Waziri wa nchi Ofisi ya Mkamu wa 
pili wa Rais Fatuma Abdullhabibi Fereji amesema kuwa Serikali ya 
Mapinduzi ya Zanzbar imekuwa ikizisaidia nyumba za kurekebisha tabia 
(Sober house) kwa kuzipatia ruzuku ya fedha kila mwaka ya kuendesha 
nyumba hizo ili kuona vijana wao wanabadilika kitabia.
Hayo ameyasema leo huko Baraza la 
Wakilishi Zanzibar wakati akijibu suali la Mjumbe wa Wawi Saleh Nassor 
Juma alietaka kujua kama Serikali inajua kuwepo kwa nyumba za 
kurekebisha tabia kwa miongozo ya dini ya kiislamu na vipi Serikali 
inazisaidia nyumba hizo.
Fatma Ferej alisema kuwa Serikali 
inajua kuwepo kwa nyumba hizo na wanazipatia ruzuku ijapo kuwa kwa 
kiwango kidogo kulingana na bajeti inayopatikana.
Alisema uendeshaji wa nyumba hizo 
hufuatia hatua kumi na mbili za kiislamu ambapo hutambulika kuwa ni 
“Milat Islam”na hatua hizo zimeletwa hapa Zanzibar kuazia mwaka 2009 
baada ya wafanyakazi wa tatu wa na kijana mmoja aliepata nafuu baada ya 
kupata mafunzo huko Marekani.
Waziri huyo aliziomba Taasisi za 
kiislamu kuzitembelea nyumba hizo kwa kutoa michango yao na daawa 
itakazowapelekea vijana wanaoishi nyumba hizo kujitambua na kubadili 
tabia
Alisema vijana hao wanahitaji kila
 aina ya huduma kwani ni watoto wao ambao walijiingiza katika tabia 
zisizo nzuri, hivyo kuwasaidia na kuwaelimisha ni kulijengea taifa 
mstakabali mwema wa vijana hao..
Alisema kuna baadhi ya wazzee 
kuwatupa watoto hao na kuwazarau kwa vile walitumbukia katika janga 
baya, lakini alisema kufanya hivyo ni kosa na jambo linalohitajika ni 
ushiriiano wa pamoja kati ya wananchi, Serikali na Taasisi nyengine 
wakiwemo wakilishi na wabunge.

No comments:
Post a Comment