Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Ndugu Bruno Ghumpi 
……………………………………………………………………………………………..
Mtandao wa Malezi Makuzi na 
Maendeleo ya Watoto Wadogo Tanzania – TECDEN ni chombo kinachoundwa na 
mashirikia mbalimbali yanayofanya kazi za kuhudumia watoto wadogo 
Tanzania. Mtandao huu ulianzishwa mwaka 2000 na kusajiliwa rasmi mwaka 
2004. Makao makuu ya Mtandao huu yapo Jijini Dar es salaam. Hadi kufikia
 mwaka 2014 Mtandao huu una jumla ya mashirika wanachama wasioungua 200 
katika mikoa 14 ya Tanzania bara na Visiwani yanayotoa huduma kwa watoto
 wadogo Tanzania
 Lengo kuu la Mtandao ni kuboresha huduma za watoto wadogo Tanzania ili waweze kukua na kufikia utimilifu wao
Shughuli Kuu za Mtandao ni pamoja na:-
• Kufanya ushawishi na utetezi wa masuala yanayohusu uboreshaji 
wa huduma na kulinda haki za watoto wadogo ikiwa ni pamoja na kushawishi
 maboresho ya sera na kufuatilia utekelezaji wa sheria na miongozo 
mbalimbali inayohusu uboreshaji wa huduma kwa watoto wadogo Tanzania.
• Kuhamasisha jamii na watoa huduma kutambua umuhimu wa 
kuimarisha na kuwezesha watoto wadogo kupata mahitaji na haki zao za 
msingi. 
• Kuimarisha mifumo ya upashanaji habari na kuelimishana katika ngazi zote za huduma kwa watoto wadogo. 
• Kutafiti na kutumia matokeo ya utafiti katika kushauri uboreshaji wa huduma kwa watoto wadogo Tanzania.
Dhana ya Malezi Makuzi na Mendeleo ya Awali ya Mtoto (MMMAM)
Malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto ni istilahi ya 
jumla ya programu na vitendo vinavyoandaliwa kuwasaidia watoto (kuanzia 
mimba, kuzaliwa hadi miaka 8) ili kukua vizuri kimwili, kiakili, 
kijamii, kihisia, kimaadili na kiroho. Watoto wanahitaji kuchangamshwa 
katika nyaja na hatua zote za ukuaji, kiakili kwa michezo, kujifunza 
kuzungumza, kukaa, kutambaa, kutembea na kupatiwa fursa ya kuanza 
kujifunza mambo mbalimbali pamoja na utamaduni wao.
Utoaji wa huduma jumui za MMMAM.
Huduma hizi hujumuishwa ili kuwawezesha watoto wengi kupata 
huduma jumuishi za MMMAM zitolewazo na sekta mbali mbali katika mkabala 
jumui. Huduma hizi zinapaswa kupatikana kuanzia ngazi ya familia ,vituo 
vya afya ya msingi,vituo vya kulelea watoto mchana, vituo vya Malezi 
Makuzi ya awali ya mtoto vinavyomilikiwa na Jamii, madarasa ya awali na 
madarasa ya msingi hususani darasa la kwanza na la pili.
Katika kutekeleza shughuli zake 
Mtandao wa TECDEN umekuwa ukishirikiana na mashirika mbalimbali ya wabia
 wa maendeleo ikiwemo shirika la Children in Crossfire kutoka nchini 
Ireland na shirika la Better Way Foundation kutoka nchini Marekani
Ili kujua habari zaidi za TECDEN 
na masuala ya utoaji huduma kwa watoto wadogo na faida zake, unaweza 
kutembelea ofisi ya Mtandao makao makuu iliyopo Jengo la Posta mkabala 
na Wizara ya Mambo ya Ndani Nchi na Makao Makao Makuu ya Polisi jijini 
Dar es Salaam.
Unaweza pia kuwasiliana kwa njia 
ya simu au barua pepe na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Ndugu Bruno Ghumpi 
kwa namba 0754 690 556 na barua pepe ecdnetwork@gmail.com na ghumpibr@yahoo.com

No comments:
Post a Comment