TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, January 23, 2015

Harakati za kuhamasisha vijana zawafikia Vijana wa Mbozi.

 unnamed (29) Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya Mbozi Bw. Elisey Ngowi akifungu semina ya Ujasiriamali, Stadi za Maisha, Ujuzi na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana iliyoandaliwa na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo hivi karibuni katika Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Mbeya. Kushoto ni Mwezeshaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa na kulia ni Afisa Vijana kutoka Wizara hiyo Bi. Amina Sanga.
unnamed (30)Vijana wa Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Mbeya wakisikiliza kwa makini mafunzo yaliyokua yakitolewa wakati wa semina ya Ujasiriamali, Stadi za Maisha, Ujuzi na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana iliyoandaliwa na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo hivi karibuni katika Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Mbeya.
unnamed (31)Mwezeshaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa kulia akifafanua jambo walipotembelea mradi wa kikundi cha vijana cha Miranaco wanaomiliki duka la madawa muhimu katika Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Mbeya. Kushoto ni Afisa Utamaduni Wilaya ya Mbozi Bw. Godfrey Msokwa, wapili kushoto ni Mkuu wa Kituo cha Vijana Sasanda Mbeya Bw. Laurean Masele na wapili kulia ni Mwenyekiti wa kikundi cha Miranaco Bw. John Maige. (Picha zote na: Genofeva Matemu – Maelezo)
…………………………………………………………….
Na: Genofeva Matemu – Maelezo, Mbeya Tarehe 22/01/2015 Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi imeshauriwa kupeleka vijana wa wilaya hiyo katika Vituo vya Vijana kupata mafunzo mbalimbali ili kuweza kupata mbinu mbadala za kiujasiriamali. Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Kituo cha Vijana Sasanda Bw. Laurean Masele wakati wa semina ya Ujasiriamali, Stadi za Maisha, Ujuzi na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana hivi karibuni katika Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Mbeya. Bw. Masele amesema kuwa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo inasimamia Kituo cha Vijana Sasanda Mbeya kinachotoa mafunzo ya ujasiriamali katika fani za Kilimo na Ufugaji, Kituo cha Vijana cha Ilonga Morogoro kinachotoa mafunzo katika fani ya teknolojia ya habari na mawasiliano na Kituo cha Vijana cha Marangu Moshi kinachotoa mafunzo ya uthubutu/ujasiri kwa vijana. Aidha Bw. Masele amesema kuwa moto uliowashwa na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kuhamasisha vijana mbinu za kiujasiriamali unalenga kuwajengea vijana ujasiri wa kuthubutu na kufikia malengo waliyojiwekea. Akizungumza wakati wa kufungua semina hiyo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi Bw. Elisey Ngowi amewataka vijana kuzingatia elimu inayotolewa na kuifanyia kazi kwani vijana bado wanauwezo mkubwa wa kufikiri hivyo kutumia akili nyingi na nguvu nyingi kufanya mambo mbalimbali kwa maendeleo ya Wilaya hiyo. Kwa upande wake kijana Yohana Chaula kutoka kikundi cha Bodoboda B. Mloo Wilaya ya Mbozi amesema kuwa kundi la vijana wasiokua na ajira kwa sasa linazidi kuongezeka hivyo kuiomba Wizara inayosimamia masuala ya Vijana kuongeza fungu katika Mfuko wa Maendeleo ya Vijana ili vijana wote nchini waweze kunufaika na Mfuko huo. Naye mwakakikundi wa kikundi cha Umoja wa Vijana Wilaya ya Mbozi Bw. Chemli Ndema ameushukuru ujumbe kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kufika Wilaya ya Mbozi na kutoa elimu ya ujuzi kwa vijana kwani elimu aliyoipata katika semina hiyo imemtoa katika giza nene na kukiri kuwa atakuwa chachu ya maendeleo na kiongozi bora katika jamii.

No comments:

Post a Comment