TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, January 23, 2015

SMZ yasaidia nyumba za kurekebisha tabia (Sober House)

indexNA ALI ISSA/MAELEZO ZANZIBAR 

Waziri wa nchi Ofisi ya Mkamu wa pili wa Rais Fatuma Abdullhabibi Fereji amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzbar imekuwa ikizisaidia nyumba za kurekebisha tabia (Sober house) kwa kuzipatia ruzuku ya fedha kila mwaka ya kuendesha nyumba hizo ili kuona vijana wao wanabadilika kitabia.
Hayo ameyasema leo huko Baraza la Wakilishi Zanzibar wakati akijibu suali la Mjumbe wa Wawi Saleh Nassor Juma alietaka kujua kama Serikali inajua kuwepo kwa nyumba za kurekebisha tabia kwa miongozo ya dini ya kiislamu na vipi Serikali inazisaidia nyumba hizo.
Fatma Ferej alisema kuwa Serikali inajua kuwepo kwa nyumba hizo na wanazipatia ruzuku ijapo kuwa kwa kiwango kidogo kulingana na bajeti inayopatikana.
Alisema uendeshaji wa nyumba hizo hufuatia hatua kumi na mbili za kiislamu ambapo hutambulika kuwa ni “Milat Islam”na hatua hizo zimeletwa hapa Zanzibar kuazia mwaka 2009 baada ya wafanyakazi wa tatu wa na kijana mmoja aliepata nafuu baada ya kupata mafunzo huko Marekani.
Waziri huyo aliziomba Taasisi za kiislamu kuzitembelea nyumba hizo kwa kutoa michango yao na daawa itakazowapelekea vijana wanaoishi nyumba hizo kujitambua na kubadili tabia
Alisema vijana hao wanahitaji kila aina ya huduma kwani ni watoto wao ambao walijiingiza katika tabia zisizo nzuri, hivyo kuwasaidia na kuwaelimisha ni kulijengea taifa mstakabali mwema wa vijana hao..
Alisema kuna baadhi ya wazzee kuwatupa watoto hao na kuwazarau kwa vile walitumbukia katika janga baya, lakini alisema kufanya hivyo ni kosa na jambo linalohitajika ni ushiriiano wa pamoja kati ya wananchi, Serikali na Taasisi nyengine wakiwemo wakilishi na wabunge.

No comments:

Post a Comment