. 
Mzee
 Kingunge Ngombale-Mwiru akiongea na wahariri wa vyombo vya habari 
ambapo ambapo aliwaeleza kuhusu umuhimu wa upatikanaji wa katiba mpya 
kwa maendeleo ya Taifa ikiwa katiba iliyopendekezwa imezingatia Masuala 
muhimu ya ukuzaji uchumi wan chi pia uzingatiaji wa makundi mbalimbali 
katika jamii na alisisitiza umuhimu wa vyombo vya habari kuendelea kutoa
 elimu kuelekea upatikanji wa katiba mpya kwani katiba ni chombo cha 
ukombozi wa nchi. 
Mwenyekiti
 wa Jukwaa la wahariri Absalom Kibanda akisamiana na Mzee Kingunge 
Ngombale-Mwiru wakati wa mkutano wa wahariri wa vyombo vya Habari na 
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara. 
Mh.
 Hamadi Rashid Muhamed akiwaeleza wahariri wa vyombo vya habari ambapo 
alieleza furaha yake kwa katiba inayopendekezwa kujikita katika kutatua 
changamoto za muungano zitakazopekea kuimarika kwa muungano wa Tanzania 
bara na Zanzibar. 
 
Baadhi wa Wahariri wa Vyombo vya Habari nchini Wakifuatilia Mada zilizokuwa zinawasilishwa katika mkutano huo 
 
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment