![]()  | 
| Rais Kabila amekuwa mamlakani tangu mwaka 2001 | 
![]()  | 
| Waandamanaji wanamtuhumu Rais kwa kufanya wanachokiita mapinduzi ya kikatiba | 
Polisi katika Jamuhuri ya 
kidemokrasi ya Congo, wamefyatua risasi hewani ili kuwatawanya 
waandamanaji waliokuwa wamekusanyika katika mji mkuu Kinshasa kupinga 
sheria mpya ya uchaguzi.
Serikali inasema kuwa watu wanne 
walifariki katika vurugu za Jumatatu ingawa upinzani unasema idadi huo 
huenda ikwa kujuu kuliko iliyonakiliwa.
Wanafunzi wameweka vizuizi
 barabarani na pia wameshuhjudiwa wakichoma magurudumu, katika barabara 
zinazoelekea katika chuo kikuu mjini humo.
Wanatuhumu wanasia 
wanaomuunga mkono Rais Joseph Kabila ambaye muhulka wake wa pili 
unatarajiwa kumalizika mwaka ujao kwa kujaribu kujiongeza muda mamlakani
 kwa kuidhinisha mipango ya kufanyika sensa ambayo itachelewesha 
uchaguzi kwa miaka mingi.
Vurugu hizi zinashuhudiwa huku baraza la
 Senate likidadisi mswada ambao huenda ukasababisha Rais Kabila 
kuongezwa muda mamlakani.
Vijana walioandamana kwa vurugugu, waliteketeza magurudumu ya magari, kupora maduka na kurusha mawe.
Wanafunzi waliambia BBC kuwa polisi walivamia chuo chao baada ya wao kuanza kuandamana.
Walisema polisi walingia katika vyumba vyao na kuwafyatulia gesi ya kutoa machozi.
Viongozi
 wa upinzani walitoa wito kwa waandamanaji kwenda barabarani kupinga 
mipango ya serikali kumuongeza muda zaidi mamlakani Rais Joseph Kabila 
huku wakiutaja mpango huo kuwa mapinduzi ya kikatiba. 
Mswada huo unapendekeza kufanytika sensa kote nchini ambayo itachukua kipindi cha miaka mitatu.
Rais Kabila amekuwa mamlakani tangu mwaka 2001. Muhula wake wa pili unakamilika mwaka 2016 kikatiba. 


No comments:
Post a Comment