TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, January 19, 2015

Vijana waendelea kupata ajira katika Utumishi wa Umma

unnamedKatibu Msaidizi Idara ya Ajira kutoka Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Malimi Muya akiwaeleza waandishi wa Habari leo jijini Dar es salaam (hawapo pichani) sababu zinazopelekea Vijana wengi kupenda kufanya kazi katika Utumishi wa Umma ikiwemo uboreshaji wa mishahara,kuboreshwa kwa mazingira ya kazi,usalama wa kazi unaotokana na kuwepo kwa taratibu za kazi zinazotabirika ,kuwepo kwa taratibu maalum zinazomhakikishia mwajiriwa maslahi au malipo bora baada ya kuhitimisha ajira yake.kushoto ni Afisa Habari wa Sektetarieti hiyo Bw. Kassim Nyaki na kulia ni Afisa Habari wa Idara ya Habari Maelezo Bw. Frank Mvungi. unnamed1Afisa Habari toka Ofisi ya Rais Sektetarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Kassim Nyaki akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam,Katikati ni Katibu Msaidizi Idara ya Ajira kutoka Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Malimi Muya na kulia ni Afisa Habari wa Idara ya Habari Maelezo Bw. Frank Mvungi.           
unnamed3Baadhi ya Waandishi wa Habari wakimsikiliza Katibu Msaidizi Idara ya Ajira kutoka Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Malimi Muya leo jijini Dar es salaam wakati wa mkutano uliolenga kutoa taarifa ya mafanikio ya Sekretarieti hiyo ikiwemo kuwapangia vituo vya kazi jumla ya waombaji kazi 12,858 walioshinda usaili kufikia Novemba 2014.
(Picha zote na Idara ya Habari Maelezo )
……………………………………………………………………………………
Frank Mvungi- Maelezo Serikali imewapangia vituo vya kazi waajiriwa 12,858 katika Utumishi wa Umma kufikia Novemba mwaka 2014 ambao walifuzu usaili kupitia Ofisi ya Rais Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma. Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Katibu Msaidizi Idara ya Ajira kutoka Sekretarieti hiyo Bw. Malimi Muya wakati wa mkutano na Waandishi wa habari uliolenga kueleza mafanikio ya Sekretarieti hiyo hadi mwishoni mwa mwaka jana. Akizungumzia suala la maombi ya ajira yaliyowasilishwa katika Sekretarieti hiyo, Muya alibainisha kuwa jumla ya barua za maombi 191,844 zilifikishwa na kupokelewa na Sekretarieti hadi Septemba 2014 ambapo jumla ya waombaji 71,124 walikidhi vigezo na waliitwa kwenye usaili baada ya uchambuzi kufanyika. “Kati ya waombaji 71,124 waliotwa kwenye usaili huo, ni waombaji 12,858 ndio waliofuzu na waliopangiwa vituo vya kazi ambapo wanaume walikuwa 7,598 sawa na asilimia 59.1 na wanawake walikuwa 5,260 sawa na asilimia 40.9.” alisisitiza Muya. Aidha kati ya waajiriwa 12,858 waliopangiwa vituo vya kazi Muya alibainisha kuwa Vijana wenye umri kati ya miaka 21-25 ni 1045 sawa na asilimia 8.1 wenye umri kati ya miaka 26-30 ni 6,346 sawa na asilimia 49.4 ambapo kati ya mwaka 2010 hadi 2014 utumishi wa umma umeajiri 57.5 ya vijana wenye umri wa miaka 21-30. Akizungumzia sababu zinazowavutia na kuwasukuma vijana kuingia katika Utumishi wa Umma, Muya alisema kuwa uboreshaji wa mishahara, kuboreshwa kwa mazingira ya kazi, usalama wa kazi unaotokana na kuwepo kwa taratibu za kazi zinazotabirika ndizo mojawapo ya sababu zinazowavutia vijana wengi kuomba kazi katika utumishi wa umma.. Sababu nyingine zinazowavutia vijana kupenda kuajiriwa katika utumishi wa umma ni kuwepo kwa mabadiliko ya mara kwa mara ya kanuni na taratibu za kazi zinayofanywa kukidhi mahitaji ya watumishi kwa wakati unaohusika, kuwepo kwa taratibu maalum zinazomhakikishia mwajiriwa maslahi bora baada ya kuhitimisha ajira yake. Akizungumzia kada zenye fursa pana ya ajira, Muya alisema kuwa kada ya gesi, petrol, Madaktari wa mifugo, wahandisi, na mafundi mchundo katika sekta za maji,umeme na afya,hivyo kuwataka vijana kusoma masomo ya Sayansi. Aidha Muya alitoa wito kwa wale wote ambao wameshapangiwa vituo vya kazi katika Utumishi wa Umma kujituma, kuwa wabunifu katika sehemu zao za kazi kwani Taifa linawategemea vijana katika kufikia maendeleo endelevu kwa manufaa ya sasa na ya baadae. Kwa upande wake Afisa Habari wa Sekretarieti hiyo Bw. Kassim Nyaki alibainisha kuwa waombaji kazi waliofanya usaili mwezi Desemba, 2014 kuwa waliofaulu na kupangiwa vituo vya kazi jumla yao ni 572 ambapo watapangiwa vituo hivyo kabla ya mwisho wa mwezi Januari 2015.

No comments:

Post a Comment