WAZIRI wa n Nchi Ofisi ya Makamu 
wa Pili wa Rais Muhamed Abuod Mohamed amesema atamuandikia barua Waziri 
wa Mambo ya Ndani wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Mathias Chikawe 
kuongeza fedha za usafiri kwa askari wa Jeshi la Polisi mara baada ya 
kustaafu na kurejea makwao.
Hayo ameyasema leo huko Baraza la 
Wawakilishi Chukwani wakati akijibu suali la nyongeza la Mwakilishi wa 
Jimbo la Wawi Saleh Nassor Juma alietaka kujua sababu za askari polisi 
anapostaafu kulipwa shilingi 66,000 kwa ajili ya nauli yake na 
kusafirisha mizigo kwa masafa ya kilomita 20 kiwango ambacho ni kidogo 
na hakikidhi haja.
Waziri Aboud amesema kutokana na 
kadhia hiyo atalazimika kuandika barua kwa Waziri Nchimbi kuliangalia 
suala hilo ili kulitafutia ufumbuzi na kuwaondoshea shida asikari hao 
wanapostaafu.
Aidha Waziri huyo alisema kuwa 
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar jukumu lake ni kuratibu masuala
 ya Muungano na kazi ya usimamizi iko chini ya Wizara ya Mambo ya 
Ndani.`
Waziri Aboud akitoa ufafanuzi wa 
madai ya askari watatu waliostaafu kutoka Mkoa wa Kaskazini Unguja 
ambapo ilielezwa kuwa walipewa milioni 16 ili kurudi makwao kwamba 
taarifa hiyo sio kweli.
Alisema ana elewa kuwepo kwa 
askari hao na kusema askari anapostaafu hutaarishiwa usafiri wa mizigo 
pamoja na familia zao hadi makwao jambo ambalo hufanyika kwa kutegemea 
mstaafu alikuwa na cheo gani.
Baada ya ufafanuzi huo alisema 
kuwa Kamishna wa Polisi aliwaita askari hao ofisini kwake na 
kuwafahamisha utratibu ulivyo,na askari hao baadae waliridhika.

No comments:
Post a Comment