TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, January 23, 2015

POSHO ZA POLISI KWA AJILI LIKIZO ZIONGEZWE

indexNa Ali Issa Maelezo Zanzibar

WAZIRI wa n Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Muhamed Abuod Mohamed amesema atamuandikia barua Waziri wa Mambo ya Ndani wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Mathias Chikawe kuongeza fedha za usafiri kwa askari wa Jeshi la Polisi mara baada ya kustaafu na kurejea makwao.
Hayo ameyasema leo huko Baraza la Wawakilishi Chukwani wakati akijibu suali la nyongeza la Mwakilishi wa Jimbo la Wawi Saleh Nassor Juma alietaka kujua sababu za askari polisi anapostaafu kulipwa shilingi 66,000 kwa ajili ya nauli yake na kusafirisha mizigo kwa masafa ya kilomita 20 kiwango ambacho ni kidogo na hakikidhi haja.
Waziri Aboud amesema kutokana na kadhia hiyo atalazimika kuandika barua kwa Waziri Nchimbi kuliangalia suala hilo ili kulitafutia ufumbuzi na kuwaondoshea shida asikari hao wanapostaafu.
Aidha Waziri huyo alisema kuwa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar jukumu lake ni kuratibu masuala ya Muungano na kazi ya usimamizi iko chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani.`
Waziri Aboud akitoa ufafanuzi wa madai ya askari watatu waliostaafu kutoka Mkoa wa Kaskazini Unguja ambapo ilielezwa kuwa walipewa milioni 16 ili kurudi makwao kwamba taarifa hiyo sio kweli.
Alisema ana elewa kuwepo kwa askari hao na kusema askari anapostaafu hutaarishiwa usafiri wa mizigo pamoja na familia zao hadi makwao jambo ambalo hufanyika kwa kutegemea mstaafu alikuwa na cheo gani.
Baada ya ufafanuzi huo alisema kuwa Kamishna wa Polisi aliwaita askari hao ofisini kwake na kuwafahamisha utratibu ulivyo,na askari hao baadae waliridhika.

No comments:

Post a Comment