TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, January 22, 2015

ATC KUANZISHA PROGRAMU YA SAYANSI ZA MAABARA

indexMahmoud Ahmad Arusha

Chuo cha Ufundi Arusha(ATC) kinatarajiwa kutoa wahitimu wengi wa program ya teknolojia ya sanyansi za maabara ili kupata wataalamu wa kufundishia masomo ya sayansi kwa skuli za sekondari.
Hayo ni miongoni mwa ahadi za Mkuu wa Chuo hicho dkta Richard Masika wakati wa mahafali ya sita ya Chuo hicho yaliofanyika jijini hapa hivi karibuni.
Katika taarifa yake hiyo kwa naibu waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi Jenista Mhagama alisema kwa miaka mingi kuna upungufu wa walimu wengi wa masomo ya sanyansi na wataalamu wa masuala ya maabara katika skuli za sekondari.
Alisema hali hiyo inathiri kwa kiwango kikubwa ufundishaji wa masomo ya Sayansi kwa wafunzi wanaochukwa masomo hayo na kushindwa katika ufaulu kwa kukosa walimu wenye ubora.
“ kutokana kutambua hali hiyo chuo kikaamua kuanzisha mpango huo ilikuwapata wataalamu wengi zaidi ili kwenda sambamba na kupanuka kwa ujenzi wa sekondari hapa nchini”alitanabaisha dkta Masika.
Alisema kuwa skuli zinahitaji waalimu wengi zaidi wa masomo ya sayansi na wataalamu wa maabara,hivyo kwa kutambua umuhimu huo ndio maana tuanzisha mpango huo.
Alisema kuwa kutokana na chuo kutambua umuhimu huo ndio maana kikaanzisha Programu hiyo wa kutoa wataalamu hao wa maabara ilikuendana na mpango wa serikali wa matokeo makubwa sasa.
Pia alisema kutokana na hatua hiyo ufundishaji wa masomo hayo kwa vitendo utaongeza uelewa,umahiri na ufaulu katika masomo ya sayansi,hatua ambayo itawezesha taifa kupata wataalamu waliobobea katika Sayansi.
“Programu hiyo utakwenda sanjari na ujenzi wa maabara katika shule za serikali za kata na utaongeza ari ya wanafunzi kupenda masomo ya Sayansi”alisema dkta Masika.

No comments:

Post a Comment