Chuo cha Ufundi Arusha(ATC) 
kinatarajiwa kutoa wahitimu wengi wa program ya teknolojia ya sanyansi 
za maabara ili kupata wataalamu wa kufundishia masomo ya sayansi kwa 
skuli za sekondari.
Hayo ni miongoni mwa ahadi za Mkuu
 wa Chuo hicho dkta Richard Masika wakati wa mahafali ya sita ya Chuo 
hicho yaliofanyika jijini hapa hivi karibuni.
Katika taarifa yake hiyo kwa naibu
 waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi Jenista Mhagama alisema kwa 
miaka mingi kuna upungufu wa walimu wengi wa masomo ya sanyansi na 
wataalamu wa masuala ya maabara katika skuli za sekondari.
Alisema hali hiyo inathiri kwa 
kiwango kikubwa ufundishaji wa masomo ya Sayansi kwa wafunzi wanaochukwa
 masomo hayo na kushindwa katika ufaulu kwa kukosa walimu wenye ubora.
“ kutokana kutambua hali hiyo chuo
 kikaamua kuanzisha mpango huo ilikuwapata wataalamu wengi zaidi ili 
kwenda sambamba na kupanuka kwa ujenzi wa sekondari hapa 
nchini”alitanabaisha dkta Masika.
Alisema kuwa skuli zinahitaji 
waalimu wengi zaidi wa masomo ya sayansi na wataalamu wa maabara,hivyo 
kwa kutambua umuhimu huo ndio maana tuanzisha mpango huo.
Alisema kuwa kutokana na chuo 
kutambua umuhimu huo ndio maana kikaanzisha Programu hiyo wa kutoa 
wataalamu hao wa maabara ilikuendana na mpango wa serikali wa matokeo 
makubwa sasa.
Pia alisema kutokana na hatua hiyo
 ufundishaji wa masomo hayo kwa vitendo utaongeza uelewa,umahiri na 
ufaulu katika masomo ya sayansi,hatua ambayo itawezesha taifa kupata 
wataalamu waliobobea katika Sayansi.
“Programu hiyo utakwenda sanjari 
na ujenzi wa maabara katika shule za serikali za kata na utaongeza ari 
ya wanafunzi kupenda masomo ya Sayansi”alisema dkta Masika.

No comments:
Post a Comment